Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Habari za Kitaifa na Kimataifa


AGIZO LA NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI KWA JESHI LA POLISI NA SUMATRA KUFANYA UKAGUZI WA KINA KWENYE VYOMBO VYA USAFIRISHAJI KABLA YA KUPEWA LESENI ITAKUWA NI KIINI MACHO

Katika maisha yetu ya kila siku, kuna misemo mbalimbali ambayo hupenda kuitumia kama miongozo, msisitizo, onyo na pengine kejeli kwa jamii husika. Kwa mfano, kuna methali inayosema, 'Kawaida ni Kama Sheria', 'Kamba Hukatika Pembemba, 'Kukunjua Makucha', 'Mwenye Macho Haambiwi Tazama'. Kila mmoja wapo ya msemo huu, una maana ndani yake.Labda kidogo tu niegemee kwenye msemo huu, 'Kawaida ni Kama Sheria', natumai kila mmoja wetu au wachambuzi wa masuala ya lugha wanaweza kutoa tafsiri zao kulingana na upeo na uzoefu wao wa kila siku katika uchambuzi wa lugha. Msemo huu, upo wazi kabisa. Kwa maana kuwa, kuna mambo ambayo yanafanyika mara kwa mara katika jamii yetu. Kutokana na kufanyika huko, basi jamii huamua kuhalalisha na kuwa mambo ya kawaida.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Ndugu Pereira Ame Silima, si mgeni hapa Tanzania. Natumaini kuwa unaufahamu vizuri msemo huu. Suala la tatizo la rushwa kwa jeshi la polisi hususani katika kitengo cha Trafiki ni jambo la kawaida. Lakini, Bwana Silima atambue kuwa, Tanzania inanuka rushwa ya hali ya juu. Takwimu za the East Africa Bribery Index (EABI) ya mwaka 2011, Tanzania ilishika nafasi ya 3 kwa kiwango cha juu cha rushwa, katika eneo la Afrika Mashariki, huku Burundi ikiwa ya Kwanza, na Uganda ya Pili. Hali kadhalika Jeshi la Polisi katika nchi zote za Afrika Mashariki, lilishika nafasi ya Kwanza. Kwa kifupi, unaweza kuona namna rushwa ilivyoshamiri katika jeshi la polisi.

Kuna msemo mwingine ambao umeenea katika jamii yetu, ambao unasema kuwa, Mpe Mchawi Akulelee Mwana (Mtoto). Hii ina maanisha kuwa, kwa sababu mtu mchawi ana tabia ya kuua watu, ukimpatia mtoto akulelee hawezi kumwua. Hali ni tofauti katika Jeshi la Polisi na hasa kitengo cha Trafiki, licha ya kubainika wazi kuwa wamekithiri kwa vitendo vya rushwa, na wanaipokea kila siku, bado watendaji hawa wa serikali, kama Naibu Waziri, wanarikirimu mamlaka na madaraka makubwa kama ya kufanya ukaguzi kwenye vyombo vya usafiri ili viweze kupatiwa leseni. Hii ni sawa na kumweka mbuzi mdomoni mwa Simba. Ule msemo wa 'mpe mchawi akulelee mwana', haupaswa kutumika kwa Jeshi la Polisi, hususani kitengo cha Trafiki, kwenye suala muhimu kama hili la kufanya ukaguzi ili leseni za usafirishaji zitolewe. Hapa, hata ukimpa mchawi mtoto akulelee, atamwua tu. Waziri atambue kuwa misemo nayo inaenda kwa wakati. Huu si wakati wake tena kuutumia msemo huu.

SUMATRA kama wanavyojiita kuwa ndio wenye mamlaka ya kudhibiti vyombo vya usafiri nchi kavu na majini, hawana tofauti na Trafiki. Mfano mdogo tu ni kuzama mfululizo kwa boti za abiria kutoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar na kutoka Zanzibar kwenda Pemba (MV Spice Islander na MV Skagit). Ndani ya miezi 10, zaidi abiria mia tatu (300) idadi iliyotolewa na serikali, waliweza kupoteza maisha, huku takwimu halisi za abiria waliopenda katika vyombo hivyo vya majini wakishindwa kujulikana. Hakuna hatu mtu mmoja ambaye ameweza kuwajibika au kuwajibishwa na mamlaka husika. Kuzama kwa Meli hizi, kumetokana na uzembe wa hali ya juu kwa mamlaka zote zinazohusika na usalama wa majini kwa vyombo ya usafiri, hususani hawa jamaa wa SUMATRA. Matukio ya kuzama kwa meli hizi mbili kunafanana kabisa. Ni vyema matamshi na kauli zao zikawa zinatathmini matukio haya yanayoendana na usalama wa abiria.

SUMATRA walijitetea kuwa hawahusiki kwa upande Zanzibar, lakini watambue kuwa wanahusika na usafiri wa majini. Kuhusika wanahusika tu kwa sababu watanzania wengi walipoteza maisha yao, huku wao wakikwepa majukumu ya msingi. Kifupi, SUMATRA hawana jipya kwenye sekta hii ya usafirishaji wa abiria. Wanachofanya ni kujinufaisha tu. Kama wanapinga, hebu nenda pale Ubungo Bus Terminal uone hali ilivyo. Kwa maisha ya sasa ya kisasa na kiteknolojia, tulitegemea Stendi Iboreke kwa kuwa na Maeneo Mengi ya Kupunguzikia Abiria nyakati zote, za masika na kiangazi, Viti vya kukaa abiria maeneo mbalimbali, angalau hata vile vilivyojengwa kwa tofali na kusilibwa na simenti.

Majengo yaliyojengwa enzi ya Nyerere, yamebaki magofu, na sasa wameamua kuegeshea magari. Stendi ni Chafu Mno. Ukiritimba, ubabe na unyanyaji na kupora pesa za waendesha vyombo vya usafiri ndiyo dili. Wao wameegemea kusimamia pesa tu za kwenye mabasi. Hawaangalie hali duni za stendi pamoja na huduma zake.

Cha Kusikitisha zaidi, leo tarehe 31 Agosti 2012, Mkurugunzi wa SUMATRA bila hata aibu, ametangaza kuchukua hatua kwa mabasi ambayo yatachimba dawa porini, bila kufikiri ni hatua gani wamezichukua toka Waziri wa Uchukuzi, Mwekyemba alipotoa tamko. Huko porini, ardhi ni ya bure, mawe ni ya bora, miti ni ya bore. SUMATRA wajiulizi ni shilingi ngapi wanazipora toka kwa Wamiliki wa Mabasi ambazo zingejenga vyoo sehemu za mapori, ambapo abiria hujihudumia. Pia, inabidi wajiulize, mtoto mdogo anaweza kusafiri masaa mawili bila kujihudumia? Nadhani hawa wa jamaa wa SUMATRA wana familia, waongee kama binadamu wenye utashi na si kubwatuka tu. Hii ni dhuluma kwa wananchi na wamiliki wa mabasi walipa kodi.

Ninachoweza kujifunza hapa ni kushamiri kwa Rushwa ambayo kwa sasa imefikia katika hatua ya kuwa 'RUSHWA YA MFUMO' kiingereza inaitwa SYSTEMIC CORRUPTION.  Rushwa ya Mfumo inatengenezwa na kulindwa na watu wenye mamlaka. Huuendeshwa kwa misingi ya kutoa matamko na maamuzi yasiyo na fikra wala busara. Maamuzi mengi huwa ni kukurupuka tu bila kuangalia athari na hatari ambazo zinaweza kujitokeza mbele. Rushwa ya Mfumo ni Hatari kwa sababu husababisha kutoamika kwa watu wale ambao wanapaswa kutoa maamuzi mazito kwa maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla.

Maamuzi wengi yanayotolewa na Watendaji na Wanasiasa wasiojali maslahi ya taifa na wananchi kwa ujumla yanakuwa katika misingi ya Rushwa ya Kimfumo. Ndiyo maana pale mwanzo niliuliza, unaweza kumweka Mbuzi karibu/mdomoni mwa Simba na ukategemea mbuzi huyo akaendelea kuwa hai? Haya ndiyo masuala ya msingi tunapaswa kuhoji kabla ya kutoa matamko na matangazo kwa umma wa Watanzania.

Kitengo cha Naibu Waziri kuwaagiza Polisi na SUMATRA kufanya ukaguzi wa vyombo vya usafiri kabla ya kupewa leseni za biashara ya kusafirisha biashara, binafsi naona una walakini/tatizo kubwa. Idara Mbili hizo, binafsi zina imani nazo. Pia, nimebaini kuwa zimeshindwa kuonesha weledi na umahiri katika kusimamia huduma za usafirishaji wa abiria, pamoja na suala zima la haki za abiri, usalama wake, na pia maslahi ya abiria wanapokuwa kwenye vituo vya mabasi kabla ya kusafiri na baada ya kuwasili kwenye vituo vingine.

Kwa mfano, kushamiri na kukifiri kwa matuta kwenye barabara kubwa ambazo zinasafirisha maelfu ya abiria ni hatari kubwa kwa usalama wa chombo chenyewe na pia abiria waliomo ndani yake. Kisayansi, ukipima mtikisiko wa basi linaporuka matuta makubwa na madogo kwa umbali wa kilometa 1000, madhara yake ni makubwa mno. Lakini angalia hawa jamaa wanaojiita wasimamizi wa usalama na huduma ya usafiri wa abiria wamekaa kimpya tu. Ni dhahiri, wanaangalia maslahi yao mengine na si usalama wa abiria.

Kwa kutumia kodi za Watanzania, hawa jamaa wanasafiri, lakini hawajifunzi hata kidogo kwenye nchi za wenzetu. Usalama wa barabarani unaendana na sayansi na teknolojia. Nenda tu hapo Afrika Kusini, unaona tofauti kubwa katika nchi hizi za kiafrika. Kwa mfano, Alama za Barabara ni Kubwa mno na hazihitaji mtu kuvaa miwani. Lakini Viashirio vya Barabara kupinda au tukio fulani muhimu huoneshwa kwa Mabango Makubwa, huku umbali unaopungua kufikia tukio hilo, ukionekana kwenye Alama hizo. Kama ulikuwa umbali wa mita 1000 utaendelea kupungua 800m, 600m, 400m, 200m, 100m, 50m. Tuna miti mingi, mbao ndio usisema, mawe ndio, basi, hata kama hatuna chuma, hatuwezi kushindwa. Ka-Alama kabarabara ni kidogo, kimoja, kamejificha, kamefutika. Yaani, ni hatari tu. je utegemee usalama hapa. Tujifunze.

Nimalizie kwa kusema kuwa Naibu Waziri unatoa maelekezo na maamuzi katika mikono isiyo misafi, na utegemee kinyume na matarajio yako, kama kweli ulikuwa na nia ya dhati ya kuwapa haki yao, abiria maskini wa Kitanzania, ambao wamekuwa wahanga wa hii Rushwa ya Kimfumo.

Imendaliwa na:

Kivenule

No comments:

Post a Comment