Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Viponzo na Viburudisho

UGIMBI/KOMONI KIBURUDISHO MURUA CHA KABILA LA WAHEHE
 
Ugimbi ni moja ya pombe ya Kienyeji hususani kwa Kabila la Wahehe, ambayo hutengenezwa kwa kutumia mahindi na ulezi na kuchachishwa na Komba ambalo huwa limeandaliwa kwa kuchanganywa na ulezi. Ugimbi pia hujulikana kwa jina maarufu la KOMBONI. Kwa siku ya kwanza, Ugimbi unapopikwa huwa ni Togwa ya Moto (Nyululu) ambaye huchemshwa kwa wastani wa kutwa nzima. Ikisha iva, huipuliwa na kupozwa, kabla ya kuwekewa Komba. Nyululu kwa kawaida ni tamu na yenye ledha ya usukari. Nyululu togwa ambayo haileweshi. Na kama ulikuwa hajala chakula, ukinywa Nyululu, basi huwa ni Shibe tosha.
 
Ugimbi au Komoni hunywewa Vilabuni, mashambani na majumbani kwa watu wa rika mbalimbali, mfano watoto, watu wazima na watoto ikibidi. Pia ugumbi/komoni hutumika kama kiburudisho kwenye misiba, sherehe na mikutano. Ugumbi kama vinywaji vingine, huwa na wapenzi wake. Mtu yupo tayari kukataa kunywa, soda, bia, au Ulanzi na kuamua kutumia Ugimbi au Komoni. 

Ugimbi au maarufu Komoni huwapo na watu maalum waliojaliwa kuonja Ladha ya Ugimbi kama ni Mtamu au la. Hawa waonja Ugimbi hujipatia umarufu kutokana na kuonja kwao pombe hii. Na mara nyingi hupewa fursa ya kuonja Ugimbi/Komoni sehemu mbalimbali.

Ugimbi ukishapatikana baada ya kuchujwa, machicha yake huhifidhiwa kwa matumizi mengine ya kupata Kileo kinachofanana na Ugumbi. Machicha ya Ugimbi hulowekwa na maji kwa muda kadhaa na kisha huchujwa vizuri. Yale male yanayopatikana baada ya kuchunjwa hayo machicha, hujulikana kama MACHORO. Ladha na thamani ya machoro hutugea ubora wa Komoni au Ugimbi uliokuwa umepikwa mwanzo.
 
Makala hii itaendelea wiki ijayo. Hapo juu ni picha ya Babu ambaye anajiburudisha na Ugimbi. Je unajua hii ni lita ngapi? Pia jiulize, machicha ya pombe yakichujwa bado yanaweza kutumika kama Pombe karibu Iringa ujaribu?

Kipindi kijacho, tutaangalia makala nyingine ya Pombe inayoitwa, Kihambule na namna inavyoandaliwa? Usisahau kuwa pia kuna Ulazi, Wanzuki na mengine mengi.
 
Nyela, Uugimbi Unono!


Imeeandaliwa na:

Adam Kivenule
0713 270364
kivenule@gmail.com
 

No comments:

Post a Comment