Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Friday 20 September 2013

KAUKI KUFANYA JUBILEI YA KUTIMIZA MIAKA 10, KUELEKEA MKUTANO MKUU WA KUMI WA KAUKI-KIDAMALI, IRINGA

KAUKI KUFANYA JUBILEI YA KUTIMIZA MIAKA 10, KUELEKEA MKUTANO MKUU WA
KUMI WA KAUKI-KIDAMALI, IRINGA

Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) unatarajia kufanya Jubilee ya Miaka
10 wakati wa Mkutano Mkuu wa Kumi wa KAUKI utakaofanyika Kidamali,
Iringa mnamo tarehe 28-29, 2014.

Jubilei ya Miaka Kumi inafanyika kwa mara ya kwanza toka kuanzishwa
kwa umoja huu mwaka 2005, Kidamali, Iringa. Sambamba na kufanyika kwa
Jubilei hiyo, pia KAUKI itakuwa inafanya Mkutano Mkuu wa 10 tangu
kuanzishwa kwake.

Akizungumza na mwandishi wa Blogu hii, Katibu Mkuu wa KAUKI Ndugu Adam
Alphonce Sigatambule Kivenule, alibainisha kuwa, ni kweli tumefikisha
miaka kumi na tarehe hiyo ya Mkutano Mkuu itakuwa pia siku ya Jubilei
yetu.

HISTORIA YA KAUKI
Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI), ulianzishwa tarehe 18 Desemba 2005
wakati wa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa KAUKI uliofanyika Kijijini
Kidamali. KAUKI ilianzishwa kutokana na mashauriano ya Ndugu watatu,
yaani Faustino Sigatambule Kivenule, Christian John Kivenule na Adam
Alphonce Kivenule.

Ndugu hawa watatu baada ya kubaini mapungufu yaliyokuwapo ndani ya
Ukoo wa Kivenule, waliamua kuungusha nguvu zao na kisha kuushirikisha
ukoo kuhusiana na adhima yao ya kutaka kuirudisha jamii ya ukoo wa
Kivenule kuwa pamoja.

Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Mashauriano ulifanyika Jijini Dar es Salaam,
mnamo tarehe 06 Februari 2005 katika Ukumbi wa Riverside uliopo eneo
la Ubungo, ambapo ndugu zaidi ya 15 walihudhuria.

Matokeo ya Kikao hiki yaliazimia kwa kauli moja, kulishirikisha wazo
la kuandaliwa kwa MKUTANO MKUU WA KWANZA WA UKOO, kwa ndugu zao
wanaoishi maeneo ya Magubike, Kidamali, Nyamihuu, Ilalasimba, Idete,
Ibogo, Nzihi na Iringa Mjini.

Kukubalika kwa wazo hili ndiko kulikopelekea kufanyika kwa Mkutano
Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule, mnamo tarehe 17 -18 Desemba 2005,
Kijijini Kidamali, Mkoani Iringa.

Tokea wakati huo, Mikutano ya KAUKI imekuwa ikifanyika kila mwaka.
Takwimu zilizopo zinaonesha kuwa, Mikutano 9 ya KAUKI imefanyika
maeneo mbalimbali ya Kanda za KAUKI kama inaoneshwa hapa chini:
Kanda ya Kidamali – Mikutano ya KAUKI 3
Kanda ya Magubike – Mikutano 2
Kanda ya Irore – Mkutano 1
Kanda ya Nduli – Mkutano 1
Kanda ya Mufindi – Mkutano 1
Kanda ya Dar es Salaam – Mkutano 1

Kwa KAUKI haya ni matokeo ya Kujivunia kwa sababu siyo rahisi
kufanyika kwa mikutano ya namna kutokana na kuwa na gharama kubwa.

MAFANIKIO YA KAUKI
KAUKI imefanikiwa kufanya yafuatayo kwa maendeleo ya wana-ukoo. Kwa mfano,
Imeanzisha Blogu zake kwa ajili ya upashanaji habari. Anuani za blogu hizo ni:
http://www.tagumtwa.blogoak.com
http://www.kauki-kauki.blogspot.com
http://www.tagumtwafoundation.wetpaint.com

Hali kadhalika, blogu inayomilikiwa na ndugu Adam Kivenule, ambaye pia
ni Katibu Mkuu wa KAUKI imekuwa ikisaidia katika suala nzima
usambazaji na upashanaji wa habari za KAUKI. Anuani ya blogu hiyo ni:
http://www.adamkivenule.blogspot.com
KAUKI pia imefanikiwa kufungua Ukurasa wa Facebook wenye anuani ifuatayo:
http://www.facebook.com/kivenule
KAUKI pia imefungua ukurasa wa TWITTER http://www.twitter.com/kivenule
Sambamba na mafanikio hayo, kwa sasa KAUKI ipo katika mchakato wa
kufungua ofisi yake KAUKI huko Kidamali, Iringa.

Hali kadhalika, unaweza kuwasiliana na viongozi wa KAUKI au ofisi ya
KAUKI kwa kutumia anuani zifuatazo:
kauki2006@gmail.com
tagumtwa@gmail.com
tagumtwa.kauki@gmail.com
kivenule@gmail.com
kivenule@live.com

Kuna masuala mengi ambayo bado yanaendelea kushuhudiwa na wana-KAUKI,
pamoja na jamii kwa ujumla. Mafanikio ya Ujumla ni kuendelea kufanyika
kwa mikutano mikuu ya KAUKI katika kanda zake. Hali kadhalika mwitikio
na ushiriki wa Wana-KAUKI katika mikutano hiyo ni mafanikio tosha.

Kuelekea kufanyika kwa Jubilei ya KAUKI, mambo mengi yanatarajiwa
kufanyika kwa lengo la kuhakikisha kuwa, Mkutano Mkuu wa KAUKI unafana
na kufanikiwa.

Sunday 15 September 2013

KAUKI KUFUNGUA OFISI YAKE KIDAMALI

KAUKI KUFUNGUA OFISI YAKE KIDAMALI

Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) upo katika mchakato wa kufungua
ofisi yake katika Kijiji cha Kidamali, Mkoani Iringa. Mpango wa
kufungua ofisi ni wa muda mrefu na ulikuwa bado kukamilika kutokana na
matatizo mbalimbali ya kifedha yanayoukabili umoja huo.

Akizungumza na mwandishi wa blogu ya KAUKI, Mwenyekiti wa KAUKI Ndugu
Faustino Sigatambule Kivenule, alisema kuwa, baada ya kuchaguliwa
kuongoza umoja huo kwa kipindi cha miaka mitatu (2013-20160,
atahakikisha ofisi inafunguliwa, inakuwa na vifaa na inafanya kazi,
kama mipango ya KAUKI inavyojieleza.

Mwenyekiti wa KAUKI aliongeza kuwa, kwa muda mrefu suala la ofisi
limekuwa likizungumzwa bila kutekeleza. Sasa imefika hatua ya
kuhakikisha kuwa ofisi hiyo inafunguliwa na kuendelea kufanya kazi
kikamilifu.

Akiongezea, Katibu Mkuu wa KAUKI, Ndugu Adam Alphonce Kivenule,
alimweleza mwandishi kuwa hatua zilizochukuliwa na uongozi mpya
uliochaguliwa mwaka 2013 katika Mkutano Mkuu wa 9 wa KAUKI,
uliofanyika katika Kijiji cha Magubike, Mkoani Iringa, ni kuhakikisha
kuwa, chumba/nyumba ya ofisi inapatikana mapema iwezekanavyo.

Hadi muda huu ninapozungumza na wewe mwandishi, Chumba cha ofisi kipo
tayari. Kuhusiana na vifaa vya ofisi, Ndugu Adam amesisitiza kuwa
jitihada za makusudi zimekuwa zikifanyika toka mwezi wa Julai 2013
hadi sasa, za kuhakikisha kuwa vifaa vya ofisi vinapatikana.

Vifaa ambavyo vipo na ahadi kwa mujibu wa takwimu zilizopo katika
ofisi ya KAUKI ni kama ifuatavyo:
Kochi la watu watatu (lipo Dar es Salaam)
Mafaili ya ofisi
Machapisho
Mapazia ya ofisi
Stepla mashine na pini zake
Punchi mashine
Meza
Stuli

Hali kadhalika kuna ahadi na fedha taslimu kwa ajili ya ununuzi wa
Kompyuta ya ofisi. Fedha taslimu ambayo tayari imepokelewa ni shilingi
15,000/=. Pia uongozi wa KAUKI kanda ya Dar es Salaam ulipokea ahadi
ya shilingi 50,000/= kutoka kwa mwana-KAUKI.

Jitihadi za ukusanyaji michango mbalimbali kwa ajili ya ofisi na
maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI bado zinaendelea katika
Kanda mbalimbali. Taarifa zilizopatikana kutoka kwa Makamu Katibu
anayetoka kanda ya Magubike, Iringa, anasema kuwa wapo katika mchakato
wa kukusanya michango ya ofisi pamoja na ununizi wa kompyuta ya ofisi.

Hali kadhalika, Kanda ya Kidamali nayo haipo nyuma katika
kulishughulikia suala hili. Mipango kabambe bado inaendelea ili
kuhakikisha kuwa vifaa vya ofisi vinapatikana kwa wakati.

Kwa mujibu wa takwimu za kiofisi kutoka kwa Katibu Mkuu wa KAUKI,
Ndugu Adam Kivenule, ilipangwa kila Kanda ichangie shilingi 35,000/-
kwa ajili ya ununuzi. Pamoja na kuwepo kwa mkakati huu, pia wana-KAUKI
kutoka katika kanda zao waliombwa kuchangia vifaa mbalimbali vya ofisi
kwa maana ya kusaidia kupunguza gharama ya ununuzi wa vifaa hivyo.

Kama ilivyoelezwa hapo juu, mwitikio umekuwa siyo mzuri sana japo bado
tunaendelea kuhimiza wana-KAUKI kuendelea kuchangia vifaa vya ofisi,
hata vya gharama ndogo.

Uongozi wa KAUKI unaamini kuwa hadi mwezi Desemba mwaka huu, ofisi
itakuwa imekamilika, huku ikiwa na vifaa muhimu vya kiofisi.