Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Friday 21 September 2012

PICHA ZA MATUKIO KATIKA MIKUTANO YA MHE. MBUNGE KATA YA MAKUBURI

CHADEMA YAZINDUA MISINGI KATA YA MAKUBURI KAMA SEHEMU YAKE YA OPERESHENI YA M4C

Zifuatazo ni baadhi ya picha za matukio katika ufunguaji wa misingi ya CHADEMA kata ya Makuburi, Jimbo la Ubungo, kama ilivyopigwa picha na mwandishi wetu.


Hapa eneo la River Side ambapo Msingi wa CHADEMA katika Kata ya Makuburi, ulihitimisha ziara ya Mhe. Mbunge Mnyika


Hapa eneo la Ubungo Kibangu Transforma karibu kabisa na Kibangu Medium School and Kanisa la Mzee wa Upako, Anthony Lusekelo, muda mfupi baada ya Mheshimiwa Mbungu kufungua msingi wa CHADEMA

Hapa ni Ubungo Kibangu, Tranforma

Mhe. Mbunge akiwasili katika viwanja vya River Side

Baadhi ya Viongozi wa CHADEMA wa Kata ya Makuburi pamoja na Mhe. Mbunge

Alama ya Chama cha CHADEMA ya Vuguvugu la Mabadiliko (Movement for Change)

Mhe. Diwani wa Kata ya Ubungo akiwasalimu wananchi na wanachama wa CHADEMA

Mhe. Mbunge, John Mnyika akiwahutubia wananchi wa eneo la Kata ya Makaburi hasa wakazi wa River Side

Mhe. Mbunge, John Mnyika akiwahutubia wananchi wa eneo la Kata ya Makaburi hasa wakazi wa River Side

Mhe. Mbunge, John Mnyika akiwahutubia wananchi wa eneo la Kata ya Makaburi hasa wakazi wa River Side

Wananchi toka sehemu mbalimbali katika Kata ya Makuburi walijitokeza kumwuliza maswali Mhe. Mbunge, ambapo baadaye aliweza kuyajibu maswali yao.


Carolyn Kivenule hakuwa mbali katika kumsikiliza Mhe. Mbunge, John Mnyika akiwahutubia wananchi wa eneo la Kata ya Makaburi hasa wakazi wa River Side

Mandhari ya eneo la Ubungo RiverSide, mara baada ya kukamilika kwa ukumbi wa kisasa wa Sherehe mbalimbali

Mhe. Mbunge, John Mnyika akiwahutubia wananchi wa eneo la Kata ya Makaburi hasa wakazi wa River Side

M4C JIMBO LA UBUNGO


CHADEMA YAZINDUA MISINGI KATA YA MAKUBURI KAMA SEHEMU YAKE YA OPERESHENI YA M4C

Na mwandishi wetu,

Mheshimiwa John Mnyika, Jumamosi ya tarehe 15 mwezi Septemba 2012, alikuwa na kazi nzito ya kufungua misingi katika Jimbo la Ubungo, hususani katika kata ya Makuburi. Akihitimisha ziara yake ya ufunguzi wa misingi, pamoja na kuhutubia mikutano mbalimbali ya hadhara, huku akijibu hoja mbalimbali zilizowasilishwa na wananchi. 

Mheshimiwa Mnyika aliwaeleza wakazi wa Jimbo la Ubungo kuhusiana na shughuli ambazo wamezifanya toka walipochaguliwa. Akiongozana na Madiwani wa Kata ya Ubungo na Kata ya Makuburi, alitoa fursa kwa wananchi kuuliza maswali mbalimbali ambayo baadaye aliyajibu kikamilifu.  

Mojawapo ya maswali yaliyoulizwa ni pamoja na tatizo la matapeli ambao wapo eneo la daraja la Ubungo, kwenye mitambo ya TANESCO, na jinsi polisi wa wa kituo cha Kata cha Ubungo RiverSide wanavyofumbia macho uhalifu huo na kuwakumbatia wahalifu, na namna watu wanavyotapeliwa na mateli hao.  

Akijibu hoji hiyo, Mhe. Mnyika aliwapa jukumu Madawani kulifuatilia kwa karibu suala hilo na kisha kumfahamisha hatua ambazo zimekwisha chukulia. Akiongezea, alisema, yeye kama Mbunge, anapambana na mtu kama Mkuu wa Jeshi la Polisi, Polisi wa Operesheni Mbalimbali na si polisi wa kituo cha polisi cha Kata.  

Kuhusu ujenzi wa daraja na barabara ya Mabibo External na Ubungo Maziwa, alisema, tayari mipango yote kuhusiana na kuanza ujenzi huo imekwisha kamilika. Kinachosubiliwa ni kuona kama kutakuwa na fungu la kuwalipa fidia watu waliofuatwa na barabara.  

Mwishoni mwa mkutano huo uliofanyika eneo la Riverside kwenye Kijiwe cha Taksi, Mhe. Mbunge alihitimisha ziara yake kwa kufungua msingi na kupandisha Bendera Mbili.

 

 

 

 

WIKI NENDA KWA USALAMA, CHANGAMOTO INAYOKUA KWA KWA KASI KWA WAENDESHAJI NA WATUMIAJI WA VYOMBO VYA USAFIRI

Wimbi la ongezeko la ajali za barabarani ni changamoto hususani kwa wadau na vyombo vinavyosimamia usalama barabarani na Wiki ya Nenda kwa Usalama. Kuthibitisha hili, shuhudi baadhi ya matukio ya ajali yaliyotokea sehemu mbalimbali hapa Tanzania.







 

WIKI NENDA KWA USALAMA, CHANGAMOTO INAYOKUA KWA KWA KASI KWA WAENDESHAJI NA WATUMIAJI WA VYOMBO VYA USAFIRI, MIUNDOMBINU NA WADAU WA USIMAMIZI
 
Angalia mlolongo wa picha zifuatazo kuthibitisha makala

WIKI NENDA KWA USALAMA, CHANGAMOTO INAYOKUA KWA KWA KASI KWA WAENDESHAJI NA WATUMIAJI WA VYOMBO VYA USAFIRI, MIUNDOMBINU NA WADAU WA USIMAMIZI

WIKI YA NENDA KWA USALAMA HAINA TIJA


WIKI YA NENDA KWA USALAMA HAINA TIJA KATIKA KUPUNGUZA AJALI NA KUONGEZA WELEDI NA UMAHIRI KATIKA KUTUMIA NA KUHUDUMIA WATUMIAJI WA VYOMBO VYA USAFIRI 

Imekuwa ni kasumba kwa Jeshi la Polisi hususani kitengo cha Usalama Barabarani kuonekana wakiwa barabarani wakiwadhibiti madereva kuhusu zoezi la ukaguzi wa magari na leseni za udereva. Na kwa bahati mbaya ukaguzi wa magari umekuwa ukiegemea zaidi kwenye magari ya abiria na kuacha magari mengine watu binafsi yakiendelea kutembea mitaani.  
Kamanda mkuu kikosi cha usalama barabarani Mohamedi Mpinga akionyesha (waandishi wa habari hawapo pichani) jinsi ya kufungua na kubandika stika maaalum kwaajili ya kampeni ya kudhibiti Usalama barabarani mara baada ya kukabidhiwa stika hizo na wadhamini wao kampuni ya simu za mkononi Airtel na Puma, wanashudia pichani toka kulia ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa airtel Bi Beatrice Singano na Mkurugenzi wa kampuni ya Mafuta Puma bw, Maregesi Manyama, na kushoto ni Naibu waziri wa Mambo ya Ndani Mh, Pereira Ame Silima, wiki ya Nenda kwa usalama mwaka huu kitaifa itafanyika mkoani iringa ikiwa imebeba ujumbe usemao “ Pambana na ajiali za barabarani kwa vitendo, zingatia sheria
Ukaguzi wa vyombo vya usafiri kama magari ni muhimu kwa sababu kuna wamiliki wengine hujisahau na hivyo kushindwa kuchukua hatua za makusudi kuangalia na kuhudumia magari yao. Lakini pia katika ajali za barabarani magari yote huusika, yawe na binafsi au ya usafiri na kwa maana hiyo, sheria lazima izingatiwe sawe kwa vyombo vyote vya usafiri. 

Lakini kwa nini serikali haiweki nguvu yake katika kushughulikia kwa mapana yake Wiki ya Nenda kwa Usalama Tanzania? Ni dhahiri, viongozi hawana mwito au nia ya dhati katika kuhakikisha kuwa roho za watanzania zinalindwa kutokana na wimbi kubwa la ajali za barabarani. Mara nyingi najiuliza ni kwa nini hakuna bajeti maalum kwa ajili ya kutoa elimu kwa watumiaji wote wa barabara na waendesha vyombo vya usafiri na watumiaji wake. Sijawahi kusikia kutengwa kwa bajeti au fungu fulani kwa ajili ya kutoa elimu ya msingi/mahususi kwa watumiaji wa magari, abiria na pia watumia barabara zetu. 

Makampuni baki kwa maslahi yao, ndiyo yameonekana kujitokeza kutoa fedha kiasi na nguo au baadhi ya vifaa kiduchu ambavyo vinatumika wakati wa wiki hiyo moja tu ya nenda kwa usalama. Hii ni kijeli na dharau kwa Watanzania ambao wengi wao wanaendelea kuumia kutokana na lindi kubwa la ajili za barabarani zinazoendelea kutokea kila siku. 

Binafsi naamini kabisa, kama serikali kupitia jeshi la polisi, kitengo cha usalama barabarani wangeelekeza nguvu zake katika kutoa elimu badala ya kujipanga barabarani kula rushwa, ajili nyingi zinazoendelea kutokea, zingekoma kabisa. Madereva na watumia barabara wangepata umahiri katika bahari hii ya usalama barabarani. Elimu pekee ndiyo njia mahsusi ya kujikwamua na taifa hili na vifo na majanga ya ajali. 

Pia, kuendelea kushamiri kwa matatu katika barabara zote za Tanzania ni chanzo kikuu cha ajali. Na hii ni ishara ya kushindwa kwa jeshi la polisi na mamlaka nyingine husika katika kusimamia matumizi bora ya barabara na watumiaji wake. Matuta barabarani yanaendelea kudidimiza uchumi wa Tanzania kutokana na wananchi kulipa fedha nyingi za kigeni kuagiza spea/vipuri vya magari yao. Mtikisiko mkubwa ambao unalipata gari dogo, gari kubwa la mizigo na basi la abiria katika umbali wa kilometa 1000, ni ishara kwamba, katika kipindi cha mwaka mmoja, gari litakuwa limepunguza zaidi ya miaka miwili ya muda wake wa kufanya kazi kwa ufanisi.  

Matuta barabarani si suluhi ya matatizo ya ajali yanayoendelea kutokea katika nchi ya Tanzania. Serikali, polisi na mamlaka nyingine husika, zimeshindwa kabisa kutafuta suluhi ya kuboresha usalama barabara na kuishia kuweka matuta. Hapa ndipo akili za wadau wa usafiri zilipoishia. Hii ni aibu kwa taifa hili, hususani kwa wageni mbalimbali wanaondelea kumiminika Tanzania.

Ukitembelea nchi za wenzetu kuna mambo mengi ya kujifunza, mfano alama za barabarani huweka kwa kutumia mabanga makubwa ambayo hayahitaji mtu kuvaa miyani kuyaona. Na pia huwekwa kila baada ya umbali wa kilometa 1 au 2 huku humu katikati kukiwa na punguza la umbali wa mita mia 200 hadi mia 300 kabla ya tukio halisi ambalo lilikuwa limelengwa. Mfano kupinda kushoto kwenda mji mwingine, ambapo aina ya barabara na idadi ya barabara huashiriwa katika mapango hayo elekezi ya usalafiri.

Tofauti na hapa kwetu, kibao cha kuonesha kuwa unapaswa kutembelea kilometa 50 kwa saa huonekana ghafla tena kwa maandishi madogo sana. Na pengine, unamkuta askari wa tochi amekaa hapo hapo na kusema, umeovaspidi. Hii ni fedheha na ni aibu kwa taifa letu.

Naamini viongozi na watendaji mbalimbali ambao ni wadau wa usafiri na usalama barabarani wanatembea mara kwa mara katika nchi za wenzetu kwa nini hawaji na somo jipya.

Kauli mbinu na fulani hazina tija kwa taifa letu katika tasnia ya usalama barabarani kama kutakuwa hakuna sera na msingi mahsusi katika utoaji elimu na pia kuwaelimisha watumiaji wa barabara, vyombo vya usafiri na vyombo vyenyewe.

WIKI YA NENDA KWA USALAMA


Naibu waziri wa Mambo ya Ndani Mh, Pereira Ame Silima akipokea sehemu ya ya stika maaalum kwa ajili ya kampeni ya Usalama barabarani toka kwa wadhamini wa stika hizo kwa mwaka huu Airtel na Puma, wnaokabidhi toka kulia ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa airtel Bi Beatrice Singano na Mkurugenzi wa kampuni ya Mafuta Puma bw, Maregesi Manyama. Anaeshudia makabidhiano ni kamanda mkuu kikosi cha usalama barabarani Mohamedi Mpinga. Airtel Tanzania na Puma ni wadhamini wakuu wa wiki ya uhameasisaji wa wiki ya Nenda kwa usalama ambapo mwaka huu kitaifa itafanyika mkoani iringa ikiwa imebeba ujumbe usemao “ Pambana na ajiali za barabarani kwa vitendo, zingatia sheria
 
WIKI YA NENDA KWA USALAMA, CHANGAMOTO INAYOKUA KWA KWA KASI KWA WAENDESHAJI NA WATUMIAJI WA VYOMBO VYA USAFIRI, MIUNDOMBINU NA WADAU WA USIMAMIZI
 
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel ikishirikiana na kampuni ya mafuta PUMA kwa pamoja wameungana na serikali ya jamuhuri ya Tanzania kwa kupitia baraza la taifa la usalama barabarani na Jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani katika kuhakikisha elimu kuhusu usalama barabarani inatolewa ili kuthibiti idadi ya ajali za barabarani nchini.


 Kutangazwa kwa ushirikiano huo kumefanyika leo katika ofisi za makao makuu ya PUMA ambapo Mkuu wa kitengo cha usalama barabarani Tanzania Kamanda Mohamed Mpinga ametangaza wiki ya nenda kwa usalama barabarani ya mwaka huu itakayozinduliwa rasmi siku chache zijazo huko mkoani Iringa.

Akiongea wakati wa hafla hiyo mgeni rasmi , Naibu Waziri wa mambo ya ndani Mheshimiwa Pereira Ame Silima alisema” nachukua fulsa hii kuwashukuru wadhamini wa kampeni ya usalama barabarani kwa mwaka huu kampuni ya simu za mkononi ya Airtel na Kampuni ya Mafuta ya PUMA kwa kutoa mchango wao wa pamoja na kushirikiana na jeshi la polisi usalama barabarani kufikia malengo kwa kuhakikisha usalama wa raia na kupunguza ajali za barabarani ”

Ajali za barabarani zinaongezeka kwa kasi na kusababisha upotezaji wa nguvu kazi huku zikiacha maafa makubwa kwa taifa, ni jukumu la kila mtanzania kuwa sehemu ya kusimamia na kuzingatia sheria za barabarini huku tukiishi na kutimiza kauli mbiu ya mwaka huu “Pambana na Ajali za barabarani kwa vitendo, Zingatia Sheria”.

Nachukua fulsa hii kuwaaasa watumiaji wa vyombo vya moto kupeleka magari yao kukaguliwa na kuthibitishwa ubora wa kutembea barabarani ili kuhakikisha vyombo vinavyotumika kubeba abiria viko salama na vinakidhi viwango vilivyowekwa kuhakikisha usalama barabarani.” aliongeza Silima.

Akiongea kwa niaba ya Airtel, Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Beatrice Singano Mallya alisema “Airtel tunajivunia kuwa sehemu ya juhudi za kuokoa maisha ya watanzania na mali zao na tunayo dhamira ya kuhakikisha tunashirikiana na wadau wote wenye wito wa kusaidia usalama barabarani na jeshi la polisi usalama barabarani kupunguza ajali za barabarini kwani ushika hiuu wa Airtel leo ni moja kati ya shughuli za kijamii tunazozifanya nchini.

Nia na madhumuni yetu makubwa ni kusaidia shughuli zinazofanywa na jeshi la polisi kusimamia na kupunguza maokeo ya ajali za barabarani, kila mwaka kuna kunakua na matukio ya ajali za barabarani ambazo zingeweza kuepukika kama wahusika wangekua na elimu ya kutosha. Hii ndio sababu kubwa na madhumini ya Airtel kuwa mmoja ya washiriki wakuu katika kusaidia kuhamasisha na kutoa elimu itakayofanikisha upungufu wa ajali barabarani kwa wa tano sasa.”.

Akizungumza kwa niaba ya kampuni ya mafuta ya PUMA ENERGY Mkurugenzi Mkuu wa PUMA ENERGY ndugu MAREGESI BEN MANYAMA… alisema “tuna malengo makuu matatu kuhusu usalama kazini nayo ni kutokua/kutosababisha ajali, kutoumiza mtu yeyote na kutoharibu mazingira. Sisi tunaamini kuwa Baraza la Usalama Barabarani lina jukumu kubwa na muhimu sana la kupunguza ajali za barabarani.

Hivyo mchango wetu kusaidia juhudi za Baraza, zinaendana sawasawa na malengo yetu ya usalama. Kama huu msaada wetu mdogo utafanikisha kuepusha hata kifo kimoja, sisi tutaona kuwa malengo ya msaada yatakuwa yamefikiwa. PUMA ENERGY wamakuwa wabia wa muda mrefu (kabla ya hapo BP Tanzania) wa masuala ya Usalama Barabarani. Ni nia yetu kwamba tutaendelea kushirikiana na jeshi la Polisi pamoja na wadau wengine kuendelea na mapapambano ya kupunguza ajali nyingi ambazo tunaamini nyingi zinaweza kuzuilika”
Nae kamanda mkuu wa jeshi la usalama Tanzania afande Mohamed Mpinga alisema.”Tunatoa wito kwa watu wote kushirikiana nasi kufanikisha zoezi hili na nimatumaini yetu elimu tutakayoendelea kuitoa kwa wananchi itasaidia katika kupunguza na kudhibiti ajali zinazotoka barabarini nakusababisha maafa makubwa kwa taifa na jamii kwa ujumla. Tunawaomba watanzania wote wahakikishe magari yao yamefanyiwa ukaguzi katika kipindi hiki cha usalama barabarani na rai yetu sio tu kwa wakazi wa Iringa ila pia ni kwa watanzania wote katika mikoa yote nchini.

Airtel kwa mwaka huu imechangia kuchapisha stika, kutoa elimu kwa kupitia vyombo za habari nchini pamoja na kutoa vitu mbalimbali ikiwemo T shirt 800 zenye ujumbe wa mwaka huu “Pambana na Ajali za barabarani kwa vitendo, Zingatia Sheria”. Tunaamini ajali za barabarani zinaweza kuepukika ikiwa kila moja atafanya sehemu yake Mallya aliongeza.

Airtel imekuwa mstari wa mbele katika kuchangia shughuli za usalama barabarani nchini , kwa miaka 4 mfululizo sasa Airtel kwa kushirikiana na Baraza la Usalama Barabarani imekuwa ikijitahidi kuhakikisha ajali zinadhibitiwa.

Wednesday 19 September 2012

Nguvu umma yamtesa pinda mwanza, azomewa, awa mbogo


Vijana Mwanza Waimba ‘People’s Power, Hatuitaki CCM’

Na mwandishi wetu
 
Mizengo Pinda, Waziri Mkuu
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda, jana alijikuta katika wakati mgumu baada ya kushindwa kuhutubia maelfu ya wakazi wa Wilaya ya Nyamagana, jijini Mwanza kwa muda kutokana na wananchi wengi kumzomea.

Kiongozi huyo alikumbana na kisanga hicho cha aina yake akiwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Clement Mabina pamoja na Mkuu wa Mkoa huo, Mhandisi Evarist Welle Ndikilo.

Pinda na viongozi hao, walikumbana na zomeazomea hiyo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Sahara jijini hapa, ikiwa ni hitimisho la ziara ya Waziri Mkuu huyo ya siku saba mkoani Mwanza.


Chanzo cha Pinda na viongozi hao kuzomewa mkutanoni hapo, ilitokana na kile kilichoonekana kuwepo kwa kero nyingi zilizodaiwa kushindwa kupatiwa ufumbuzi na Serikali ya CCM chini ya Rais Jakaya Kikwete.


Kitendo hicho cha wananchi kilimlazimisha Pinda kushindwa kuhutubia kwa muda, huku akionekana kujawa jazba.


Sababu nyingine ya wananchi kuzomea, ni hatua ya Pinda kuwaambia wananchi hao watoke mjini waende vijijini wakalime waachane na mambo ya upinzani wa kisiasa.


Pinda alitoa kauli hiyo baada ya kundi la vijana mkutanoni hapo kuonesha alama ya V, bendera ya CHADEMA na nyimbo za Peoples, Power.


Kwa mazingira hayo, askari wa polisi wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU), waliokuwa na silaha nzito za kivita aina ya SMG, mabomu na marungu waliokuwepo mkutanoni hapo, walianza kuwatishia kuwapiga wananchi hao kwa lengo la kumlinda kiongozi huyo.


Baada ya kuzidi zomeazomea hiyo, Waziri Mkuu, Pinda alilazimika kumuita mbunge wa Nyamagana, Ezekiel Wenje (CHADEMA), aliyekuwa meza kuu, kisha kusema: "Nyamazeni basi!. Wenje...hii ndiyo serikali ya siku chache zijazo. Kwa namna hii naona hamuwezi, maana itakuwa ni vurugu asubuhi hadi jioni". Akazomewa kisha wakaimba hatutaki CCM, hatutaki CCM. .


Baada ya kuona hivyo, Pinda akacheka na kusema: "Hahahaaaaa, hata mkiimba peoples power, CCM ndiyo inayowaongoza". Akazomewa tena kisha Pinda akashindwa kuendelea kuzungumza jukwaani.


Akahutubia mkutanoni hapo, Pinda aliwataka wananchi hao waache ushabiki wa kisiasa, na kwamba halmashauri ya jiji la Mwanza inayoongozwa na CHADEMA, ndiyo itapaswa kulaumiwa kama itashindwa kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wananchi wake.


"Hapa jiji la Mwanza linaongozwa na CHADEMA. Meya wa CHADEMA, mwenyekiti wa Mipango miji wa CHADEMA, Naibu Meya ni wa CHADEMA. Lakini kama wameshindwa kuweka mipango mikakati ya kuwasaidia tutasema hawafai," alisema kisha akazomewa kwa mara nyingine.

Baada ya zomeazomea hiyo kuonekana kumwelemea Waziri Mkuu huyo, Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Ndikilo alilazimika kuingilia kati kwa kusema: "Wanaozomea tunawafahamu, na tunawafahamu waliowaleta hapa ili mje kufanya nini". Akazomewa.

Hata hivyo, baada ya hali kutulia kidogo, Pinda aliendelea kuhutubia huku akiwataka wananchi wa jiji la Mwanza waondoke mjini waende vijijini wakalime, jambo lililoonekana pia kuwakasirisha wananchi wengi kisha kumzomea tena.


Ingawa Pinda alilazimika kutumia muda mfupi kutoa hotuba yake, aliwaomba wana Mwanza washirikiane kuleta maendeleo yao, na kwamba iwapo tatizo ni Mkurugenzi wa jiji suala hilo litaangaliwa.


Aliwaomba wadumishe amani iliyopo hapa nchini, ikiwa ni pamoja na kushirikiana na Serikali kupambana na vitendo vya uvuvi haramu katika Ziwa Victoria, ili kuweza kuzua samaki wadogo wasivuliwe kisha kuharibu mazalia ya rasilimali hiyo.


"Jambo jingine ninalotaka kuwaeleza hapa leo ni hili la uvuvi haramu. Samaki ndani ya Ziwa Victoria wameisha...na hii ni kwa sababu ya uvuvi usiozingatia sheria. Tushirikianeni kupambana na vitendo hivi", alisema Pinda kisha akazomewa tepa.

Tuesday 18 September 2012

WAZIRI NCHIMBI HAKUVAMIA KWA BAHATI MBAYA MAANDAMANO YA WAANDISHI


WAZIRI NCHIMBI HAKUVAMIA KWA BAHATI MBAYA MAANDAMANO YA WAANDISHI WA HABARI LEO JANGWANI

Mwandishi wa Kujitegemea
 
Nawapongeza sana waandishi wa habari kwa kumtimua waziri wa mambo ya ndani Emmanuel Nchimbi nawapongeza sana kwa kuonyesha hisia zenu kwa kitendo kiovu kabisa ambacho kila mpenda demokrasia na haki katika ulimwengu huu ambacho amefanyiwa mbali ya kuwa mwandishi wa habari ni Mtanzania mwenzetu huyu marehemu Daudi Mwangosi.

Haina ubishi polisi ndio wameua kinachopiganiwa hapa wahusika wote ambao wako nyuma ya mauji haya washughulikiwe zaidi wale ambao wanatoa amri dhalimu kwa polisi,lakini nataka niwaambie waandishi wa habari Emanuel Nchimbi waziri wa mambo ya ndani, kuvamia maandamano yenu ya wanahabari na kutaka kuhutubia bila kualikwa sio bahati mbaya anajua mtaandika zaidi kuhusu yeye kutimuliwa kwake kwenye maandamano na kuacha kuandika maaovu na ujumbe mliokusudia kuupeleka kwa serikali na polisi wao,haingii akilini kwa mtu mwenye ngazi ya waziri kuvamia kwa mfano sherehe ambayo hana kadi ya mwaliko?

Kwa hiyo rai yangu kwa wanahabari ni kuandika kile ambacho mlikusudia kukiwakilisha leo kwa watanzania na dunia nzima !!Hawa ndio mawaziri wa tanzania huwezi kujua wakati gani yuko serious!!

Je mnakumbuka mjadala wa dowans ulivyopamba moto wakatuletea kikombe cha babu loliondo?? Na viongozi wote waserikali wakawa wa kwanza kupata kikombe na kusifia kikombe?? Kwa hiyo nchimbi asiwatoe kwenye lengo lenu. Kama hamfahamu vizuri Nchimbi ni zao la wanamtandao waliomweka Kikwete madarakani na ndio mwenyekiti aliyevuruga uvccm, na kama mnataka ukweli zaidi nendeni mkamhoji Sumaye Fredrick waziri mkuu mstaafu alikua anamaanisha nini alivyosema "anayefagia njia ya kwenda ikulu kwa karatasi basi akifika huko atatumia risasi ili aweze kutawala"mwaka 2005 kwenye kinyang'anyilo cha urais alipokuwa amechafuliwa sana na wanamtandao kwenye kampeni za kuwania urais kwa tiketi ya CCM.
kwa hiyo waandishi mshikamane mno kipindi hiki kwani serikali inajaribu kutumia kila aina ya hila kuwagawa na kuwatoa kwenye mjadala wa msingi kuwa waliomuua Daudi Mwangosi wachukuliwe hatua na wengine wawajibishwe kutokana na nyadhfa zao.

Maoni ya Wananchi

Maoni ya Wananchi
 
Nchimbi angekatwa shingo!!!
Kama mtanzania niliyeumizwa na mauaji ya makusudi aliyofanyiwa Mwangosi na Jeshi la Polisi, nimesikitishwa sana na uamuzi wa Nchimbi kwenda kuingilia kati Maandamano halali ya wanahabari pale Jangwani yaliolenga kuonyesha hisia zao na kulaani. Nchimbi hakualikwa kuwepo mahala hapo kwa wakati huo, baada ya kumuomba aondoke, nilimsikia kwa kauli yake anasema wao (kama Serikali) wanachochukia sana ni Mtu kufanya maandamano bila kibali, je yeye alipata wapi kibali cha kuingilia kati maandamano ya waandishi wa habari?
Waziri wa Mambo ya Ndani Emmanuel Nchimbi akisindikizwa na Polisi kutoka eneo la Viwanja vya Jangwani
Jeshi la Polisi lililo chini ya mamlaka ya Nchimbi limekuwa likijichukulia sheria mkononi ikiwemo kuhukumu vifo kama lilivyofanya kwa Mwangosi kwa watu wa aina ya Nchimbi ambao kwa maelezo yao linadai wanakuwa wanasabibisha fujo, je hizi sheria za kudhibiti fujo hazi-apply kwa Nchimbi? Kwa polisi walio makini nilitegemea Nchimbi angekamatwa mara moja na kuhojiwa kwa kosa la kuingilia maandamano halali ya waandishi wa habari na hivyo kuhatarisha amani.
Nijuavyo mimi kwa maandamano ya majonzi kama yale yakifanywa na watu wasio wastahimilivu iwapo atatokea mtu asiyealikwa na kuyaingilia kati anaweza akauawa, hiki ndicho kilichonilazimu niandike thread hii kuwapongeza wanahabari kwa kuwa na mioyo ya ustahimirivu.
Ninawapongeza sana Waandishi wa habari kwa kumuonyesha Nchimbi kwamba wao ni wakomavu kuliko yeye kwasababu waandishi wa habari wameingiliwa katika maandamano yao lakini hawakuchukua sheria mkononi kama wanavyofanya Polisi mbali na ukweli kwamba waandishi wa habari hawajapata mafunzo maalumu kama Jeshi la Polisi jinsi ya kumshughulikia mharifu.
Nawapongeza sana waandishi wa habari msingekuwa wakomavu na wastahimirivu jana Nchimbi angekatwa Shingo.
Ushauri wangu kwa Waandishi wa Habari. Nawaombeni mumsamehe bure Nchimbi huenda hajui alifanyalo.
Ushauri wangu kwa Polisi. Nawaombeni mumkamate Nchimbi na kumhoji ili muweze kujua alikuwa amekusudia nini kwenda mahala ambapo hajaalikwa? je alitaka waandishi wa habari wamfanyie fujo ili wapigwe risasi na baadhi ya Polisi wasiojua kazi yao hasa ni nini? ikiwezekana mumshitaki Nchimbi kwa kuingilia kati maandamano yasiyo muhusu ili iwe onyo kwa wananchi wengine wasio staarabika kwani kitendo alichofanya jana Nchimbi kikiendelea kuchukuliwa kama ni cha kawaida ipo siku amani yaweza kuvunjika. kwa mfano Waislam waweza kuwa na maandamano yao akatokea Mchungaji mbele yao kwa nia ya kuwapokea, hopefully wasipokuwa wastahimilivu amani yaweza kutoweka.
Ushauri wangu kwa Nchimbi. Nakuomba uwatake radhi waandishi wa habari kwa fujo ulizozifanya jana, pia uwatake radhi wananchi maana wengi wetu hatukutegemea kama ipo siku kiongozi kama wewe unaweza kukosa busara kiasi hicho kwa kwenda mahala bila mualiko kwasababu uzijuazo wewe mwenyewe.

WANAHABARI WAMTIMUA WAZIRI NCHIMBI KATIKA MAANDAMANO YAO

WANAHABARI WAMTIMUA WAZIRI NCHIMBI KATIKA MAANDAMANO YAO

Na Mwandishi Wetu
Waziri wa Mambo ya Ndani Emmanuel NchimbiKatibu wa Jukwaa la Wahariri Bw. Nevil Meena akiongea kwa uchungu mbele ya wanahabari wenzake ambapo pamoja na maazimio mengine wametangaza kutoandika habari zinazohusiana na jeshi la polisi kwa siku 40.

Wakiwa katika nyuso za huzuni kubwa ya kuondokewa na mwenzao ambaye aliuawa kwa kupigwa na bomu, kundi la Wanahabari wao wamemtimua Waziri wa Mambo ya Ndani Mh. Emmanuel Nchimbi kutokana na kuwaingilia kwenye maandamano yao.

Wanahabari kote nchini leo wamefanya maandamano ya amani kwa lengo la Kulaani mauaji ya mwenzao wa kituo cha Televisheni cha Channel Ten, Daudi Mwangosi.

Kufukuzwa na kuzomewa kwa Waziri Nchimbi kumekuja baada ya kugundulika kuwa ameingilia maandamano kwa lengo la kuyapokea bila kupewa mwaliko.

Kutokana na zomea zomea hiyo ya wanahabari hao dhidi ya Waziri Nchimbi hali ilionekana kuwa si shwari na kupelekea waziri huyo kuondolewa na rais wa UTPC Keneth Simbaya na viongozi wengine wakiwemo askari polisi.

Akizungumza na kundi la waandishi Katibu wa Jukwaa la Jukwaa la wahariri (TEF) Neville Meena amesema “Hatuna ugomvi na Waziri Nchimbi kwani ni mwenzetu, rafiki yetu, ila leo hana vazi la msiba”.

Mara baada ya kuondoka bila kupenda Waziri Nchimbi, hali ya utulivu ilikuwa kama kawaida na shughuli zingine ziliendelea kama ilivyopangwa.

Monday 10 September 2012

Usafiri wa Baiskeli Tegemeo Kubwa Afrika

Adha ya Usafiri katika nchi za Kiafrika
Usafiri wa baiskeli umekuwa ni wa kutegemea kwa kiwango cha juu katika bara la Afrika na mabara mengine duniani. Toka baiskeli ilipogunduliwa mwanzoni mwa miaka ya 1900, familia nyingi za kiafrika ziliutegemea sana usafiri huu. Familia ilionekana yenye maendeleo pale tu ilipoweza kupata baiskeli. Lakini kutokana na kuendelea kudidimia kwa maendeleo hususani katika maeneo ya vijijini, tofauti na na miaka ya nyuma ambapo uzalishaji wa mazao mbalimbali ya nafaka na mifugo ilikuwa juu, familia ziliweza kupata ziada na baadaye kuuza na kununua baiskeli.
 
Baada ya Azimio la Arusha kufa, maendeleo ya vijiji vingi yamekuwa yakididimia kila siku na hivyo kupelekea maradhi wakuu wa watatu waliokuwa wanaikabili Tanganyika na Tanzania baadaye baada ya uhuru, kuendelea kuwanyanyasa wananchi. Suala la kupata baiskeli au usafiri mbadala katika baadhi ya vijiji, imekuwa ni ndoto tofauti na hali halisi ya maendeleo ya sayansi na teknolojia inavyoendelea kukua.
 
Kama mwananchi akifanikiwa kuipata baiskeli huiboresha ili ifanye kazi zaidi na kumudu mahitaji mengine ya kifamilia mfano kutoa huduma ya usafiri. Mfano mdogo tu, angalia picha hii hapa ambapo baiskeli ina uwezo wa kubeba idadi kubwa ya abiria. Shuhudia mwenyewe... Haya ndiyo maisha ya dunia ya tatu.

Birthday Party for Carolyn Kivenule


Happy birthday Carolyn Adam Kivenule

Carolyn Adam Kivenule PhotoIt was a marvellous Sunday of 9th September 2012, when Carolyn Adam Kivenule celebrated her second birthday at Ubungo Kibangu, Dar es Salaam. The event started at 19:00 hours after a tight schedule which involved  relatives, send off meeting and Sunday prayers. Mr. Adam Kivenule with a companion of many children whom are close relatives and neighbourhood of Carolyn took part in the cherish event. Carolyn who had a lot of expectations and miscellaneous troubled the event, sometimes crying and sometime laughing. She never tried to dance herself rather than seeking company from somebody else.

It was very entertainment night accompanied with different types of local and gospel dances celebrating invitees.

Juices and a special cake which was taken by everybody who participated the event flavoured the occasion. Photos which was  taken by participants will continue to cherish and remain as a great memory to the anniversary of two years of Carolyn Adam Kivenule.


Thanks,