Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Wednesday 26 June 2013

MZEE HUSSEIN TAVIMYENDA TAGUMTWA KIVENULE AFARIKI DUNIA



TANZIA

MZEE HUSSEIN TAVIMYENDA TAGUMTWA KIVENULE AFARIKI DUNIA


BABU HUSSEIN TAVIMYENDA TAGUMTWA KIVENULE AMEFARIKI DUNIA AKIWA NA UMRI WA MIAKA 115, KATIKA HOSPITALI YA IPAMBA IRINGA. MIPANGO YA MAZISHI BADO INAENDELEA KUFANYIKA NA UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI). MZEE HUYU ALIZALIWA ENEO LA ULEFI, MAGUBIKE, MKOANI IRINGA KUNAKO MIAKA YA 1890. KWA TAARIFA ZAIDI: http://www.kauki-kauki.blogspot.com /http://www.tagumtwa.blogoak.com au simu 0713270364
E-mail: kauki2006@gmail.com / kivenue@gmail.com

HISTORIA YA BABU HUSSEIN TAVIMYENDA TAGUMTWA KIVENULE
Mzee Hussein Tavimyenda Kivenule alikuwa ni mtoto wa nne wa Bibi Mkami Sekabogo. Yeye aliishi eneo la Ulefi na baadaye Mlafu. Kwa sasa alikuwa anaishi eneo la Magubike. Mpaka leo hii anafariki, Babu Hussein Kivenule anakadiriwa kuwa na umri wa miaka zaidi ya 115 kwa mujibu wa taarifa na tafiti ambazo tunazo.

Babu Hussein Tavimyenda Kivenule ameshiriki kikamilifu katika Vita vya Pili ya Dunia. Wakati anashiriki vita hiyo alikuwa na umri wa zaidi ya miaka 44. Amepigana vita maeneo mbalimbali mfano Burma, India, Ulaya na Makoloni mbalimbali ya Waingereza. Alikuwa anakabiliwa na upofu wa macho ambao anasema ulisababishwa na Baruti. Hali kadhalika anakiri kuwa kuendelea kuwa hai ni kwa sababu alipigana upande wa Mwingereza. Anakiri vita ndiyo iliyomsababishia upofu pengine asingekuwa na hali aliyonayo kwa sasa.

Mzee Hussein Kivenule alioa wake wawili na kubahatika kupata watoto kumi na tatu (13). Kwa mke wake wa kwanza Bibi Yimilengeresa Semsisi. Babu Hussein alipata watoto wafuatao:
1.     Nyakudila          Benjemin      Kivenule
2.     Sekiyavile          Modesta       Kivenule
3.     Dominicus                            Kivenule
4.     Emmanuel                            Kivenule
5.     Luciana                                Kivenule
6.     Ajendina                             Kivenule

Kwa upande wa mke wa pili wa Bibi Dalika Setala, Mzee Hussein Kivenule alipata watoto wafuatao:
1.     Kabogo Bernadi           Kivenule
2.     Sembata Josephine Kivenule
3.     Necia               Kivenule
4.     Batromeo          Kivenule
5.     Brandino           Kivenule
6.     Tavina              Kivenule
7.     Masikitiko         Kivenule

Asilimia kubwa ya familia ya Babu Hussein Kivenule inaishi maeneo ya Magubike, Idete na Ibogo. Pia wapenda historia mnakaribishwa kwenda kumtembelea Babu Hussein Kivenule.

No comments:

Post a Comment