Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Friday 18 December 2015

MAANDALIZI YA MKUTANO MKUU WA 11 WA UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)


Adam Kivenule, Katibu Mkuu-KAUKI

Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) kwa kushirikiana na Kanda ya Nduli, kwa heshima kubwa unapenda kuwajulisha ndugu, jamaa, marafiki na Wana Ukoo wote, umeanza maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 11 wa KAUKI, utakaofanyika Kijijini Nduli, Mkoani Iringa, tarehe 2 had 3 Julai, 2016.

Kwa taarifa hii, tunaomba Viongozi wote wa KAUKI na Viongozi wa Kanda, kuanza kujiandaa kwa Mkutano huo muhimu. Sambamba na hilo, Viongozi wa KAUKI waendelee kuratibu maandalizi ya Mkutano kwa kusambaza taarifa na kuweka mikakati imara ya kuhakikisha kuwa Mkutano Mkuu wa 11 wa KAUKI unafanikiwa. Wadau wakuu wa maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 11 wa KAUKI ni Viongozi wa Kanda kwa kushirikiana na ndugu wote.

Ikumbukwe kuwa, mwaka huu (2015), Mkutano wa Mkuu wa KAUKI uliopangwa ufanyika Kijijini Irore, Mkoano Iringa, umeshindwa kufanyika kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wetu. Maana nyingine Kanda ya Irore bado inayo nafasi nyingine ya kuandaa Mkutano Mkuu wa 12 wa KAUKI, 2017. Kwa hiyo wana Irore na sehemu zote za Igominyi mnaombwa kuanza kufanya maandalizi ya mkutano wenu, sambamba na maandalizi ya Mkutano Mkuu utakaofanyika Nduli mwakani.

Kuna mambo mengi muhimu yanaweza kufanyika kama sehemu muhimu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 11 wa KAUKI, utakaofanyika Kijijini Nduli:
1. Kila ndugu kushiriki kikamilifu katika maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 11 wa KAUKI na kuhakikisha kuwa unafanikiwa. Kila mwana ukoo anaweza kujitoa kwa chochote kile ambacho kitasaidia kufanikisha Mkutano Mkuu wa 11 wa KAUKI.
2. Ndugu wenye uwezo kujitolea ili kufanikisha Mkutano Mkuu wa 11 wa KAUKI. Kuna wana Ukoo ambao wamejiajili na wana vipato vya uhakika. Tunaomba kwa moyo wa upendo wasaidie kuandaa mkutano huu. Pia kuna ndugu ambao wameajiliwa na wana vipato vizuri. Tunaomba wachukue jukumu la kusaidia kugharama za maandalizi ya Mkutano huo.
3. Wana Ukoo wa Kanda ya Nduli na Kanda nyingine ambazo zina fursa ya ardhi, wanaweza kulima angalau nusu ekari kwa lengo la kupanda mazao ambayo yatatumika kwa ajili ya kufanikisha Mkutano Mkuu wa 11 wa KAUKI. Mazao ambayo yanaweza kupandwa ni pamoja na Mahindi, Maharage, Viazi na mazao mengine ya nafaka.
4. Kuhamasishana na kuhimizana ndugu na wana ukoo miongoni mwetu ili kuendelea kuwa na moyo wa kupendana, kushirikiana na kusaidiana; na pia kuwa pamoja katika masuala yote yanayohusu ndugu na ukoo kwa ujumla kwa faida yetu wote.
Matarajio ya Mkutano Mkuu wa 11 wa KAUKI, utakaofanyika tarehe 2 – 3 Julai, 2016, Kijijini Nduli.
Mkutano Mkuu wa 11 wa KAUKI unatarajia yafuatayo:
1. Kuendelea kuboresha Kitabu cha Wana Ukoo kwa kujaza taarifa mbalimbali za ndugu (Clan Organization Tree).
2. Kuwafahamisha wana ukoo, Historia na Chimbuko la Ukoo. Hususani Ukoo wa Kivenule.
3. Mwingiliano wa Ukoo wa Kivenule na Koo nyingine uliopelekea kuwepo kwa Ukoo wa Kivenule.
4. Kufanya tathmini ya mipango mbalimbali ya KAUKI tuliyojiwekea kwa miaka kadhaa.
5. Kutathmini changamoto na vikwazo mbalimbali vinavyoukabili Umoja wetu.
6. Yatakayojiri katika Mkutano Mkuu wa 11 wa KAUKI, utakaofanyika tarehe 2 – 3 Julai,

Imeandaliwa na kusambazwa na:

Katibu Mkuu (Adam Alphonce Kivenule)
Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI)
Mobile: 0713 270364
            kivenule@gmail.com




No comments:

Post a Comment