Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Sunday 10 September 2023

TAARIFA MUHIMU KWA WANAUKOO WA KIVENULE

Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) ulifanya kikao cha dharura cha masaa matatu (3) tarehe 7 Septemba 2023 siku ya Alhamisi, Kijijini Kidamali baada ya kuhitimisha mazishi ya ndugu yetu Steward Edgar Kivenule.

Kikao hicho kilichoongozwa na Mwenyekiti wa UKOO wa Kivenule Ndugu Faustino Sigatambule Kivenule; na kilihudhuriwa na Wanaukoo wengi waliohudhuria mazishi ya Marehemu Stewart Edgar Kivenule.

Agenda Kuu ya Kikao hicho ilikuwa ni kujadili changamoto zilizosababisha kutoendelea kufanyika kwa Mikutano ya UKOO. (Taarifa Rasmi itatolewa).

Aidha UKOO wa Kivenule kupitia Mkutano huu umeazimia kwa Pamoja kuendelea kufanya Mikutano ya UKOO wa Kivenule.

Mkutano Mkuu wa Ukoo wa Kivenule ujao umepangwa kufanyika Tarehe 29 ya Juni 2024 Kijijini Kidamali. Lengo la kufanyika Kidamali ni kuendelea kuongeza hamasa kwa Wanaukoo wote, na hasa ikizingatiwa kuwa Kidamali kuna mkusanyiko mkubwa wa ndugu.

Kabla ya kufanyika kwa Mkutano huo, kutakuwa na Vikao vya Utangulizi kwa Viongozi wa Kanda mbalimbali ili kuweza kuwasilisha taarifa na pia kuweka mikakati ya kufanikisha Mkutano Mkuu wa Ukoo wa Mwaka 2024.

Imetolewa na Uongozi wa KAUKI

No comments:

Post a Comment