Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Washiriki wa Mkutano Mkuu wa13 wa KAUKI

Washiriki wa Mkutano Mkuu wa13 wa KAUKI
Washiriki wa Mkutano Mkuu wa13 wa KAUKI

Nembo ya Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI)

Nembo ya Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI)
Nembo ya Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI)

Wednesday, 25 March 2026

MAPAMBANO YA WAHEHE NA WANGONI

 Wahehe ni moja ya kabila linalopatikana mkoani Iringa. Ni moja ya kabila ambalo limejiwekea historia kubwa hapa Tanzania. Inafafanuliwa kuwa kabila la Wahehe ni muunganiko wa makabila madogomadogo kama kabila la Wadongwe,  na koo zingine kutoka Ng’uluhe na Lungemba, ambayo yalipata kukaa maeneo ya Iringa. Sababu ya muunganiko huo ni vita vilivyokuwa vikipigana kati ya Wahehe na Wasangu.

Kabla ya miaka ya 1860, hakukuwa na kabila lililofahamika kwa jina la Wahehe, lakini  mpaka kufikia miaka ya 1860, kipindi ambacho wageni wanafika na kuandika habari za makabila ya Tanzania, walipolipa jina kabila hili kuitwa Wahehe. Na asili ya jina hili linatokana na namna ya makelele( Heee….heeee….heee…) waliokuwa wakiyapiga wakati wa kwenda kwenye vita au hata wakati wa kupambana vitani.


 Ufalme wa kihehe ambao uliopata kukua karne ya 19, ulitokana na uongozi wa chifu Munyigumba (Bunini au Mugohang’amwa) na mtoto wake Mkwawa. Inasimuliwa kuwa mnamo miaka ya 1850, ufalme wa wahehe au kabila hili la wahehe lilikuwa likiogopeka sana na makabila mengine kama Wasengo hata Wasangu pia.

Walikuwa wakiogopeka kutokana na kuwa na jeshi kubwa na imara kama lile la mtemi Mirambo wa Urambo. Na mpaka wageni wanafika kwenye miaka ya 1850/1860, Wahehe bado walionekana kuwa imara katika masuala ya kivita. Kwani mpaka kufikia miaka ya 1870, Wahehe walifanikiwa kupigana na kabila la Wamasai waliokuwa wametokea kaskazini-mashariki mwa Tanzania, ambao nao pia walikimbia vita  kutoka kwa Wachaga na Wapare. Na zaidi ya hapo miaka hiyo hiyo ya 1870, wahehe walikuwa wameshafanikiwa kutawala maeneo ya Dodoma hasa yale ya upande wa kusini na kusini-magharibi. Hivyo sio tu makabila mengine waliowaogopa Wahehe bali hata wageni hao waliwahofia sana Wahehe katika masuala ya kivita.

Kabila la wahehe wakiwa chini ya utawala wa Munyigumba, walikuwa na mipango mingi ya kivita dhidi ya maadui zao. Na kwa wakati ule Wasangu ndio walikuwa maadui wakubwa sana wa kabila la Wahehe. Na kwenye hiyo miaka ya 1850, vita vilivyokuwa vikipiganwa vilikuwa kati ya Wahehe na Wasangu. Wasangu ni moja ya kabila ambalo nalo lilionekana kukua kutokana na kuunganika kwa koo mbalimbali zilizopata kuishi maeneo ya Iringa. Sababu kuu ya vita kati ya Wahehe na Wasangu ni kwamba, kila kabila lilikuwa na sera yake ya upanuzi wa eneo lao la utawala, na kila kabila lilihitaji kuteka makabila madogo madogo na kuzifanya kuwa tawala zao. Hivyo kwenye hiyo miaka ya 1850 mapambano kati ya Wahehe na Wasangu yalikuwa makubwa sana.

Lakini mambo yalikuja kubadilika mara baada ya Wangoni kuingia katika ardhi ya Uhehe wakitokea maeneo ya kusini mwa Afrika(Rejea historia ya Wangoni ilishaandikwa). Wangoni ambao walionekana nao kuwa imara katika vita, kwani walisababisha maafa makubwa sana katika ardhi ya uhehe. Ujio wa Wangoni kwa mara ya kwanza kwenye ardhi ya Uhehe ulikuwa kwenye miaka ya 1870 na ujio wa mara ya pili ulikuwa miaka ya 1882. Hivyo mipango ya kivita ya Wahehe, ikabadilika kutoka kwa Wasangu na kugeukia kwa Wangoni.

Na kuna uhakika kuwa, Wasangu waliamua kuungana na Wabena, kwa lengo la kupambana na Wangoni walioonekana wakija kwa kasi kubwa sana. Na wakati huo Wangoni wanafika katika ardhi ya Uhehe, walikuwa wameshagawanyika kwenye makundi matano.

Kwa mara ya kwanza Wangoni na wahehe walipigana maeneo ya  Nyamurenge, ambapo Wahehe waliwapiga Wangoni na kumuua kiongozi shupavu wa wangoni aliyefahamika kama Chipeta. Kitendo cha Wahehe kumuua Chifu Chipeta ambaye ndie alikuwa kiongozi wa Wangoni kwa upande ule, kilipelekea Wahehe kushinda vita.

Mbali na hapo mapambano mengine kati ya Wahehe na Wangoni yalikuwepo maeneo ya Idete mnamo miaka ya 1870. Inafafanuliwa kuwa mapambano kwenye hayo Wangoni walipigwa sana na hii ni kutokana na sababu ya njaa walikuwa nayo. Kwani mtwa Mkwawa  alitoa amri kwa Wahehe wote kuhama na vyakula vyote na kuchoma moto mazao mengine. Wahehe walifanya hivi kwa sababu walijua kuwa ujio wa Wangoni maeneo hayo ulikuwa ni kutafuta chakula,, hivyo kitendo cha kuchoma moto mazao hayo ni moja ya mbinu ya kuwashinda Wangoni.

Mapambano ya awamu hii kati ya Wahehe na Wangoni yalifika mpaka maeneo ya  Ndandu karibu na bwawa la Itombololo. Mbali na Wangoni kufa kwa njaa, wengi wao walisukumwa kwenye hilo bwawa na kufia mule. Na mwisho wa siku, mapambano kati ya Wahehe na Wangoni yalipelekea kugawanyika kwa Ubena, yaani kukawa na Ubena ya kusini chini ya  Wangoni na Ubena ya kaskazini chini ya Wahehe. Na mwisho wa siku yaani miaka ya1880 muunganiko kati ya Wangoni na wahehe ukaanzia huko na utani kati ya Wahehe na Wangoni ukaanzia huko

Inafafanuliwa kuwa kwa kipindi chote hiko cha miaka ya 1870, Wahehe walikuwa chini ya uongozi wa Munyigumba.

Na mara baada ya kifo cha Munyigumba, mtoto wake ambaye ndiye Mkwawa, alichukua madaraka na kuendeleza ufalme wa Wahehe. Inafafanuliwa kuwa kifo cha Munyigumba kilisababishwa na mapambano kati ya Wahehe na Wabena walioungana na Wandamba kutoka maeneo ya Kilombero. Vita kati ya Wabena na Wahehe, Wabena na Wandamba waliongozwa na Mutengela kutoka kwenye ukoo wa wakina Wakinamanga.

No comments:

Post a Comment