Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Washiriki wa Mkutano Mkuu wa13 wa KAUKI

Washiriki wa Mkutano Mkuu wa13 wa KAUKI
Washiriki wa Mkutano Mkuu wa13 wa KAUKI

Wednesday, 7 August 2013

UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI) ULIKOTOKA



UTANGULIZI
Ni mwaka 2005, tarehe 6 Februari, ndipo Wazo la Kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule lilipojadiliwa. Ufuatao ni muhtasari wa Kikao Hicho na maaamuzi yaliyochukuliwa, endelea...
 

MUHTASARI WA MKUTANO WA KWANZA WA KAMATI KUU YA MAANDALIZI YA MKUTANO MKUU WA UKOO WA KIVENULE, DESEMBA 17 – 18, 2005

Mahali Ulipofanyika: Ubungo - River Side Bar
Tarehe: Februari 06, 2005
Muda: 10:32 Jioni

Waliohudhuria:
Jina Kamili Mahali Anapoishi Namba ya Simu
1. Christian Kivenule Morogoro 0744 031 675
2. Adam A. Kivenule Ubungo, Dar es Salaam 0741 270 364
3. Innocent Kivenule Ubungo, Dar es Salaam 0748 663 315
4. Edgar S. Kivenule Mwenge, Dar es Salaam 0741 215 724
5. Ignas Kivenule Tabata, Dar es Salaam 0744 060 183
6. Raphael Kivenule Mbezi Beach, Dar es Salaam 0745 949 218
7. Philemon Kivenule Buguruni, Dar es Salaam 0744 757 844
8. Priskus F. Kivenule Mbezi, Dar es Salaam
9. Bakhita A. Kivenule Ubungo, Dar es Salaam
10. Tenus F. Kivenule Dar es Salaam
11. Valenia Kivenule Dar es Salaam 0745 555 521
12. Monica Kivenule City Center, Dar es Salaam 0745 409 138
13. Phesto Ngimba Dar es Salaam
14. Hamidu Mtono Mabibo, Dar es Salaam 0748 443 319
15. Athuman Mtono Kibamba, Dar es Salaam 0748 708 708
16. Nuhu Js Mtono Mabibo, Dar es Salaam

KUFUNGUA MKUTANO
Mkutano ulifunguliwa mnamo saa 10:32 jioni kwa Mwenyekiti wa muda wa Kamati ya Muda ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Ukoo wa Kivenule, ndugu Christian Kivenule, na baadaye kuuombea kwa Sala iliyochukua muda wa dakika mbili hivi. Baada ya Sala, pia Mwenyekiti wa muda aliitumia fursa hiyo kuomba msamaha kwa Ndugu Edgar Kivenule ambaye ni Baba na Mkubwa wa Ukoo wa akina Kivenule wote waishio Dar es Salaam na mikoa ya karibu, kwa kushindwa kumshirikisha kikamilifu katika hatua za awali za Mashauriano na Maandalizi ya Mkutano huo pamoja na suala zima la kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa akina Kivenule.

UTAMBULISHO
Mwenyekiti wa muda pia aliitumia fursa hii kumwomba na kumkaribisha Ndugu Edgar Kivenule ambaye ni Mkubwa wa Ukoo wa Kivenule waliishio Dar es Salaam, kutoa utambulisho kwa wajumbe waliojitokeza kuhudhuria mkutano huo.

Utambulisho ulianza kama ifuatavyo:
1. Christian Kivenule (Baba yake John toka Kidamale) anaishi Matombo, Morogoro
2. Adam Kivenule (Baba yake Alphonce toka Kidamale) anaishi Ubungo, DSM
3. Innocent Kivenule (Baba yake Mareh. Samwel toka Ilole) anaishi Ubungo, DSM
4. Edgar S. Kivenule (Baba yake Sigatambule toka Kidamale) anaishi Mwenge, DSM
5. Ignas Kivenule (Baba yake Pangayena toka Ilole) anaishi Tabata, DSM
6. Raphael Kivenule (Baba yake Pangayena toka Ilole) anaishi Club Oasis, DSM
7. Philemon Kivenule (Baba Mareh. Gwelino toka Ilole) anaisha Buguruni, DSM
8. Priskus F. Kivenule (Baba yake Mareh. Francis toka Magubike) anaishi Mbezi, DSM
9. Bakhita A. Kivenule (Baba yake Alphonce toka Kidamali) anaishi Ubungo, DSM
10. Tenus F. Kivenule
11. Valeria Kivenule (Mke wa Innocent Kivenule) anaishi Ubungo, DSM
12. Monica Kivenule (Baba yake Mareh. Francis toka Magubike) anaishi Zanaki, DSM
13. Phesto Ngimba
14. Hamidu Mtono (Baba yake Juma toka Nzihi) anaishi Kibamba, DSM
15. Athuman Mtono (Baba yake Juma toka Nzihi) anaishi Kibamba, DSM
16. Nuhu Js Mtono (Baba yake Juma toka Nzihi) anaishi Kibamba, DSM
 

DHUMUNI LA MKUTANO
Mwenyekiti alianza kuwaeleza wajumbe kwa kusema kuwa Wazo la Mkutano Mkuu wa Ukoo wa Kivenule, lilibuniwa na Ndugu Faustin Kivenule ambaye ni Baba yake mdogo pamoja na yeye mwenyewe Christian Kivenule, alipokuwa likizo kijijini, Kidamali mwishoni mwaka jana (2004). Mtu wa tatu kulipata wazo alikuwa ni ndugu Adam Kivenule, anayeishi Ubungo, mjini Dar es Salaam kutoka kwa Christian Kivenule mwaka huo huo wa jana.

Mambo mbalimbali yalijitokeza kutokana na wazo (kusudio) la kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule, Desemba 17-18, 2005 kijijini Kidamale. Kati ya mambo hayo ya msingi ni pamoja na suala nzima la mahusiano ndani ya wana ukoo, suala la elimu, suala la UKIMWI, kufahamiana na kuujua ukoo kwa ujumla, kufanya senza ili kujua idadi ya ndugu na mahali wanapoishi pamoja na mambo mbalimbali ambayo tunayategemea yatajitokeza.
 
Suala la Ukoo pamoja na Mahusiano baina ya wanandugu ndani ya ukoo, suala la elimu na gonjwa hatari la UKIMWI ni mambo ya msingi pia ni kiini na changamoto ya mambo mengi ambayo yatajitokeza katika mkutano huo mkuu. Mahusiano duni baina ya wana ndugu, kukosa kwa ushirikiano katika mambo mbalimbali ya kimaendeleo, kiuchumi na kijamii, matatizo ya kifamilia na kiukoo ni kati ya masuala msingi yaliyofikiriwa sana kabla ya kuletwa kwa wazo hili katika kikao hiki.

Mwelekeo wa ukoo wa Kivenule kuhusiana na suala nzima la Elimu hasa katika dunia hii ya Utandawazi (Globalization) ambapo dunia imekuwa kama kijiji kisicho na mipaka na kila mtu anaruhusiwa kuingia na kutoka, kuongezeka kwa viwanda vinavyotumia teknolojia ya hali ya juu, kuongezeka kwa teknolojia ya mawasiliano, kupanuka na kujengeka kwa miji, pamoja na soko huria. Mambo yote haya ndiyo yanayoweza kuonyesha mustakabali na nafasi ya ukoo wa Kivenule kwa maisha ya baadaye. Ilionekana kuwa ukoo wetu upo nyuma sana katika suala nzima la elimu, hii linajidhihirisha kutokana na kuwa na ndugu wachache sana ambao wameweza kupata elimu kwa kiwango kinachostahili. Hii ni hatari kwa sababu tunajenga ukoo tegemezi ambayo baadaye utakosa mwelekeo. Mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia yanayojitokeza kila kukicha yanaibadili dunia na hivyo kutulazimisha nasi katika ukoo wa Kivenule kubadilika. Matumizi ya teknolojia ya habari na mawasiliano katika simu za mikononi, computer, radio na satellite ni changamoto kwetu.

Maambukizo ya ugonjwa wa UKIMWI ambayo kwa kiasi kikubwa yameathiri familia nyingi zikiwemo familia zetu sisi wana ukoo, yanapaswa kutopuuzwa bali kuwekewa mikakati madhubuti. Ufahamu kuhusiana na gonjwa lenyewe livyoenea na madhara yake katika jamii, njia mbadala za kujilinda na maambukizi ya ugonjwa wenyewe pamoja na kuitikia mialiko mbalimbali ya wanajamii wanaopambana na janga hili ni mambo ya msingi sana ambayo yatajadiliwa kwenye mkutano huo.

Ilipendekezwa kuwa, wakati wa mkutano huo kutakuwa na nafasi kutoa uzoefu katika mambo mbalimbali ya kitaalum pamoja na mada ambazo tutazijadili kwenye agenda za mkutano huu wa leo, nazo zitawasilishwa kwenye mkutano huo.

Maandalizi ya mkutano mkuu wa ukoo yameanza mapema ili kutupa nafasi kubwa zaidi ya kujadili, kuandaa pamoja na kuwasilisha michango yetu ndani ya wakati unaotakiwa.

AGENDA ZA KIKAO
Agenda mbalimbali zilijadiliwa kwenye kikao zikiwa na mwelekeo na malengo mahususi ya kufanikisha kufanyika kwa mkutano mkuu wa ukoo. Agenda zilizojitokeza ni:-
1. Kuunda Kamati ya Maandalizi ya Mkutano huo itakayoratibu shughuli mbalimbali za wanaukoo wanaoishi Dar es Salaam.
2. Kulitoa kwa wajumbe wazo la Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule unaotegemewa kufanyika kijijini Kidamale, Desemba 17 – 18, 2005.
3. Mashauriano baina ya Ndugu wa Ukoo wa Kivenule waishio ILOLE, NDULI, ILULA NA ENEO LA KIDAMALI kama wanakubali kuwepo na kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Kwanza Ukoo wa Kivenule, hapo Desemba 17 hadi 18, 2005.
4. Kupitia viwango vya michango vilivyopendekezwa.
5. Kuweka Mikakati mbalimbali ya kufanikisha mkutano huo.
6. Kupitia Mada zilizopendekezwa kuwasilishwa kwenye Mkutano Mkuu.

KUJADILI AGENDA ZA MKUTANO
1. Kuunda Kamati ya Maandalizi ya Mkutano huo itakayoratibu shughuli mbalimbali za wanaukoo wanaoishi Dar es Salaam
Ndugu Ignas Kivenule alianza kwa kutoa mapendekezo kuwa Kamati iliyoandaa kikao cha kwanza cha maandalizi ya mkutano mkuu wa ukoo wa Kivenule iendelee kufanya kazi kwani imeshaonyesha nia. Pia Ndugu Edgar Kivenule alipendekezwa awepo mbele kwa waongoza mkutano kama kiungo muhimu cha wana ukoo waishio Dar es Salaam. Pia aliuliza swali, je kutakuwa na vikao vingapi kabla ya mwezi wa kumi (12) wakati wa Mkutano Mkuu?

Ndugu Edgar Kivenule alipendekeza kuwa kuundwe Kamati. Alipendekeza yeye awe mshauri tu katika masuala mbalimbali ambayo yatakuwa yanajitokeza kuhusiana na maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule, Desemba 17-18, 2005 kijijini Kidamale. Pia alishauri kupata viongozi ambao wataunda Kamati itakayokuwa na kazi ya kuyaratibu yote ambayo yatakuwa yanajadiliwa na wajumbe kuhusiana na maandalizi ya mkutano. Kazi nyingine ya kamati itakuwa kuwaunganisha ndugu wote wa ukoo wa Kivenule wanaoishi mjini Dar es Salaam na mikoa ya karibu pamoja na kushughulikia majukumu mbalimbali kama itakavyotakiwa kufanya hivyo. Alipendekeza achaguliwe Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu na Mweka Hazina.

Wajumbe waliochaguliwa kuunda Kamati ni:
1. Christian Kivenule Mwenyekiti
2. Athuman Mtono Makamu Mwenyekiti
3. Adam Kivenule Katibu
4. Innocent Kivenule Mweka Hazina
5. Edgar Kivenule Mshauri Mkuu wa Kamati

Ndugu Edgar Kivenule alipendekezwa kuwa Mshauri na Kiungo cha wanaukoo wa Kivenule wanaoishi Dar es Salaam na mikoa ya karibu.

Kuhusu suala vikao vingapi vitafanyika hadi mwezi wa kumi na mbili! Ilikubaliwa kuwa umuhimu wa vikao utatokana na mahitaji ya kamati ambayo ndiyo yenye jukumu kubwa la maandalizi ya mkutano mkuu. Kuchangamka au kudorora kwa maandalizi ya mkutano huo ndio kutakako amua ni vikao vingapi vifanyike.

2. Kulitoa kwa wajumbe wazo la Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule unaotegemewa kufanyika kijijini Kidamale, Desemba 17 – 18, 2005
Wazo la kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule lilikubaliwa na wajumbe wote.

3. Mashauriano baina ya Ndugu wa Ukoo wa Kivenule waishio ILOLE, NDULI, ILULA NA ENEO LA KIDAMALI kama wanakubali kuwepo na kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Kwanza Ukoo wa Kivenule, hapo Desemba 17 hadi 18, 2005
Wajumbe wote toka Ilole, Nduli, Ilula, Kidamali na Dar es Salaam walikubali kwa kauli moja umuhimu wa kuwepo kwa mkutano huo, pia waliaahidi kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule.

4. Kupitia viwango vya michango vilivyopendekezwa
Hapo awali ilipendekezwa kuwa kila mjumbe anayeishi mjini na wale wanaoishi vijijini wenye uhakika wa kipato pia watoe kiasi cha Tsh. 15,000.00; na vijijini watoe kiasi cha Tshs. 5,000. Kwa upande wa vijijini pia ilipendekezwa kuwa kwa wale wasio na uwezo wanaweza kutoa mifugo mfano kuku wawili au mifugo yoyote mingine. Na mwisho wa kutoa michango ilipendekezwa iwe mwezi wa tisa mwaka huu.

Kati ya wajumbe waliotoa/waliochangia mawazo yao alikuwa ni Priskus Kivenule wa Magubike ambaye aliahidi kutoa kiasi hicho licha ya kuwa na hali ngumu ya kiuchumi, lakini anadhani mkutano una umuhimu sana. Naye Rafaeli Kivenule toka Ilole, alihoji ni kiasi gani cha fedha kinakadiriwa kugharimu Mkutano huo mkuu? Mwenyekiti wa Kamati alifafanua kwa kusema, kiasi cha shilingi laki tisa na elfu kumi (910,000.00) kinakadiriwa kutumika baada ya kuchambua gharama za mahitaji na vitu mbalimbali ambavyo ni muhimu kuwepo kwenye mkutano huo mkuu.

Pia Rafaeli Kivenule aliuliza kama kutakuwa na wawakilishi wowote toka Dar es Salaam au kuna utaratibu gani wa kwenda kwenye mkutano huo? Mwenyekiti alimjibu kuwa toka Dar es Salaam au sehemu yoyote nyingine hakutakuwa na usafiri wa moja kwa moja. Ila kuna utaratibu umepangwa wa kuwa na usafiri kuanzia Iringa Mjini mpaka Kidamali kwa wageni mbalimbali wanaishi nje ya Kidamali. Kiasi cha Tshs. 50,000.00 kimewekewa bajeti kuwasafirisha wageni to ka Iringa mjini hadi Kidamali na 50,000 nyingine kuwarudisha toka Kidamali hadi Iringa mjini. Hakutakuwa na mwakilishi yeyote toka Dar es Salaam kwenye kwenye kikao hicho, ila kila ambaye atachanga kiasi cha Tshs. 15,000 atakuwa amejipa tiketi ya kushiriki na itabidi agigharamie nauli toka hapa hadi Iringa Mjini na toka Iringa Mjini hadi Dar es Salaam.

Swali jingine lilikuwa ni kigezo gani kimetumika kupitia viwango vya michango? Swali hili lilijibiwa na Mwenyekiti pamoja na Mshauri Mkuu, huduma mbalimbali zilizopendekezwa kuwepo kwenye mkutano mkuu ndiyo kigezo na utaratibu mahsusi uliotumika kupendekeza viwango vya michango. Pia Adam Kivenule, Katibu wa Kamati aliongeza kwa kusema kuwa makadirio yaliyopendekezwa mwanzo yanaweza yasikidhi haja, kwani kuna mambo mbalimbali yanaweza kujitokeza na hivyo kuongeza gharama. Hata hivyo kiwango cha michango kikizidi lengo hamna ubaya wowote, kuna ununuzi wa vifaa vya kudumu vitakavyotumika wakati wa shughuli. Tunategemea vifaa hivyo vitaendelea kutumika katika shughuli mbalimbali za kiukoo zitakazokuwa zinajitokeza kama misiba na masuala mengine ya kiukoo ambayo yatakuwa yanawakusanya ndugu wengi. Baadhi ya vifaa hivyo ni pamoja na vyombo vya chakula (sahani, vijiko, vikombe, sufuria, visu), viti (vya plastiki na mbao) pamoja, meza pamoja na magodoro.

5. Kuweka Mikakati mbalimbali ya kufanikisha mkutano huo
Mikakati mbalimbali imewekwa ili kufanikisha kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule. Kamati imepanga kuandaa kadi za kuchangisha michango ndani ya wanaukoo na nje ya wanaukoo. Mwenyekiti aliahidi kuwapelekea kadi ya kuomba michango Askofu wa Jimbo la Iringa Ngalaleku Mtwa pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Iringa. Pia kwa makadirio ya haraka haraka kama watapatikana watu 50 toka Dar es Salaam na wakalipa shilingi 15,000.00 kila mmoja, tunategemea kupata Tsh. 750,000.00. Kwa hiyo tutakuwa tunatakiwa kukamilisha kiasi cha Tshs. Tshs. 160,000.00. Kwa hiyo Kamati imeona ni vyema kama tarehe ijayo ya Februari 26, 2005 ya kufanya kikao, pia itumike kusambaza kadi za kuomba michango.

Mikakati mingine ni kuwahamasisha wale wenye uwezo kuchangia zaidi, na pia tunashauri wajumbe waangalie baadhi ya maeneo ambayo wanadhani kuna uwezekano wa kusaidiwa kama wakipeleka barua, miniti, kadi za michango pamoja na wazo zima la mkutano. Kupatikana kwa wingi wa michango kutasaidia pia kuboresha baadhi ya mambo/huduma ambazo zimeminywa kutokana na ufinyu wa bajeti.

Pia kamati itakayochaguliwa itakuwa na jukumu la kwenda kijijini Kidamali na vijiji vingine wanakoishi wana ukoo kwa lengo la kuwahamasisha jamii nzima ya ukoo ya Kivenule ione umuhimu wa mkutano huo, na pia ichukue jukumu la kuuchangia kwa namna moja au nyingine. Pia tutaandaa vipeperushi mbalimbali ambavyo vitakuwa ni sehemu ya hamasa pamoja na mabango ya kubandika sehemu mbalimbali vijijini yakiwa yamejaa ujumbe mzito kuhusiana na mkutano huo.


6. Kupitia Mada zilizopendekezwa kuwasilishwa kwenye Mkutano Mkuu
Mada zote zilizopendekezwa kuwasilishwa na kufundishwa kwenye mkutano mkuu, zilikubaliwa na wajumbe wa mkutano. Mwenyekiti wa Kamati alizitaja mada na wawezeshaji waliopendekezwa kusaidia ufanikishaji wa ufundishaji kuwa ni:-

Mada zilizopendekezwa:-
1. HISTORIA YA UKOO
• Ukoo ni Nini na Unapatikanaje?
• Dhana ya Kuenea na Kukua kwa Ukoo.
• Mgawanyiko wa Ukoo (Chora Mchoro Kuonyesha Ukoo unavyoundwa).
• Kupotea kwa Ukoo.

2. MAHUSIANO BAINA YA NDUGU NDANI YA UKOO
• Ukaribu wa Wana Ndugu.
• Ushirikiano Katika Nyanja Mbalimbali.
• Kutembeleana kama Sehemu ya Kudumisha Mahusiano.
• Kuondoa Tofauti na Kusaidiana.

3. ELIMU NA MUSTAKABALI WA UKOO
• Nafasi ya Ukoo wa Kivenule katika Elimu.
• Umuhimu wa Elimu.
• Dunia ya Utandawazi.
• Nini Kifanyike Kuinua Elimu Katika Ukoo Wetu.

4. UKIMWI NDANI YA UKOO NA ATHARI ZAKE
• UKIMWI ni nini?
• Namna gani UKIMWI unavyoenea/kuambukizwa?
• Njia Mbadala za Kujilinda na Maambukizi?
• Jukumu la Ukoo/Familia Kukabiliana na Janga la UKIMWI.

Wawezeshaji Waliopendekezwa:-
1. Agatha Mhapa
2. Alphonce Kivenule
3. Christian Kivenule
4. Donath Mhapa
5. Edger Kivenule
6. Florian Kivenule
7. Ignas Kivenule
8. Adam Kivenule
9. Innocent Kivenule
10. John Kivenule
11. Justin Kivenule
12. Lizeta Kivenule
13. Piera Kivenule
14. Siha Kivenule
15. Victoria Kivenule
16. Zavery Kivenule

Rafael Kivenule aliuliza kuhusiana na mada zilizopendekezwa kwenye mkutano mkuu wa Kidamale kama zitahusika na kwenye vikao vyetu vitakavyokuwa vinafanyika huku? Jibu lilikuwa kuwa Mada zinahusika kote kwani malengo ya mkutano mkuu ni yale yale ya kudumisha mahusiano, elimu, UKIMWI, kujuana na kusaidiana.

Mshauri Mkuu wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Ukoo uliufunga mkutano kwa kutoa nasaha mbalimbali ikiwemo kuujali na kuona umuhimu wa mikutano mbalimbali itakayokuwa inaitishwa na Kamati hii iliyoundwa. Pia alipendekeza kikao kingine kinachofuata kisiwe mbali sana na hiki cha mwanzo. Alisisitiza umuhimu wa kuwajulisha ndugu wengine ambao hawakuhudhuria waje na washirikiane na wajumbe wengine ambayo tayari wana taarifa.

Kikao cha pili cha Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule kilipendekezwa kifanyika tarehe 26 Februari 2005, saa 9.00 Ubungo, River Side Bar.

Kikao cha kwanza kilifungwa saa 12:58 jioni
Imetiwa Saini na:
____________________ _________________
Christian Kivenule Adam Kivenule
Mwenyekiti wa Kamati Katibu wa Kamati

_______________________
Edgar Kivenule
Mshauri Mkuu wa Kamati

http://www.kauki-kauki.blogspot.com/

HOTUBA YA UFUNGUZI WA MKUTANO MKUU WA TISA WA KAUKI



HOTUBA YA UFUNGUZI WA MKUTANO MKUU WA TISA WA KAUKI
JUNI 29 – 30, 2013, MAGUBIKE – IRINGA

Ndugu Mgeni Rasmi,
Ndugu Wageni Waalikwa;
Wanaukoo na Jamii yote inayounda KAUKI;
Ndugu Majirani, Marafiki na Jamii yote Iliyojumuika Nasi;
Mabibi na Mabwana;

Kamwene…, Munogage…, Makasi…,

Awali ya yote, nimwombe Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, uzima na Baraka, awape nguvu, afya na amani, wote mliokusanyika katika Mkutano huu wa 9 wa KAUKI.

Pili, nimwombe Mwenyezi Mungu, awaepushe na hatari, rapsah na ubaya wowote ulioelekezwa kwenu; awalinde kutoka saa hii ya ufunguzi wa Mkutano hadi kesho wakati wa kuhitimisha shughuli hii muhimu kwa mwaka huu 2013.

Tatu, nawaomba wote tusimame kwa dakika moja (1) kuwakumbuka ndugu zetu ambao wametangulia mbele ya haki kutoka mwaka jana hadi mwezi Juni mwaka 2013. Ndugu waliotangulia mbele za haki ni:
1.     Luhanage Ponsiano Sigatambule Kivenule
2.     Flomina Pangalas Kivenule
3.     Gidagumhindi (Cecilia) Sigatambule Kivenule
4.     Atanas
5.     Mzee wetu Babu Hussein Tavimyenda Tagumtwa Kivenule

Mwenyezi Mungu azilaze Roho za Marehemu mahali pema peponi, Amina.

Baada ya utangulizi huo mfupi, ni furaha kubwa kujumuika na hadhara hii siku ya leo.  Ni matumaini yangu kuwa wote ni wazima wa afya na pia uwepo wenu unaonesha namna mnavyothamini shughuli hii muhimu itakayofanyika kwa muda wa siku mbili; yaani leo na kesho, hali kadhalika kuhakikisha kuwa Mkutano Mkuu wa 9 wa KAUKI unafakiwa.   

Ni furaha iliyoje kuwa nanyi katika hadhara hii. Ni matumaini yangu kuwa, wote ni wazima wa afya na kuwepo kwenu pia kuonesha jinsi mnavyothamini shughuli ambayo tutaifanya kwa siku mbili, yaani leo na kesho katika kuhakikisha kuwa Mkutano Mkuu wa Tisa wa KAUKI unafanikiwa.

Ndugu Mgeni Rasmi;  nianze kutoa historia fupi ya umoja huu. KAUKI ni Umoja wa Ukoo wa Kivenule, ulioanzishwa rasmi mwaka 2005, kukabiliana na changamoto mbalimbali za maendeleo, zinazoikabili jamii inayounda umoja huu; hususani katika kujikwamua na ugumu wa maisha na pia kutumia fursa zinazopatikana ili kukabiliana na kuondokana na wimbi la umaskini, ujinga, maradhi na utegemezi. Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI), ulianzishwa rasmi mnamo Desemba 17 - 18, 2005 Kijijini Kidamali. Harakati za kuanzishwa kwa KAUKI zilianza mwezi Februari 06, 2005 Jijini Dar es Salaam kwa kufanya mkutano wa kwanza wa mashauriano. Harakati nyingine na kuunda kamati za maandalizi zilielekezwa upande wa Kidamali, Ilole na Nduli. Kwa upande wa Kidamali, Mkutano wa kwanza wa maandalizi ya Mkutano Mkuu ulifanyika mwezi Mei ambapo wajumbe toka Dar es Salaam walishiriki katika majadiliano, kuchagua viongozi wa kuunda kamati ya maandalizi na kuhamasisha.

Ndugu Mgeni Rasmi; Umoja wa Ukoo wa Kivenule ulizinduliwa rasmi mwaka 2006, katika Mkutano Mkuu wa Pili wa Ukoo wa Kivenule uliofanyika tarehe 24 – 25 Juni 2006 katika Ukumbi wa Sanga Kijijini Kidamali, Iringa. Kuzinduliwa kwa Umoja wa Ukoo wa Kivenule, kulienda sambamba na uzinduzi wa Mfuko wa Ukoo pamoja na Kuipitisha Rasimu ya Katiba ya Umoja wa Ukoo wa Kivenule na kuwa Katiba Rasmi; hivyo kutoa fursa ya kuanza kwa utekelezaji wa shughuli na mipango mbalimbali ya maendeleo. Pia, pamoja na mambo mengine, katika Mkutano Mkuu wa Pili wa Ukoo, kulifanyika uchaguzi wa Viongozi wa Kanda, uchaguzi wa Walezi wa Ukoo na hivyo utendaji rasmi wa KAUKI kuruhusiwa kuanza.

Ndugu Mgeni Rasmi; Huu ni Mkutano Mkuu wa Tisa wa KAUKI; na tayari mikutano mingine Nane imekwisha fanyika, mitatu kijijini Kidamali na mkutano moja kijijini Irole, Nduli Magubike, Igowole-Mufindi na Jijini Dar es Salaam. Huu ni mzunguko mwingine tena baada ya kumaliza kanda zote. Pengine mkutano huu utashauri namna nyingine ya uendeshaji wa mikutano ya namna hii.

Malengo ya KAUKI
Ndugu Mgeni Rasmi; malengo makuu ya KAUKI ni kujaribu kwa kila hali kwa kutumia ujuzi na maarifa, kuinua uwezo wa kielimu, kiuchumi na kimaendeleo, kwa wanajamii wanaounda umoja huo, kwa kutumia rasilimali mbalimbali zinazopatika katika nchi ya Tanzania na hususani katika maeneo wanayoishi; ikiwa ni pamoja kuihamasisha jamii hii kufanya kazi kwa juhudi na maarifa ili kupunguza umaskini unaowakabili.

KAUKI imeanzishwa kukidhi shida na mahitaji ya jamii iliyounda umoja huu na hususani katika maeneo lengwa ya elimu, afya, uchumi na maendeleo, kwa kushirikisha mawazo, fikra, ujuzi na maarifa ya kila mwanaukoo, katika mikutano mikuu na mikutano midogo midogo, ambayo inaandaliwa na wanaukoo wenyewe. Kwa kukutana pamoja, fikra za kujenga, ujuzi, uzoefu, kujengewa uwezo na maarifa, huunganishwa pamoja na kisha kupanga mikakati mbadala ya kuweza kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika maisha.

Ndugu Mgeni Rasmi; malengo KAUKI ni mengi na baadhi yake ni:
·         kuwa na ofisi yake Kijijini Kidamali na pia sehemu nyingine za Kanda
·         Kuisajili KAUKI na kuwa na mfuko wa kusaidia ndugu katika elimu, afya na matatizo mengine. Tayari mfuko umeanzishwa na unaendelea kuchangiwa. 
·         kuwa na sanduku lake la posta, tovuti. Kwa sasa ina tovuti  inayopatika kupitia www.tagumwafoundation.wetpaint.com na inaboreshwa kupitia www.tagumtwa.blogoak.com  na www.kauki-kauki.blogspot.com   
·         Kuwa na Akaunti katika Benki – tayari imefungua katika Benki ya NMB, Iringa Mjini
·         kuwa na vitendea kazi mfano Kompyuta, Printa, Simu, Meza na Viti
·         kuanza kutoa elimu mbalimbali kwa wadau wake. Inatoa elimu katika mikutano yake
·         kubuni na kutekeleza miradi ambayo itawasadia wanajamii. Mpango wa Mradi wa Alizeti-Irole, ambao bado haujaanza kutekelezwa.
·         kuwa na kitengo cha Utaalam wa Kitaaluma na Kiujuzi ambacho kitafanya shughuli za kuiletea fedha KAUKI, pamoja na miradi mbalimbali. Ipo katika mchakato.
·         Kuchapisha kitabu toleo la kwanza cha Umoja wa Ukoo wa Kivenule kwa kipindi cha mwaka 2009-2013. Kazi inaendelea na taarifa mbalimbali zinaendelea kukusanywa.

Mafanikio
Ndugu Mgeni Rasmi; KAUKI imefanikiwa kufanya yafuatayo:
·         kuendelea kufanyika kwa mikutano mkuu. Mikutano Mikuu nane tayari imefanyika Kidamali mara tatu, Irole, Nduli, Magubike, Igowole-Mufindi na mara moja moja.
·         kupanua wigo wa ushiriki kutoka Irole, Nduli, Itagutwa, Mgongo na Mufindi; Kilimanjaro, Dar es Salaam, Morogoro na maeneo mengine.
·         Kuongezeka kwa ufahamu na uelewa wa watu kuhusu KAUKI na mada zinazofundishwa
·         Kufahamiana baina ya wana-KAUKI kumeongezeka mara dufu
·         Kuanzishwa kwa Mfuko wa KAUKI
·         Imeanzisha blogs ambazo zinabeba taarifa mbalimbali za KAUKI na wana-KAUKI kwa ujumla.

Changamoto
Ndugu Mgeni Rasmi; Changamoto zinazoikabili KAUKI ni pamoja na
·         Ushiriki duni wa wanaukoo katika mikutano mikuu.
·         Kasi ndogo na moyo wa kuchangia mfuko wa kusaidia wanaukoo
·         Kutokidhi gharama za kuandaa mikutano hii kwa sababu michango inakuwa ni kidogo
·         Kutofikia malengo ya mipango tunayojiwekea
·         Ndugu wa mijini kuwa na mwamko mdogo wa kuunga mkono jitihada hizi

Matarajio katika Mkutano Mkuu wa Tisa wa KAUKI
Ndugu Mgeni Rasmi; Kama Ratiba inavyoonesha, hayo ndiyo yatakayofanyika katika siku mbili za Mkutano Mkuu wa Tisa wa KAUKI. Lakini, tunategemea kuwa na Mada kadhaa ikiwemo ya Chimbuko Historia ya Ukoo ambapo tutaijadili kwa undani zaidi. Lakini pia, masuala mengine mfano elimu, maendeleo na ushirikiano wa dhati baina ya wanandugu yatapewa kipaumbele.

Utambulisho baina ya wanaukoo utafanyika kwa kina na kila ndugu/mwanaukoo atakuwa na kitambulisho ambacho atakivaa kifuani kwake. Kutakuwa na fursa mbalimbali kwa wanandugu kupeana uzoefu mbalimbali wa utafutaji wa maisha bora. Mbinu za kujiinua kimaisha zitafundishwa na wadau wenye uzoefu pamoja na aina mbalimbali za miradi ambayo ndugu wanaweza kufanya.

Tutakuwa na kipindi cha kupeana uzoefu wa shughuli mbalimbali za kiuchumi kutoka katika maeneo mbalimbali ambako ndugu wanaishi. Kama ilivyofanyika katika Mkutano Mkuu wa Tatu, Nne, Tano, Sita, Saba na Nane wa KAUKI, maeneo yatakayotolewa uzoefu Kilimo, biashara na ajira kutoka katika maeneo mbalimbali. Kwa kupeana elimu ya ujasiliamali itasaidia kutufungua macho na hivyo kuongeza uwezo wa kufikiri na kwenda kutafuta maisha katika maeneo ambayo ni mbadala kwetu. Pia taarifa hizi zitawasaidia wanandugu toka maeneo mengine kupata mwanga wa shughuli mbadala zitakazosaidia kupata kipato na kuboresha maisha.

Matarajio ya Mbeleni
Ndugu Mgeni Rasmi; Mipango ya KAUKI kwa mwaka uliopita 2011 na 2012
·         Kuendeleza jitihada za kufungua ofisi Kidamali na kununua vifaa vya ndani ya ofisi kama vile kompyuta, printa na fenicha.
·         Kuchapisha kitabu cha historia ya wahehe ambapo ndani yake pia kutakuwa na taarifa za KAUKI.
·         Kuongeza wigo wa ushiriki katika mikutano; na
·         Kuhamasisha wana-KAUKI kuchangia mfuko

Hitimisho
Ndugu Mgeni Rasmi; KAUKI imeendelea kujikita katika kuongeza uangavu na weledi kwa wanaukoo kutokana na kutambua changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika dunia hii ya ushindani. Ugumu wa maisha, mfumuko wa bei, ukosefu wa ajira, na changamoto mbalimbali ambazo kila mwana-KAUKI anaiona, ameguswa nayo au kuathiriwa nayo. Tatizo la ufisadi wa raslimali za watanzania, rushwa katika huduma za jamii mfano kukosa dawa hospitalini, maji safi na salama, elimu duni na ukosefu wa ajira, vyote vinatuathiri sisi. KAUKI inaamini kuwa mwana-KAUKI mwenyewe ndiye mwenye uamuzi wa mwisho ya kuamua hatma na mustakabali wa maisha yake ya sasa na baadaye. KAUKI haitarajii maisha bora kwa kila mwana-KAUKI au mtanzania mwingine yataletwa na wanasiasa au watu baki waliopo nje ya nchi yetu. Jukumu la maendeleo ni letu sisi wenyewe. Ndio maana tunahimiza watu kujitoa kwa hali na mali kuuchangia mfuko wetu ili uweze kuisaidia jamii yetu katika nyanja zote za kiuchumi, elimu, afya na maendeleo.

Ndugu Mgeni Rasmi, baada ya kusema hayo machache, kwa niaba ya Kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu ya Kidamali, Iringa, inakuomba Ufungue Rasmi Mkutano Mkuu wa Tisa wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI).

Karibu Sana


Imetolewa na:

Ndugu Jovin Kivenule
Mwenyekiti wa KAUKI
Kwa Niaba ya Kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu  wa Tisa wa KAUKI

HISTORIA FUPI YA KAUKI



UTANGULIZI

Tembelea Blog ya KAUKI kwa taarifa mbalimbali za Ukoo wa Kivenule
KAUKI ni Umoja wa Ukoo wa Kivenule, ulioanzishwa rasmi mwaka 2005, kukabiliana na changamoto mbalimbali za maendeleo, zinazoikabili jamii inayounda umoja huu; hususani katika kujikwamua na ugumu wa maisha na pia kutumia fursa zinazopatikana ili kukabiliana na kuondokana na wimbi la umaskini, ujinga, maradhi na utegemezi. Kuanzishwa kwa KAUKI kuliambatana na maandalizi yaliyojumuisha mikutano zaidi ya 10 ya mashauriano iliyofanyika sehemu mbalimbali Jijini Dar es Salaam na Kidamali, Iringa.

Dira ya KAUKI
Kuwa na jamii elewa, angavu na inayowajibika kwa kujitegemea.

Maono ya KAUKI
Kujengeana uwezo kwa kutumia raslimali, stadi, ujuzi, maarifa na weledi, kupitia mafunzo, kongamano, mijadala na mikutano ili kuboresha maisha.

Malengo ya KAUKI
Lengo Kuu
Kuinua na kuboresha maisha ya wanaukoo wa Kivenule, kielimu, kiuchumi na kisayansi kwa kutumia ujuzi, maarifa na raslimali zinazotunguka.

Malengo mengine mahsusi
§        Kuujua na kuelewa kwa kina Chimbuko na Historia ya Ukoo wa Kivenule;
§        Kuzikusanya, kuziratibu na kuzihifadhi kumbukumbu mbalimbali za Ukoo wa Kivenule.
§        Wanaukoo kupata fursa ya kufahamiana na kutambuana;
§        Kufanya senza ya ndugu/wanaukoo wanaounda Ukoo wa Kivenule kila inapobidi kufanya hivyo na Senza hiyo itajumuisha watu waliohai na wafu;
§        Kuanzisha Mfuko wa Ukoo wa Kivenule utakaosaidia kuinua kiwango cha Elimu na pia kusomesha wanaukoo wasio na uwezo wa kumudu kulipa ada za shule au vyuo;
§        Kuboresha Elimu ndani ya Ukoo wa Kivenule ili ndugu/wanaukoo wawe na uelewa wa hali juu na kumudu mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia katika Dunia ya Utandawazi;
§        Kusuluhisha na kutatua matatizo yanayojitokeza katika Ukoo wa Kivenule kwa kupitia vikao vinavyokubalika;
§        Kuelimisha Wanaukoo/ndugu kuhusiana na madhara ya ugonjwa wa UKIMWI, matumizi ya Madawa ya Kulevya na Ulevi wa kupindukia;
§        Kuinua viwango vya maisha vya wanaukoo wa Kivenule na kuishi maisha mbadala yenye milo kamili, furaha na nyumba bora na nadhifu;
§        Kuongeza na kuimarisha mahusiano mazuri ndani na nje ya ukoo kwa kushirikiana katika matatizo mfano raha, ugonjwa, misiba pamoja na majanga makubwa;
§        Kuwa na nguvu ya kurekebisha tabia zisizostahili kwa wanaukoo/ndugu ndani ya Ukoo na kutafuta suluhu ya migogoro/migongano baina ya mtu au jamii inayotuzunguka;
§        Wanaukoo kuutambua na kuuelewa mtawanyiko/mgawanyiko wa Ukoo wa Kivenule;
§        Wanaukoo/ndugu kushirikiana katika shughuli za uzalishaji mali pamoja na utendaji kazi wa kila siku;
§        Kushirikiana na umoja au vikundi vingine vilivyoungana ili kuuletea Ukoo wa Kivenule maendeleo endelevu;
§        Kuanzisha Mfuko wa kukopeshana (SACOSS); na
§        Kupunguza au kuondoa kabisa tabia ya uvivu na uzembe ndani ya Ukoo wa Kivenule.

Muundo wa KAUKI
KAUKI inaundwa na Kanda sita ambazo ni Kidamali, Irole, Nduli, Magubike, Mufindi na Dar eS Salaam. Kwa mujibu wa Katiba ya KAUKI, kuna Mkutano Mkuu ambao ndio mkutano mkubwa kuliko yote. Hufanyika mara moja kwa mwaka. Pia KAUKI ina mikutano ya Kamati ya Utendaji ambayo hufanyika mara nne kwa mwaka kwa vipindi vya miezi mitatu mitatu. Katika Kanda pia kuna mikutano midogo midogo ambayo jukumu lake ni kujadili masuala yanayohusiana na maendeleo ya kanda. Muundo wa Uongozi wa KAUKI upo kama ifuatavyo:

Nafasi za Uongozi Mkuu wa KAUKI
§        Mwenyekiti:                  Donath P. Mhapa       0658 843 565
§        Makamu Mwenyekiti:     Christian J. Kivenule   0714 146 382
§        Katibu Mkuu:                        Adam A. Kivenule       0713 270 364
§        Mweka Hazina               Justin D. Kivenule      0784 855 739

Nafasi za Uongozi wa Kanda
Kila kanda ina kiongozi wake ambaye ni Mwenyekiti, ambaye naye husaidiana na Katibu. Pia ndani ya Kanda kuna viongozi wa Kamati mbalimbali ambazo zipo kwa mujibu wa Katiba ya KAUKI.
Katiba ya KAUKI ndiyo mwongozi mkuu wa shughuli zote zinazofanywa na umoja huu. Katiba ya KAUKI ilipitishwa rasmi katika Mkutano MKuu wa Pili wa KAUKI uliofanyika Kidamali, Iringa.

Historia Fupi ya Kuanzishwa kwa KAUKI
Harakati za kuanzishwa kwa KAUKI zilianza kwa kuratibu mawazo ya wana-ukoo wawili, yaani Ndugu Faustino Kivenule na Ndugu Christian Kivenule mwezi Desemba 2004. Mawazo hayo yalifanyiwa kazi kwa kumshirikisha pia Ndugu Adam Kivenule, ambaye bila kuchelewa, waliweza kuandaa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Mashauriano, Jijini Dar es Salaam. Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa River Side, tarehe 6 Februari, 2005 – Jijini Dar es Salaam.

Harakati nyingine za maandalizi zilielekezwa upande wa Kidamali, Irore na Nduli. Kwa upande wa Kidamali, Mkutano wa Kwanza wa Mashauriano kwa ajili ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule, ulifanyika mwezi Mei ambapo wajumbe toka Dar es Salaam walisafiri kwenda huko ili kuwasilisha hoja, kufanya mashauriano na majadiliano, kuchagua viongozi wa kusimamia uratibu na kuunda kamati ya maandalizi.

Maeneo mengine kama Nduli na Irore hazikuweza kufanya maandalizi ya moja kwa moja japo taarifa toka Dar es Salaam ziliweza kufikishwa na baadhi ya wanaukoo wanaishi huko. Mjumbe mmoja tu ndugu Augustino Kivenule, toka Mgongo, Iringa ndiye aliyeweza kumudu kushiriki katika Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule.

Mkutano Mkuu wa Tisa wa KAUKI
Huu ni Mkutano Mkuu wa Tisa wa KAUKI ambao unafanyika nyuma ya mikutano mingine Nane ambayo imekwisha fanyika, mitatu Kijijini Kidamali na Mkutano moja moja Kijijini Irole, Nduli, Magubike (Iringa Vijijini), Igowole (Mufindi) Mkoani Iringa, na Mkutano mmoja Jijini Dar es Salaam (Karibu na Tabata Shule). Kwa mujibu wa makubaliano na utaratibu ambao umewekwa na Wana-KAUKI, mikutano hii itakuwa inafanyika katika ngazi ya Kanda, ili kuipa fursa jamii inayounda KAUKI kushiriki moja kwa moja. Lakini pia, vipaumbele huwekwa pale ambapo kuna idadi kubwa ya wana-KAUKA, lakini huridhiwa wakati wa Mkutano Mkuu. Kwa msingi huo, Mkutano Mkuu wa Nane wa KAUKI, kwa kauli moja, uliazimia kuwa Mkutano Mkuu wa Tisa ufanyike katika Kanda ya Kidamali, Iringa Vijijini, tarehe 29– 30 ya Juni, 2013.

Angalia picha za matukio katika Mkutano Mkuu wa Nane wa KAUKI uliofanyika Jijini Dar es Salaam, Juni 30 - Julai 1, 2012
http://www.facebook.com/photo.php?fbid=497523093617046&set=a.497521733617182.1073741825.100000780786862&type=1&theater

Kwa taarifa zaidi, angalia http://www.tagumtwa.blogoak.com http://www.facebook.com/tagumtwa na http://www.twitter.com/tagumtwa 

TANGAZO

MKUTANO WA TISA (9) WA UMOJA WA UKOO WA KIVENULE-KAUKI

Uongozi wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI), kwa heshima na taadhima, unachukua fursa hii kuwatangazia Wana-KAUKI wote, Ndugu, Jamaa na Marafiki, wanaoishi mijini na vijijini kutoka katika Mikoa yote ya Tanzania Bara; Mkutano wa Mkuu wa Tisa (9) wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI), utakaofanyika katika Kijijini Kidamali, Wilayani ya Iringa Vijijini, Mkoani Iringa; kuanzia tarehe 29 - 30 Juni, 2013.

Wana-KAUKI Wote na Wapenda Maendeleo kwa Ujumla, na wale wote wanaoguswa na harakati zetu, wanaombwa kusaidia maandalizi ya Mkutano huo kwa kuchangia fedha, nafaka na raslimali nyingine, ambazo zitasaidia kufanikisha kufanyika kwa mkutano huo, pamoja na huduma muhimu kama chakula, kabla, wakati na baada ya Mkutano huo, kwa wageni wote.

Kwa niaba ya Kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 9 wa KAUKI, inakuomba/inawaomba

Pia nachukua fursa hii kuwakaribisha jamaa na marafiki ambao wanapenda kujifunza namna KAUKI inavyofanya kazi kwa kipindi cha miaka 8, toka umoja huu ulipoanzishwa rasmi mwaka 2005.

Kwa taarifa na mawasiliano unaweza kutufikia kupitia.
Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI)
Kando ya Barabara ya Hifadhi ya Ruaha
Sanduku la Posta 193
Kidamali, Iringa
Simu: +255 713 270364 (Katibu Mkuu-KAUKI)
Barua-pepe:        kauki2006@gmail.com
                            kivenule@gmail.com
                            tagumtwa.kauki@gmail.com
Blogu:        http://www.kauki-kauki.blogspot.com
                  http://www.tagumtwa.blogoak.com
                  http://www.tagumtwafoundation.wetpaint.com

Twitter:      https://twitter.com/kivenule
Facebook: https://www.facebook.com/kivenule
 

Natanguliza shukrani zangu za dhati,

Wako katika kazi,

Adam Kivenule
KATIBU MKUU-KAUKI



KUMBUKUMBU YA MZEE XAVERY SIGATAMBULE KIVENULE

WITH GREAT MEMORY OF MY LATE YOUNG FATHER, XAVERY SIGATAMBULE TAVIMYENDA KIVENULE, who passed away in April 2012. My late father hosted the 7th KAUKI ANNUAL GENERAL MEETING, at Igowole-Mufindi, Iringa. Open this link to see photos taken during the burial ceremony at Igowole, Mufindi.

https://www.facebook.com/kivenule/media_set?set=a.345508532151837.70482.100000780786862&type=1