Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Monday 29 October 2012

Mikasa ya Soko Kuu la Mwanjelwa

Ni mwaka wa tatu sasa toka Soko la Mwanjelwa lianze kujengwa upya baada ya ajali ya moto iliyowapatia hasara kubwa wafanyabiashara wa Mbeya kwa kuunguliwa bidhaa na mazao mbalimbali ya biashara, yaliyokuwemo katika soko hilo.

Wengi wao walitarajiwa kuwa ujenzi wa soko ungeenda haraka kutokana na umuhimu na mahitaji makubwa ya soko hili kwa wakazi wa Mbeya, mikoa ya karibu na nchi jirani za Zambia na Malawi.

Hali imekuwa tofauti kwa sababu sasa ni mwaka wa tatu tangu ujenzi uanze huku shauku kubwa kwa wafanyabiashara ikilitaka liishe mapema na waingie kuendeleza biashara zao.

Mkoa wa Mbeya ni Jiji linalokua kwa kasi na matarajio wengi kuboreka kwa miundo mbinu na masoko ya biashara kama kichocheo cha uchumi.

Je, pamoja na jitihada mpya ya kulijenga soko hili, je litaweza kumudu majanga ya moto ambayo yamekuwa yakilikumba soko hilo mara kwa mara. Hili ndilo swali kubwa ambalo linapaswa kuulizwa na kila mmoja wetu mpenda maendeleo. Tusubili tuone mara baada ya kukamilika na kuanza kutumika.

Zifuatazo ni baadhi ya picha zilizopigwa kuonesha ujenzi wa Soko la Mwanjelwa ukiendelea....









No comments:

Post a Comment