Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Sunday 10 January 2016

KISA MKASA

Ilikuwa siku iliyochosha sana, mvua kubwa ilikua ikinyesha ikiambatana na radi, ngurumo na miale isiyokwisha. Niliingia nyumbani mishale ya saa tano na nusu usiku. Nilikuwa nimechoka mno!! Nyumbani nilikuta ukimya usio wa kawaida huku nikipokelewa na kiza tororo "Maria! Maria!" niliita jina la mke wangu lakini sikupata muitikio wowote.Nikiwasha taa na kumkuta akiwa amelala ktk kochisebuleni.Kwa vile nilikua na njaa nilienda kula chakula alichoniandaliakilichokuwa mezani, sikutaka kumsumbua kumuamsha. Baada ya kula nilienda kuoga na nikaenda kulala. Kwa vile nilikuwa nimechoka nilipitiwa na usingizi mzito mno! Niliamshwa asubuhi na miale ya mwanga wa jua laasubuhi. Niliangalia muda na kukuta nikiwa nimechelewa kwenda kazini. Lakini kwa vile nilikua nimejiajiri sikuona kama itakuwa shida.Niliamka kivivu na kuanza kumuita maria lakini sikupata muitikio wowote pia, nilitoka nje na kumuangalia ila sikumkuta, nikajua atakuwa ashawahi kwenda kazini na hakutaka kunisumbua kuniamsha. Nilioga na nikala kifungua kinywa alichokua ameniandalia. Nilihisi hali ya tofauti kuhusu Maria. Miaka yetu mitano ya ndoa siku zote tumekuwa tukiongea wote kabla ya kwenda kazini. Na leo imekuwaje hali hii!? Nilipata wasiwasi sana.Baada ya kumaliza kifungua kinywa nilimpigia simulakini hakupokei nilifanya hivyo mara kadhaa lakinihakupokea hata mara moja. Niliumia mno moyoni.Nikaamua kwenda kazini. Huko kazi hazikwenda muda wote nilikuwa nikimkumbuka mke wangu. Watu wanasema ukimkumbuka mtu sekunde huwa kama mwaka. Niliamini huo msemo. Kila muda nilikuwa nikiangalia muda na simu yangu labda nitapata simu ya mke wangu lakini haikuwa kama nilivyotarajia.Niliumia sana. Nilikuwa nampenda sana mke wangu na sikujua kwanini amebadilika ghafla namna hiyo!Nilimaliza kazi zangu na kuondoka ofisini straight to home huku nikiwa na hamu ya kumuona mke wangu. Nikifika home na kupokelewa na binti yangu wa miaka mitatu. Alifurahi kuniona nikampachocolate na kumuuliza wapi mama. Alinionesha kuwa yuko jikoni. Nilikimbia haraka kuelekea jikonikama fisi aliyeuona mfupa. Nilimuona akiwa anaandaa chakula cha jioni. Nilinyata taratibu na kumkumbatia kwa nyuma. Ajabu hakuonesha kustuka wala kufurahia jambo lile. Alinisukuma nyuma na kuondoka jikoni. Sikumuelewa kwa kweli. Nilichanganyikiwa!!Siku zilisonga akizidi kujiweka mbali na mimi. Nikimuuliza kwanini sikupata jibu lolote la maana. Mapenzi yanauma sana. Hauwezi amini jinsi nilivyokonda kwa hizo siki chache. Nilimmiss mke wangu sio kidogo. Ufanisi wa kazi ulipungua sana. Alianza tabia ya kuwahi kwenda kazini na kuchelewa sana kurudi! Sikuweza kupata sababu yoyote ya maana!!Nilirudi nyumbani kama siku zingine za kawaida, nikijua nitamkuta Maria amelala kama kawaida, ila bahati nzuri nilimkuta akiwa macho sebuleni akionekana kunisubiri mimi. Nilifurahi walau sasa naweza pata wasaa wa kuzungumza nae. Aliinuka na kuja kunipokea begi langu la kompyuta pakato. Niliiona huzuni kubwa machoni mwake. Nilitaka kumkumbatia lakini alinikwepa na kwenda kukaa ktk kochi.Nilikaa karibu yake! "Nafikiri sikupendi tena David, nahitaji taraka yangu" moyo wangu ulinipasuka kupita maelezo ni kama fundi wa tanesco au kishoka anapopigwa na shoti ya umeme wa gridi ya taifa. Nilihisi sikusikia vizuri analosema. Nilimuuliza kama anajua analoongea. Akashikilia msimamo wake kwamba anataka taraka kwa kuwahanipendi tena. Niliinuka bila kumsemesha chochote nikaelekea chumbani kwangu. Mwanaume Nililia sana, niliumia moyoni, nilimpenda mke wangu mno!! Yeye ndiye aliyekuwa furaha yangu. Sasa bila sababu yoyote ya msingi anataka taraka yake. Niliangalia ni wapi nimemkosea sikuona kosa lolote! Au amepata mchepuko? Kwa kweli sikujua ni nin kimempata....nikazama ktk mawazo mazito.Nilikumbuka jinsi tulivyoonana kwa mara ya kwanza chuo kikuu cha Dar es salaam wote tukiwa wanafunzi mwaka wa kwanza, nikakumbuka jinsi mapenz yetu yalivyopitia vikwazo vingi ikiwemo wazazi wake kunikataa kabisa pale nilipoenda kumchumbia. Nikakumbuka jinsi alivyotoroka kwao na kuja kuishi na mimi ktk chumba changu kimoja huko kigogo sambusa.Nikakumbuka jinsi alivyozozana na wazazi wake mpaka akawaambia kama laana wampe tu, kwani ashakuwa kichaa juu ya kunipenda mimi. Leo hii tumeishi wote ktk shida mpaka mwenyezi Mungu ametujalia utajiri ambao tumeusotea wote. Hanitaki tena!!Sikumuelewa!Nililia mno!! Wala hakuja kunifuta machozi. Nikajua kweli amemaanisha na hanipendi tena. Nilipitiwa na usingizi.!Asubuhi niliamka na kumkuta akiwa pembeni yangu, safari hii akiwa na karatasi za kutia sahihi ya taraka. Sikumuelewa kwa kweli. Sikukubali kumpa taraka.Nilijiandaa nikaenda kazini! Kazi hazikuwa rafiki kwangu hata kidogo nilikuwa ktk mtihani mzito sanaa! Niluamua nirudi tu nyumbani nikaongee nae labda atanielewa.Nilipokelewa na ukimya usio wa kawaida. Nilimuitamke wangu lakini sikupata muitikio wowote. Nilienda chumbani moja kwa moja na kumkuta akiwa amelala huku uzuri wake ukijionesha dhahiri, nilijiambia kuwa nitajilaumu kama nikikubali kumpa taraka mke wangu mzuri aliyenivutia miaka yote kiasi hiki. Alikuwa amelala huku amekumbatia fremu kubwa yenye picha yangu. Nikahisi kuwa kumbe bado ananipenda.! Nilimshtua lakini hakuamka nilimtikisa lakini hakuonekana kushtuka. Nilimgusa ktk shingo na kumuona akiwa wa baridi mno. Sikutaka kuamini ninachokiona!Niliinua ile picha na mara ikaanguaka karatasi, ulikuwa ni ujumbe alioundika mke wangu na ulisomeka hivi.Mpendwa mme wangu David.Naandika kwa masikitiko makubwa waraka huu. Sijawahi kuona upendo wa dhati kama ulionao mume wangu. Nimekuwa nikikupenda sana ulikamilisha asilimia zote za maisha yangu. Kuwa na wewe nilijihisi ni mwanamke mwenye bahati sana ambaye amepata kuishi ktk ulimwengu huu. Hata hvyo nasikitika sana kwa kukatisha furaha hii kubwa tuliyokuwa nayo. Vituko vyote nilivyokuwa nikikufanyia ilikuwa na katika harakati za kukuwezesha kuishi bila mimi tena. Kwani nahisi ingekuwa tabu sana kwako kama ningeondoka ghafla!Ukweli ni kwamba siku ile uliponituma kusimamia mradi wetu wa kule morogoro wewe ukiwa nje ya nchi, wakati nikirudi Dar es salaam gari liliniharibikia. Kwa vike nilichelewa kuondoka Morogoro kiza kilikuwa kimeshaingia. Na kulikuwa kukitisha mno! Ghafla nilivamiwa na vijana wanne ambao mpaka sasa siamini kama walikuwa ni vibaka kwani hawakuniibia chochote. Walichofanya ni kwamba walinibaka kwa zamu na kwa vile walikuwa na mapanga sikuweza kupiga kelele kwa kuhofia kuchalazwa mapanga. Nilijihisi kutendewa unyama mkubwa!!Walivyomaliza walitokomea wakiniacha nikiwa na maumivu makali mno. Bahati nzuri niliomba msaada wa dereva wa lorry ambaye pia alikuwa naujuzi wa utengenezaj wa magari gari likatengamaa na nikarudi Dsm. Tukio lile halikukaa kufutika kichwani mwangu na kwa bahati mbaya nilivoendakupima nikakukutwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi. Ndio maana kwa miezi mitano nimekuwa nikikukwepa bika ya kushirikiana na wewe.Sijaona sababu ya mimi kuendelea kuishi, sina furaha tena. Nimejiona sina thamani tena ktk ulimwengu huu. Wewe bado ni kijana siwezi kukuua na kukatisha zile ndoto zetu tulizokuwa tukizipanga pamoja.Jambo moja tu. Naomba umtunze binti yetu kama ulivokua ukiniambia kuwa utakuwa baba bora kwake basi endelea kuwa hivyo hvyo! Akiniulizia mwambie mama ametangulia kwa Mungu tutaenda kumuona huko siku ikifika.Nakupenda David!Wasaalam Maria!Nililia! nililia! Sikuamini maisha yalivyonibadilikia kwa kasi mno, niliwalaani wabakaji wote duniani! Niliwachukia mno.Mpaka leo naandika haya binti yangu ana miaka 20, akiwa mwaka wa pili chuo kikuu cha Dar es salaam akisomea shahada ya sayansi ya uhandisi. Sijawahi kifikiria suala la kuoa tena. Nimekuwa nikimlea binti yangu mwenyewe. Yeye ndio zawadi pekee ambayo mke wangu Maria ameniachia na furaha yangu iliyobaki duniani.Napenda kuwaambia ubakaji bado umeshamiri Hapa Tanzania na duniani kote. Ni vema tukajikita katika kupambana na hali hii. Wahanga bado ni wengi, muda mwingine wanawajua waliowafanyia unyama lakini kwa vile wanapokea vitisho wamekuwa kimya tu.

No comments:

Post a Comment