Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Sunday 10 January 2016

MAAJABU YA MUNGU

Ilikuwa ni mwaka 1979, nikiwa nasafiri kutoka Dares salaam kwenda Arusha. Sijui ilikuwaje, lakiniilitokea. Tuliondoka Dar es salaam saa 12:30jioni. Wakati ule mabasi yalikuwa yakisafiri jionina usiku, siyo kama siku hizi.Nilikuwa nakwenda Arusha kwenye usaili kwa ajiliya ajira, nikiwa ndo kwanza nimemaliza kidatocha nne. Niliajiriwa moja kwa moja serikalini,kwani siku zile ajira zilikuwa ni za kumwaga.Hata hivyo, sikulizishwa na kazi niliyokuwanafanya, hivyo niliomba kazi kwenye kampunimoja kule Arusha na niliitwa kwa usaili.Tulifika mji unaoitwa Korogwe, ambao wakati uleulikuwa ndiyo mji maarufu kwa hoteli zake katikabarabara yote ya Segera hadi Moshi na Arusha.Tulipofika Korogwe, basi lilisimama kwa ajili yaabiria kupata chakula. Niliingia kwenye hotelimoja ambayo nakumbuka hadi leo kwamba,ilikuwa ikiitwa Bamboo. Niliagiza chakula na kulaharaka kutokana na muda mfupi wa kulauliotolewa na wenye basi la TTBS ambalo ndilonililosafiri nalo.Wakati wa kulipa ndipo niliposhangaa nakuogopa. Niliingiza mkono mifukoni na kukutakwamba, sikuwa na hela. Nilianza kubabaika namwenye hoteli alisema hawezi kukubali ujingahuo. "Abiria wengine wahuni bwana, anakula nakujifanya kaibiwa, ukikubaliana nao kla sikuhasara tu." Mwenye hoteli alisema kwakudhamilia hasa.Kulizuka zogo kubwa, huku mwenye hotelakisema ni lazima anipeleke polisi. Ni kweli,alimtuma mmoja wa watumishi wake kwendakituo cha polisi ili nishughulikiwe.Hapo hotelinikulikuwa na bwana mmoja aliyekuwa amekaapembeni na mkewe na mtoto wao wakila. Yulebwana alipoona vile, alimtuma mhudumu mmojaaniiite. Niliondoka pale kaunta nilipokuwanabembeleza na kuja kwa yule bwana.Alikuwa ni kijana mtu mzima kidogo, mwenyemiaka kama 50 hivi. Nilimsalimia na aliniitikia.Nilimsalimia mkewe pia. Yule mtu aliniuliza kisacha vurugu ile na nilimsimulia. Aliniuliza sasahuko Arusha ningeishi vipi wakati wa usaili kamanilikuwa nimeibiwa fedha zote, na ningerudi vipiDar es salaam. Nilimwambia nilikuwa napangakuangalia namna ya kurudi Dar es salaam, kamahuko polisi ningeaminika.Kama mzaha, bwana yule aliniambia angenipafedha za kutumia huko Arusha na nikirudi Dar essalaam, nimrudishie fedha zake. Nakumbukaalinipa shilingi 90 kwa ahadi kwamba nikirudi Dares salaam, nimpelekee pesa zake ofisini kwake.Alinielekeza ofisini kwake, mtaa wa Nkurumah nakuniambia kwamba, ameamua kunisaidia kwasababu, kila binadamu anahitaji msaada wamwingine na maisha haya ni mzunguko.Nilishukuru na kuondoka kukimbilia basini. Basililikuwa linanisubiri mimi tu. Nilipanda ndani yabasi na abiria wengine walinipa pole. TuliondokaKorogwe, lakini haikuchukuwa muda kabla basiletu halijapata tatizo la pancha ya gurudumumoja la mbele. Ilibidi tuegeshe pembeni ililitengenezwe. Baada ya matengenezo, tuliondokakuendelea na safari yetu.Karibu na mji wa Same kwenye saa saba usiku,basi letu lilisimama ghafla. Abiria walisimamandani ya basi na kulizuka aina ya kusukumana.Huko nje kulikuwa na ajali. Abiria tulishukaharaka na wengine huko chini walishaanza kupigamayowe, hasa wanawake. Niliposhuka niliona garindogo nyeusi ikiwa imebondeka sana na hapokando kulikuwa na maiti wawili.Nilijua ni maiti kwa sababu, walikuwawamefunikwa gubigubi. Halafu kulikuwa nakatoto kalikokuwa kanalia sana, kakiwakamefugwa kanga kichwani. "Tumwahishe huyumtoto hapo Same hospitalini, ameumia, ingawasiyo sana". Nilikatazama kale katoto ka kiumekenye umri wa miaka kama mitatu. Kalikuwakameumia kwenye paji la uso, lakini kalikuwa hai.Bila shaka, wale walikuwa ni wazazi wake,kalikuwa yatima tayari. Machozi yalinitoka.Baada ya kutoa msaada na askari wa usalamabarabarani kuchukua maiti wale, tulipanda basinikuanza safari yetu. Kale katoto kalichukuliwa najamaa fulani waliokuwa na Landrover ya serikalikukimbizwa hospitalini. Ndani ya basimazungumzo yalikuwa ni kuhusu ajali ile tu, haditunafika Arusha. Tulichelewa sana kufika Arushakwani tulifika kwenye saa tano asubuhi, badalaya saa mbili.Nililala kwenye hoteli rahisi na kufanya usailikesho yake. Ni hiyo kesho, baada ya usaili,niliponunua gazeti ndipo nilipata mshtukomkubwa ajabu. Kumbe wale watu wawiliwaliokufa kwenye ajali ile ya Same walikuwa niYule bwana aliyenisaidia hela na mkewe. Yulemtoto wao ndiye aliyeokoka. Niligundua hilobaada ya kusoma jina lake na jina la Kampunialiponiambia nimpelekee fedha zake nikirudi Dar,pamoja na picha yake, mke na mtoto. Nililia sanakama mtoto.Nilishindwa kujua ni kwa nini ilikuwa afe.Nilijiuliza ni nani sasa ambaye angemlea mtotoyule? Yalikuwa ni maswali yasiyo na majibu napengine ya kijinga pia. Nilijua kwamba, nilikuwa nadeni, deni la shilingi tisini zilikuwa ni sawa nashilingi laki moja za sasa. Kwa mara ya kwanzasasa nilijiuliza ni kwa nini marehemu Yulealiniamini na kuamua kunipa fedha zile. Sikupatajibu.Nilikata kipande kile cha gazeti la kiingerezakilichokuwa na habari ile. Nilichukua kipandehicho na kukiweka kwenye diary yangu. Deni,ningelipa vipi deni la watu? Nilijikuta nkipigamagoti na kuomba. Niliomba Mungu anipe uwezowa kuja kulilipa deni la mtu yule mwema. "Kwanjia yoyote Mungu naomba uje uniwezeshekulilipa kwa sura na namna ujuavyo wewe.Nataka kulilipa ili nami niwe nimemfanyia jambomarehemu." Niliomba. Nilirejea Dar es salaamsiku hiyohiyo.Kwa sababu ya mambo mengi na hasa baada yamatokeo ya usaili ule kuwa mabaya kwangu,nilijikuta nimekuwa na mambo mengi na kusahauharaka sana kuhusu mtu yule aliyenisaidia.Nilifanikiwa hata hivyo kupata nafasi ya kwendakusoma Chuo cha Saruji na baadaye chuo chaUfundi na hatimaye nilibahatika kwendaUingereza. Mwaka 1991, nilianza shughuli zangu.Ilikuwa ni mwaka 1995, nikiwa ofisini kwangupale jengo la Nasaco, ambalo liliungua mwaka1996. Nikiwa nafanya kazi zangu niliambiwa naseketari wangu kwamba kulikuwa na kijanaaliyekuwa anatalkka kuniona. Nilimuuliza ni kijanagani, akasema hamjui. Nilimwambia amruhusuaingie. Kijana huyo aliingia ofisini. Alikuwa kijanamdogo wa miaka 17 au 18 hivi, mweupe mrefukidogo. Alikuwa amevaa bora liende, yaanihovyohovyo huku afya yake ikiwa hairidhishisana.Nilimkaribisha ili mradi basi tu, kwani nilionaatanipotezea bure muda wangu. Ni lazima niwemkweli kwamba, sikuwa mtu mwenye hurumasana na nilikuwa naamini sana katika watuwenye pesa au majina. Nilimuuliza, "nikusaidienini kijana na ukifanya haraka nitashukuru maananina kikao baada ya muda mfupi." Nilisema nasikuwa na kikao chochote, lakini nilitaka tuaondoke haraka."Samahani mzee, nilikuwa na shida.Nina..nimefukuzwa shule na sina tena mtu wakunisaidia kwa sababu…Nime…nkokidato cha pilina hivyo natafuta tu kama atatokea mtu…"Nilimkatisha, "sikiliza kijana. Kama huna jambolingine la kusema, ni bora ukaniacha nifanye kazi.Hivi unafikiri kama nikiamua kumsaidia kila mtualiyefukuzwa shule, si nitarudi kwetu kwa mguu!Nenda Wizara ya Elimu waambie…Kwanzawazazi wako wanafanya kitu gani, kwa niniwashindwe…Kwa nini walikupeleka shule yakulipia kama hawana uwezio, wanataka sifa?""Hapana wazazi wangu walikufa na ninasomashule ya serikali. Nimekosa mahitaji ya msingi nanauli ya kwendea shuleni. Nasoma shule yaKwiro, Morogoro. Shangazi ndiyeanayenisomesha,naye ana kansa hivi sasa hatakazi hafanyi…" Alianza kulia.Huruma fulani ilinijia na nilijiambia, kama ni naulitu na matumizi ni kwa nini nisiwe mwema,angalau kwa mara moja tu. "Baba na mamawamekufa lini?" Niliuliza nikijua kwambawatakuwa wamekufa kwa ukimwi, maana kipindikile ndipo fasheni ya ukimwi ilipoanza, ambapokila anayekufa alihesabiwa kwamba kafa kwaukimwi."Walikufa kwa ajali nilipokuwa mdogo sana,nilipokuwa na miaka mitatu. Ndiyo shangaziyangu alinichukua na kunilea hadi sasa anakufakwa kansa." Yule kijana alilia zaidi. Naombaniwaambie wasomaji kwamba, kuna nguvu fulanina sasa naamini kwamba, ziko nguvu nyingiambazo huwa zinaongoza maisha yetu bila sisikujua.Kitu Fulani kilinipiga akilini paa! Nilijikutanamuuliza yule kijana. "Kwa nini umeamua kujakwangu, ni nani alikuelekeza hapa na wazaziwako walikufa mwaka gani na wapi?" Yule kijanaalisema "nimeona nijaribu tu kwa mtu yeyoteambaye anaweza kunisaidia, ndiyo nimejikutanikiingia hapa, sijui…sikutumwana mtu. Wazaziwangu walikufa mwaka 1979 huko Same na mimiwanasema nilikuwa kwenye ajali, nikaokoka.Niliumia tu hapa," alishika kwenye kovu juu yapaji lake la uso.Nilihisi kitu fulani kikipanda tumboni na kujakifuani, halafu niliona kama vile nimebanwa nakushindwa kupumua. "Baba yako alikuwa anaitwanani?" "Alikuwa anaitwa Siame…Cosmas Siame…"Niliinuka ghafla hadi yule kijana alishtuka.Nilikwenda kwenye kabati langu mle ofisini nakuchakura kwenye droo moja na kutoka na diary.Mikono ikitetemeka, nilitoa kipande cha gazetikutoka ndani ya diary hiyo, nilichokuwanimekihifadhi."Ndiyo, alikuwa anaitwa Cosmas Siame. Huyu nimtoto wake, ni yule mtoto aliyenusurika."Nilinong'ona. Nilijikuta nikipiga magoti na kusali."Mungu wewe ni mweza na hakunakinachokushinda. Nimeamini baba kwamba, kilajema tunalofanya ni akiba yetu ya kesho nakesho hiyo huanzia hapa duniani." Halafunilinyamaza na kulia sana. Nililia kwa furaha naugunduzi wa nguvu zinazomgusa binadamu kwaanalofanya.Nilisimama nikiwa nimesawajika kabisa. Nilijihisikuwa mtu mwingne kabisa. Nilimfuata yule kijanana kumkumbatia huku bado nikiwa ninalia. "Mimini baba yako mdogo, ndiye nitakayekulea sasa.Ni zamu yangu sasa kukulea hadi mwisho." Nayealilia bila kujua sababu na alikuwaamechanganyikiwa kabisa. Nilirudi kwenye kiti nakumsimulia kilichotokea miaka 17 iliyopita.Tuliondoka hapo na kwenda kumwona shangaziyake Ubungo, eneo la Maziwa ambako alikuwaamepanga chumba. Kutokana na hali yakenilimhamishia kwangu, baada ya kumsimuliakilichotokea. Huyu dada yake Cosmas alifurahihadi akashindwa kuzungumza kwa saa nzima.Hata hivyo alifariki mwaka mmoja baadaye, lakiniakiwa ameridhika sana.Kijana Siame alisoma na kumaliza Chuo Kikuu nakwenda Australia kufanya kazi. Ukweli nikwamba, ni mwanangu kabisa sasa. Naaminihuko waliko Mbinguni wazazi wake wanafurahiakile walichokipanda miaka mingi sana nyuma.Lakini nami najiuliza bado, ilikuwaje Cosmasakanipa msaada ule? Halafu najiuliza, ni kitu ganikilimvuta mwanaye Siame hadi ofisini kwanguakizipita ofisi nyingine zote? Nataka nikuambie,usiwe mbishi sana bila sababu, kuna nguvu zaziada zinazoongoza matokeo maishani mwetu.***************************kama umeguswa jaribu kuishare na rafiki zakowaisome

No comments:

Post a Comment