Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Washiriki wa Mkutano Mkuu wa13 wa KAUKI

Washiriki wa Mkutano Mkuu wa13 wa KAUKI
Washiriki wa Mkutano Mkuu wa13 wa KAUKI

Wednesday, 9 January 2013

SHUKRANI KWA NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI

SHUKRANI KWA NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI KATIKA MSIBA WA MAREH. FLOMINA PANGALASI KIVENULE
Katibu Mkuu - KAUKI
Kwa niaba ya Uongozi wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) na wanaukoo kwa ujumla, naomba kutumia fursa hii kuwashukuru wote walishiriki kikamilifu katika kumwuguza na hatimaye kufanikisha mazishi ya Marehemu Flomina Pangalasi Kivenule, aliyefariki siku ya Ijumaa ya tarehe 28 Desemba 2012 katika Hospitali ya Ocean Road iliyopo Jijini Dar es Salaam. 
Uongozi unaamini kuwa jitihada kubwa zilizofanyika kwa pande zote katika kuhakikisha kuwa, mgonjwa anapata huduma kama inavyopaswa na pia kuhakikisha kuwa anafanyiwa mazishi yenye heshima baada ya kifo chake. 
Kuna changamoto mbalimbali zilizojitokeza katika msiba huu na pia ni funzo kwa wengine. Kama Mola anavyowaasa binadamu kuwa hawajui saa wala siku Bwana Mungu atakapokuita. Ni vyema tukandaa nafsi zetu katika matendo mema ya kumpendeza kila mmoja wetu. 
Mazishi yalifanyika vizuri huko Igula-Iringa kama ilivyopangwa (yaani Jumapili ya tarehe 30 Desemba 2012) na pia baada ya mazishi, wazazi wa marehemu walipeleka msiba kwao Ilula, Iringa ili pia jamii ambayo haikupata fursa ya kushiriki Dar es Salaam na Igula ipate nafasi ya kuwafariji wafiwa. 
KAUKI inawashukuru wanakikundi cha Umoja wa Watu wa Igula ambao walifanikisha upatikanaji wa huduma ya gari la kusafirisha mwili pamoja na sanduku la kuhifadhi mwili wa marehemu. 
KAUKI pia inawashukuru majirani wa Mbezi Inn nyumbani kwa marehemu kwa moyo wao mwema na wa ukarimu waliouonesha katika kuwahudumia wageni mbalimbali pamoja na wafiwa. Bila kuwasahau ndugu, jamaa na marafiki kwa uvumilivu wao hadi hatua ya mwisho ya kuuaga mwili kabla ya kusafirisha Iringa.
Kwetu hili ni somo kubwa na kuhaadi kuyachukua mazuri yote kwa faida ya kizazi kijacho.
Mwenyezi Mungu Awalinde, Amina. 
Imeandaliwa na:
 
Adam Kivenule
Katibu - KAUKI
 
Picha za Matukio Siku ya Msiba
Akina mama wakitoa heshima zao za mwisho mbele ya geneza lenye mwili wa Flomina Kivenule
Akina mama wakiendelea wakitoa heshima zao za mwisho mbele ya geneza lenye mwili wa Flomina Kivenule
Akina mama wakiendelea wakitoa heshima zao za mwisho mbele ya geneza lenye mwili wa Flomina Kivenule

LILIAN KIVENULE AAGWA

LILIAN IGNUS KIVENULE AAGWA NA FAMILIA YAKE


Usiku wa tarehe 02 ya mwezi Januari mwaka 2013, ulikuwa wa aina ya pekee kwa Familia ya Lilian Ignus Pangayena Kivenule, pale binti yao mpendwa Lilian alipoagwa na wazazi wake, pamoja na ndugu, jamaa na marafiki katika ukumbi wa Kanisa la Yesu Mfalme, lililopo Tabata, Jijini Dar es Salaam.

Lilian Ignus Pangayena Kivenule
Lilian Kivenule akikata keki katika moja ya sherehe zake kabla ya kuagwa siku ya tarehe 02 Januari 2013 katika Ukumbi wa Yesu Kristo Mfalme, Tabata Jijini Dar es Salaam

Ilikuwa ni siku ya furaha kwa familia yake ambayo imemlea hadi kufikia hatua hiyo muhimu ya kupata mwenzake wa kushirikiana katika shida na raha katika siku zao za maisha hapa duniani.




Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) unawatakia kila la kheri katika maisha yao mapya. Mwenyezi Mungu awazidishie pale panapopungua.

Kwa picha za matukio katika siku hiyo, angalia links hizi hapa kutoka facebook

http://www.facebook.com/photo.php?fbid=520831541294309&set=at.517995654911231.124811.100001024023552.100001498014794&type=1&theater

http://www.facebook.com/photo.php?fbid=454121264647803&set=a.205615882831677.48963.100001498014794&type=1&theater

Lilian Ignus Pangayena Kivenule
Lilian Kivenule akipongezwa na marafiki siku ya Kuagwa kwake katika ukumbi wa Yesu Kristo Mfalme


Lilian Ignus Pangayena Kivenule
Liliani Kivenule akimkaribisha mmewe mtarajiwa kwenda kupata chakula siku ya sherehe ya kuagwa kwake, katika ukumbi wa Kanisa la Yesu Kristo Mfalme, Tabata Jijini Dar es Salaam

Asante,




Imeandaliwa na:




Adam Kivenule

Katibu - KAUKI

Monday, 29 October 2012

Mikasa ya Soko Kuu la Mwanjelwa

Ni mwaka wa tatu sasa toka Soko la Mwanjelwa lianze kujengwa upya baada ya ajali ya moto iliyowapatia hasara kubwa wafanyabiashara wa Mbeya kwa kuunguliwa bidhaa na mazao mbalimbali ya biashara, yaliyokuwemo katika soko hilo.

Wengi wao walitarajiwa kuwa ujenzi wa soko ungeenda haraka kutokana na umuhimu na mahitaji makubwa ya soko hili kwa wakazi wa Mbeya, mikoa ya karibu na nchi jirani za Zambia na Malawi.

Hali imekuwa tofauti kwa sababu sasa ni mwaka wa tatu tangu ujenzi uanze huku shauku kubwa kwa wafanyabiashara ikilitaka liishe mapema na waingie kuendeleza biashara zao.

Mkoa wa Mbeya ni Jiji linalokua kwa kasi na matarajio wengi kuboreka kwa miundo mbinu na masoko ya biashara kama kichocheo cha uchumi.

Je, pamoja na jitihada mpya ya kulijenga soko hili, je litaweza kumudu majanga ya moto ambayo yamekuwa yakilikumba soko hilo mara kwa mara. Hili ndilo swali kubwa ambalo linapaswa kuulizwa na kila mmoja wetu mpenda maendeleo. Tusubili tuone mara baada ya kukamilika na kuanza kutumika.

Zifuatazo ni baadhi ya picha zilizopigwa kuonesha ujenzi wa Soko la Mwanjelwa ukiendelea....









The Wonder of Mount Kilimanjaro







































Mount Kilimanjaro

Resources Abundance Versus Poverty Paradox



Tanzania is a resource-rich country with abundant gold (2,222 tones of proven reserves), natural gas (33 trillion cubic feet of proven reserves), uranium (35.9 million pounds of proven reserves), coal (1.5 billion tones of proven reserves), diamond 50.9 million carat of proven reserves), to mention only a few extractive resources in the country. Tanzania had since 2009 implemented EITI during which the country has produced two reports; February 2011, and Jun 2012. The latter awaits EITI International Secretariat Review.









Wise Words



When something serious is going on silence is a lie, if you know the truth and you keep quiet you are a liar too. If you do not know your right you have no right. Tanzanians we do not need good infrastructure anymore we need justice first.