Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Wednesday 9 January 2013

SHUKRANI KWA NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI

SHUKRANI KWA NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI KATIKA MSIBA WA MAREH. FLOMINA PANGALASI KIVENULE
Katibu Mkuu - KAUKI
Kwa niaba ya Uongozi wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) na wanaukoo kwa ujumla, naomba kutumia fursa hii kuwashukuru wote walishiriki kikamilifu katika kumwuguza na hatimaye kufanikisha mazishi ya Marehemu Flomina Pangalasi Kivenule, aliyefariki siku ya Ijumaa ya tarehe 28 Desemba 2012 katika Hospitali ya Ocean Road iliyopo Jijini Dar es Salaam. 
Uongozi unaamini kuwa jitihada kubwa zilizofanyika kwa pande zote katika kuhakikisha kuwa, mgonjwa anapata huduma kama inavyopaswa na pia kuhakikisha kuwa anafanyiwa mazishi yenye heshima baada ya kifo chake. 
Kuna changamoto mbalimbali zilizojitokeza katika msiba huu na pia ni funzo kwa wengine. Kama Mola anavyowaasa binadamu kuwa hawajui saa wala siku Bwana Mungu atakapokuita. Ni vyema tukandaa nafsi zetu katika matendo mema ya kumpendeza kila mmoja wetu. 
Mazishi yalifanyika vizuri huko Igula-Iringa kama ilivyopangwa (yaani Jumapili ya tarehe 30 Desemba 2012) na pia baada ya mazishi, wazazi wa marehemu walipeleka msiba kwao Ilula, Iringa ili pia jamii ambayo haikupata fursa ya kushiriki Dar es Salaam na Igula ipate nafasi ya kuwafariji wafiwa. 
KAUKI inawashukuru wanakikundi cha Umoja wa Watu wa Igula ambao walifanikisha upatikanaji wa huduma ya gari la kusafirisha mwili pamoja na sanduku la kuhifadhi mwili wa marehemu. 
KAUKI pia inawashukuru majirani wa Mbezi Inn nyumbani kwa marehemu kwa moyo wao mwema na wa ukarimu waliouonesha katika kuwahudumia wageni mbalimbali pamoja na wafiwa. Bila kuwasahau ndugu, jamaa na marafiki kwa uvumilivu wao hadi hatua ya mwisho ya kuuaga mwili kabla ya kusafirisha Iringa.
Kwetu hili ni somo kubwa na kuhaadi kuyachukua mazuri yote kwa faida ya kizazi kijacho.
Mwenyezi Mungu Awalinde, Amina. 
Imeandaliwa na:
 
Adam Kivenule
Katibu - KAUKI
 
Picha za Matukio Siku ya Msiba
Akina mama wakitoa heshima zao za mwisho mbele ya geneza lenye mwili wa Flomina Kivenule
Akina mama wakiendelea wakitoa heshima zao za mwisho mbele ya geneza lenye mwili wa Flomina Kivenule
Akina mama wakiendelea wakitoa heshima zao za mwisho mbele ya geneza lenye mwili wa Flomina Kivenule

No comments:

Post a Comment