ADAM KIVENULE BLOG: For information call +255 713 270364 E-mail: kivenule@gmail.com Blog: https://adamkivenule.blogspot.com/ Twitter: https://www.twitter.com/kivenule Youtube: https://www.youtube.com/tagumtwa KIVENULE CLAN BLOGS: https://tagumtwa-kivenule.blogspot.com/ https://kauki-kauki.blogspot.com/ E-mail: KAUKI2006@gmail.com or tagumtwa@gmail.com
Thursday, 9 May 2013
Friday, 3 May 2013
GIDAGUMHINDI CECILIA SIGATAMBULE KIVENULE WA MAGUBIKE-IRINGA AFARIKI
TANZIA
Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) kwa masikitiko makubwa
unawatangazia Wana-KAUKI, ndugu, jamaa, marafiki na wanaukoo kwa ujumla, kifo cha
Bi. Gidagumhindi Cecilia Sigatambule Kivenule, kilichotokea tarehe usiku wa
kuamukia tarehe 18 Aprili 2013, huko Magubike, Iringa Vijijini, Mkoani Iringa.
Marehemu Gidagumhinda Kivenule alikuwa akiumwa kwa
muda mrefu na hasa akisumbuliwa na tatizo la upofu wa macho, homa, miguu na
uzee. Kabla ya mauti kumkuta, Marehemu alilazwa kwa muda wa wiki mbili katika
hospitali ya Ipamba, na hali yake kupata auheni lakini siku ya Jumatano tarehe
17 Aprili 2013 akiwa nyumbani hali ilibadilika na hatimaye kumpelekea mauti
kumfika usiku wa tarehe 18 Aprili 2013.
Bi Gidagumhindi ni Mtoto wa Kwanza kwa Bibi
Siwangumhavi Singaile, ambaye alikuwa Mke Mkubwa wa Sigatambule Tavimyenda Tagumtwa
Kivenule. Bibi Siwangumhavi alikuwa na watoto 7 ambapo mpaka sasa wamebaki
watoto 3 tu. Wengine waliomfuata Bi Gidagumhindi ni Semyamba Khadija Kivenule,
Sivinitu Alphonce Kivenule, Kadungu William Kivenule, Fibumo Xavery Kivenule,
Mlagile Anyesi Kivenule na John Kivenule.
Mazishi yake yalifanyika tarehe 18 Aprili 2013, eneo
la Magubike katika Makaburi ya Ukoo wa akina Nyangalima. Bi Gidagumhindi ataendelea
kukumbukwa kwa upendo, mshikamano na hamasa yake katika kuhakikisha kuwa KAUKI
inaendelea kuwa imara hususani katika eneo la Magubike.
Mwenyezi Mungu Ailaze Roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi,
Amina.
Imeandaliwa na:
Adam Alphonce Kivenule
Katibu Mkuu - KAUKI
Friday, 12 April 2013
Thursday, 11 April 2013
TANGAZO LA NAFASI ZA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI DARAJA ‘A’ NA STASHAHADA KWA MWAKA 2013/2014
|
TANGAZO LA NAFASI ZA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI DARAJA ‘A’ NA STASHAHADA KWA MWAKA WA MASOMO 2013/2014 Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi anatangaza nafasi za Mafunzo ya Ualimu ngazi yaCheti na Stashahada kwa mwaka wa masomo 2013/2014 | http://www.moe.go.tz/index.php?option=com_content&view=article&id=1670:tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-cheti-daraja-a-na-stashahada-kwa-mwaka-20132014&catid=1:latest-news |
TANGAZO LA UALIMU
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
Simu: 022-2110146/2110150/2211679, Faksi: 022-2113271
Tovuti: www.moe.go.tz
TANGAZO LA NAFASI ZA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI DARAJA
‘A’ NA
STASHAHADA KWA MWAKA WA MASOMO 2013/2014
Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
anatangaza nafasi za Mafunzo ya Ualimu ngazi yaCheti na Stashahada kwa mwaka wa
masomo 2013/2014 kama ifuatavyo:
A: MAFUNZO YA UALIMU TARAJALI NGAZI YA CHETI DARAJA
‘A’: MUDA MIAKA 2
UALIMU: KAWAIDA
- Mwombaji awe amehitimu Kidato cha IV kati ya mwaka
2008 na 2012 na kufaulu kwa kiwango
kisichopungua daraja la IV alama 27 katika Mtihani
uliofanyika katika kikao kimoja Au
-Awe na ufaulu kwa kiwango cha alama C katika masomo
manne tofauti katika Mtihani wa Kidato cha IV ulioyofanyika katika vikao zaidi
ya kimoja.
-Kipaumbele kitatolewa kwa waliofaulu masomo ya ‘Mathematics’,
‘Biology’, ‘Physics’, ‘Chemistry’, ‘English’
na Kiswahili;
-Mwombaji aliyehitimu Kidato cha VI kati ya mwaka 2008
na 2012 hiyo ni sifa ya nyongeza.
UALIMU: MICHEZO
- Mwombaji awe amehitimu Kidato cha IV kati ya mwaka
2008 na 2012 na kufaulu Kidato cha IV kwa kiwango kisichopungua daraja la IV alama
27 kwa Mtihani uliofanyika katika kikao kimoja.
-Kipaumbele kitatolewa kwa waliofaulu masomo ya ‘Mathematics’,
‘Biology’, ‘Physics’, ‘Chemistry’, ‘English’
na Kiswahili;
-Mwombaji aliyehitimu Kidato cha VI kati ya mwaka 2008
na 2012 na mwenye uzoefu katika kufundisha michezo (uthibitisho uambatishwe) ni
sifa ya nyongeza.
UALIMU: ELIMU YA AWALI
-Mwombaji awe amehitimu Kidato cha IV kati ya mwaka
2008 na 2012 na kufaulu Kidato cha IV kwa
kiwango kisichopungua daraja la IV alama 27 kwa
Mtihani uliofanyika katika kikao kimoja; na
-Mwombaji aliyehitimu Kidato cha VI kati ya mwaka 2008
na 2012 ni sifa ya nyongeza.
B: MAFUNZO YA UALIMU TARAJALI NGAZI YA STASHAHADA:- MUDA
MIAKA 2
UALIMU:- MASOMO YA SAYANSI, SAYANSI YA JAMII, BIASHARA
NA LUGHA.
- Mwombaji awe amehitimu Kidato cha VI kati ya mwaka
2008 na 2013 na kufaulu kwa kiwango
kisichopungua ‘Principal Pass’ moja na ‘Subsidiary’
moja.
- Awe mhitimu wa mafunzo mbalimbali katika ngazi ya NTA
level 5 kutoka katika chuo chochote
kinachotambuliwa na Serikali.
1.
Tanbihi: Masomo ya ‘Economics’, ‘Basic
Applied Mathematics’, ‘General Studies’, ‘Islamic
Knowledge’ na ‘Divinity’ hayatatumika
kama kigezo cha kumchagua au kumdahili mwombaji.
UALIMU: MICHEZO, MUZIKI, SANAA ZA UFUNDI NA SANAA ZA
MAONESHO.
- Mwombaji awe amehitimu Kidato cha VI kati ya mwaka
2008 na 2013 kwa kiwango kisichopungua
‘Principal Pass’ moja na ‘Subsidiary’ moja kwa kuzingatia masomo yafuatayo kwa kila kozi:-
Sanaa za Ufundi: masomo ya ‘Fine Art’ pamoja na
ufaulu wa Kidato cha IV masomo ya ‘Biology,
History,
Physics, English, na Civil Engineering’
Sanaa za Maonesho: masomo ya ‘Thearte Arts’ pamoja
na ufaulu wa Kidato cha IV masomo ya ‘Literature in English, Kiswahili, Geography na History;
Muziki: masomo ya ‘Music’ pamoja na ufaulu wa Kidato
cha IV masomo ya ‘English, Kiswahili,
Music, Physics, Geography na History’; na
Elimu kwa Michezo: masomo ya ‘Physical Education’
pamoja na ufaulu wa Kidato cha IV masomo
ya Biology, Chemistry, Physics, English’ na Kiswahili.
UALIMU: UFUNDI
- Mwombaji awe amehitimu mafunzo ya FTC kati ya mwaka
2008 na 2013 kutoka vyuo vya Ufundi
Au awe amehitimu mafunzo ya ufundi katika ngazi ya NTA
level 6 kutoka chuo chochote cha Ufundi
kinachotambulika na Serikali.
UALIMU: KILIMO
- Mwombaji awe amehitimu Kidato cha VI kati ya mwaka
2008 na 2013 kwa kiwango kisichopungua
“Principal Pass” moja na “Subsidiary” moja katika
somo la ‘Agricultural Science’ na ‘Biology’
Au ‘Chemistry’.
UALIMU: SAYANSI KIMU
- Mwombaji awe amehitimu Kidato cha VI kati ya mwaka
2008 na 2013 na kufaulu kwa kiwango
kisichopungua ‘Principal Pass’ moja na ‘Subsidiary’
moja katika masomo ya ‘Biology’,
‘Chemistry’ na ‘Nutrition’.
C: MAFUNZO YA
UALIMU KAZINI NGAZI YA STASHAHADA: MUDA MIAKA 2
UALIMU: MASOMO YA SAYANSI, SAYANSI YA JAMII, BIASHARA
NA LUGHA.
- Mwombaji awe mwalimu wa Daraja A aliyethitimu Kidato
cha VI na kufaulu kwa kiwango
kisichopungua “Principal Pass” moja na “Subsidiary”
moja; na awe na uzoefu wa kufanya kazi
kwa muda wa usiopungua miaka miwili
( 02) Tanbihi: Masomo ya ‘Economics’, ‘Basic
Applied Mathematics’, ‘General Studies’, ‘Islamic Knowledge’
na ‘Divinity’ hayatatumika kama kigezo cha kumchagua au
kumdahili mwombaji, na
UALIMU: ELIMU MAALUM
(i) Mwombaji awe mwalimu mwenye Stashahada ya Ualimu
fani ya Sayansi; Au Sayansi ya Jamii na
uzoefu kazini usiopungua miaka miwili
(02) ; na
(ii) Awe mwalimu wa Daraja A aliyethitimu Kidato cha
VI na kufaulu kwa kiwango kisichopungua
“Principal Pass” moja na “Subsidiary” moja; na awe na
uzoefu kazini usiopungua miaka miwili
(02)
Tanbihi: Masomo ya ‘Economics’, ‘Basic
Applied Mathematics’, ‘General Studies’, ‘Islamic
Knowledge’ na ‘Divinity’ hayatatumika
kama kigezo cha kumchagua au kumudahili mwombaji, na
Mwalimu anayefundisha watoto wenye mahitaji maalum [wasioona,
viziwi, wenye ulemavu wa akili n.k.
(vithibitisho viambatishwe)
], ni sifa ya nyongeza.
2
D: MAFUNZO YA UALIMU KAZINI NGAZI YA CHETI: MUDA MWAKA
1
UALIMU: SAYANSI KIMU
- Mwombaji awe mwalimu wa Daraja A na awe na uzoefu
kazini usiopungua miaka miwili
(02) .UALIMU: ELIMU MAALUM
- Mwombaji awe mwalimu wa Daraja A na awe na uzoefu
kazini usiopungua miaka miwili
(02)
- Awe amefaulu angalau somo moja la Sayansi katika
Mtihani wa Kidato cha IV.
Tanbihi: Mwalimu anayefundisha Elimu Maalum hata kama
hana mafunzo rasmi ni sifa ya nyongeza
(uthibitisho uambatishwe) .
A)
VIAMBATISHO
Waombaji wa mafunzo ya Ualimu watume barua za maombi
yao kwa njia ya posta. Barua hiyo iwe na
anuani sahihi ya mwombaji
(ya posta, au anuani ya barua pepe) , pamoja na viambatisho
vifuatavyo kulingana na aina ya mafunzo:
(i)Nakala za vyeti vya ufaulu Kidato cha IV ,VI na
ufundi;
(ii)Nakala za vyeti vya kuhitimu mafunzo ya ualimu
ngazi ya Cheti na Stashahada
(kwa waombaji walioajiriwa)
; na
(iii) Barua zilizopitishwa na waajiri
(kwa waombaji walioajiriwa)
.B)
MAELEZO MUHIMU
(i) Sifa zilizoelekezwa kwa mafunzo ya ualimu ngazi Cheti
Daraja ‘A’ni kwa ajili ya waombaji wa
mafunzo ya ualimu katika vyuo vya ualimu vya Serikali
na visivyo vya Serikali.
(ii)Wahitimu Kidato cha IV mwaka 2012 waliojaza nafasi
ya mafunzo ya ualimu ngazi Cheti Daraja ‘A’kwenye “Seforms” wakati wanamalizaelimu
ya sekondari wanatakiwa kuomba upya mafunzo hayo kwa njia ya barua na
watachaguliwa kwa kufuata vigezo vilivyowekwa.
(iii)Sifa zilizoelekezwa kwa mafunzo ya ualimu ngazi
ya Stashahada ni kwa ajili ya waombaji wote kwavyuo vya ualimu vya Serikali na
vyuo vya ualimu visivyo vya Serikali isipokuwa mwombaji kwa vyuovya ualimu
visivyo vya Serikali anaweza akawa amehitimu Kidato cha VI kati ya mwaka 2003
na 2013.
(iv)Waombaji wa mafunzo ya ualimu aliyeajiriwa
apitishe barua ya maombi kwa mwajiri wake.
(v)Majibu kwa watakaochaguliwa kujiunga na mafunzo ya
ualimu yatatolewa kwenye Tovuti ya Wizara yaElimu na Mafunzo ya Ufundi: www.moe.go.tz, na OWM-TAMISEMI: www.pmoralg.go.tz;
(vi)Waombaji watakaochaguliwa watatumiwa barua za
kujiunga na mafunzo na Wakuu wa Vyuo ambako
watakuwa wamepangwa kupitia anuani zao sahihi.
(vii)Tangazo hili lipo pia katika tovuti ya Wizara: www.moe.go.tz, OWM-TAMISEMI:
www.pmoralg.go.tz, kwenye ofisi za
Makatibu Tawala (M)
na vyuo vya
ualimu.
Tanbihi: Kwa waombaji walio Dar es Salaam wanaweza kufika Wizarani na kutumbukiza barua
za maombi
kwenye sanduku lililowekwa mapokezi. Tafadhali barua
zote za maombi zitumbukizwe kwenye sanduku la
maombi na si vinginevyo.
MWISHO WA KUPOKEA BARUA ZA MAOMBI NI TAREHE 10 Mei,
2013.
Maombi yatumwe kwa:
KATIBU MKUU,
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI,
S.L.P. 9121,
DAR ES SALAAM
(Aione: Mkurugenzi, Idara ya Elimu yaUalimu)
Thursday, 28 March 2013
OMBI LA TAARIFA ZA KABILA LA WAHEHE
Ndugu Mpendwa,
YAH: OMBI LA TAARIFA MBALIMBALI KUHUSU
HISTORIA YA KABILA LA WAHEHE NA WABENA
Rejea kichwa cha habari hapo juu.
Uongozi wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) kwa heshima na taadhima, unakuomba
usaidie kutupa taarifa mbalimbali za Historia ya Wahehe na Wabena ili tuweze
kuzitumia wakati wa Mkutano Mkuu wa Tisa wa KAUKI, utakaofanyika kwa siku
mbili, Kijijini Kidamali, Wilaya ya Iringa Vijijini, Mkoani Iringa; tarehe 29
hadi 30 Juni, 2013. Wakati wa mkutano, pia tutajadili hatua tulizofikia ili kuchapisha
kitabu cha Historia ya Wahehe ambacho kipo katika mchakato wa ukusanyaji
taarifa, na mada yake itawasilishwa katika mkutano huo na Mwalimu Israel
Mposiwa. Huu ni mfululizo wa mikutano ya KAUKI ambayo imekuwa ikifanyika maeneo
ya Kidamali mara 3, Irole mara 1, Nduli mara 1, Magubike mara 1, Igowole-Mufindi mara 1 na Dar es Salaam mara 1.
Uongozi wa KAUKI unaitambua kazi yako muhimu ya upashanaji habari na
thamani yake kwa jamii, na pia nafasi yako katika jamii na ushiriki katika
harakati mbalimbali za kupunguza umasikini na kuleta maendeleo kwa kuhabarisha
jamii ya Watanzania.
Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Tisa wa KAUKI yanafanyika katika kanda za
Irole, Nduli, Itagumtwa, Mgongo, Idete, Nyamihuu, Kalenga, Wasa, Nyamahana,
Ilala Simba, Nzihi, Dar es Salaam, Kidamali, Magubike, Mufindi na kwingineko
ambako wanaukoo wanatoka. Maandalizi yanajumuisha michango ya fedha, mazao na mifugo
kwa wale ambao hawana fedha, yote ikiwa ni kwa ajili ya kutoa huduma za
chakula, maji, uchapishaji wa matini na barua, kabla na siku ya mkutano; na
usafiri toka Iringa Mjini hadi Kidamali; na Kidamali hadi Magubike kwa wageni
na wenyeji.
Kutokana na uzito wa jukumu hili, uongozi wa KAUKI, pia umeamua kuandika
barua rasmi ya kukualika katika mkutano huo. Ratiba na ramani vimeambatanishwa
pamoja na barua hii kwa taarifa zaidi.
Mipango ya KAUKI inajikita katika kujiimarisha katika ngazi zote za
kiutendaji, kiuendeshaji na kuleta mabadiliko ya kiuchumi, kielimu, kisiasa,
kimaendeleo na kimapinduzi.
Toka mwaka 2005 Mikutano ya KAUKI ilipoanza kufanyika, kumekuwa na
mwamko wa hali ya juu kabisa na wanaukoo wengi kutoka maeneo ya Iringa Vijijini
na kwingineko wamekuwa wakihudhuria na kujifunza mambo muhimu ya kimaendeleo.
Kwa wastani washiriki 160 na 180 toka zaidi ya vijiji 20 Wilaya ya Iringa
Vijijini, wamekuwa wakihudhuria katika siku mbili za mkutano na kupata mafunzo
mbalimbali kutokana na mada ambazo zimekuwa zikifundishwa.
KAUKI ina malengo mengi, lakini baadhi ya
hayo ni pamoja na:
·
Kuchapisha kitabu cha Historia ya Wahehe toleo la Kwanza: Ndani
ya kitabu kutakuwa na sehemu zifuatazo: Historia ya Wahehe na Kuibuka kwa Tawala na Koo mbalimbali ndani ya
Uhehe (Wanitole, Wahabeshi, Wangazija); Harakati za Mapambano ya
Kikabila na Himaya mbalimbali (Vita za Luhota; Mkwawa na Wajerumani; Mkwawa na
Mnyigumba; Mkwawa na Wabena, Wasangu na Himaya Mbalimbali; Sehemu ya Pili: Historia ya Koo za Wahehe: Chimbuko na
Historia ya Ukoo wa Kivenule [Mtengelingoma
Balama na akina Tagumtwa Kivenule], Vita za Vatawangu na Ushujaa wa Tagumtwa
katika Vita; Sehemu ya Tatu: Umoja
wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI); Mipango na Harakati zake katika kuwakwamua Wanaukoo
katika lindi la umaskini, ujinga na maradhi, kutoka zaidi ya Vijiji 25 vya
Wilaya ya Iringa Vijijini;
·
KAUKI kuwa na ofisi yake
Kijijini Kidamali na pia sehemu nyingine za Kanda zake ili kurahisisha
mawasiliano na utekelezaji wa mipango yake;
·
Kuisajili KAUKI na kuwa na
mfuko wa kusaidia wanaukoo katika elimu, afya, uchumi na matatizo mengine. Pia
kuchukua jukumu la utunzaji na uendelezaji wa historia ya Wahehe pamoja na
sehemu mbalimbali za kumbukumbu za mashujaa katika Wilaya ya Iringa Vijijini. Tayari
mfuko umeanzishwa na wanaukoo wanaombwa kuuchangia;
·
KAUKI kuwa na sanduku la
posta na tovuti. Tovuti (blog) yetu ya muda inapatikana kupitia www.tagumwafoundation.wetpaint.com
·
KAUKI kufungua Akaunti
katika Benki. Akaunti tayari imefunguliwa na inajulikana kwa jina la: KAUKI,
Benki ya NMB, Akaunti Namba 6052301709, Tawi la
Mkwawa, Iringa Mjini;
·
KAUKI kuwa na vitendea kazi
mfano Kompyuta, Printa, Simu, Meza na Viti. Hii inatokana na kuongezeka kwa
kazi za KAUKI zinazohusisha kuandika na kuprinti sana. Kusudio la kuchapicha kitabu cha
historia ya Wahehe, kinahitaji vitendea kazi kama
kompyuta, printa, meza na viti;
·
KAUKI kuanza kutoa elimu
mbalimbali kwa wadau wake. Inatoa elimu katika mikutano yake. Elimu hiyo inalenga
kuifanya jamii kujitambua, uelewa katika masuala ya kiafya, umuhimu wa elimu,
ujasiliamali na kujengeana uwezo kwa kupeana uzoefu katika shughuli za
uzalishaji mali
ili kupunguza umaskini. Uzoefu unatolewa na wajumbe toka sehemu wanakotoka
hususani katika nyanja za uchumi, biashara, kilimo, elimu na uzalishaji mali;
·
KAUKI kubuni na kutekeleza
miradi ambayo itawasadia wanajamii. Kwa mfano Irole wamebuni na mradi wa kilimo
cha Alizeti na wanakusudia kuuanzisha. Taarifa zaidi zitatolewa kwenye mkutano
wa sita wa KAUKI. Jamii nzima tunapenda ijitambue na kutafuta namna ya
kukabiliana na hali ngumu ya kiuchumi kwa kuanzisha miradi midogo midogo ya
kiuchumi mfano kilimo cha mazao ya biashara na chakula; na
·
KAUKI kuwa na kitengo cha
utaalam, taaluma na ujuzi (teknolojia) ambacho kitafanya shughuli za kuwajengea
uwezo wana-KAUKI kupitia elimu, ushawishi, utetezi wa kisera na sheria mbovu;
kupunguza umaskini, magonjwa, ujinga na pia kuiletea fedha KAUKI kupitia
maandiko ya miradi (project proposal and appraisal), pamoja na miradi
mbalimbali ya ujasiamali. Suala hili lipo katika mchakato.
Baadhi ya kueleza hayo machache, napenda kutanguliza shukrani zangu
dhati, na natumaini utalikubali ombi letu.
Wako katika kazi,
Adam Kivenule
Katibu Mkuu - KAUKI
TANGAZO NA RATIBA YA MKUTANO MKUU WA 9 WA KAUKI
RATIBA
MKUTANO
MKUU WA TISA WA KAUKI
Siku ya Kwanza ya Mkutano Mkuu – Kidamali, Iringa: Tarehe 29 Juni 2013 |
||
|
Muda
|
Shughuli/Jukumu
|
Wahusika
|
|
12.00 – 12.45
|
Kuamka
na Kufanya Maandalizi ya Kuingia kwenye Mkutano
|
Washiriki Wote |
|
12.45 – 01.15
|
Kupata
Kifungua Kinywa
|
Washiriki
wote
|
|
01:15 – 02:00
|
Kuwasili
Mkutanoni na Kujisajili na kupata Vitambulisho
|
Washiriki
wote
|
|
02.00 – 02.20
|
Hotuba ya Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Tisa
wa KAUKI
|
Mwenyekiti wa KAUKI/Mwenyekiti wa Kamati ya
Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 9
|
|
02.20-02.45
|
Ufunguzi
Rasmi wa Mkutano na Mgeni Rasmi
|
Mgeni
Rasmi
|
|
02.45-03.15
|
Utambulisho
baina wa Ndugu na Wageni Waalikuwa
|
Wote
|
|
03.15 - 04.00
|
Mada I: KAUKI NI NINI? LENGO KUU, MALENGO MAHSUSI,
MUUNDO, JUKUMU LA KILA MWANA-KAUKI NA UENDESHAJI WAKE
Washiriki waijadili mada na
kutoa mapendekezo
|
Viongozi
wa KAUKI waongoze mjadala wa mada hii.
|
|
04.00 – 04:30
|
Mada II: CHIMBUKO, HISTORIA NA MUUNDO WA UKOO WA
KIVENULE
(a). Washiriki wasambaziwe nakala ya muundo wa Ukoo na kisha
kuujadili na kutoa mawazo yao
katika makundi
(b). Washiriki waijadili mada na
kutoa mapendekezo
|
|
|
04:30– 05:00
|
Pumziko la Chai / Kahawa/Maji |
Washiriki Wote |
|
05.00-05.45
|
Mada
Inaendelea.
(c).
Washiriki waijadili mada na kupendekeza nini kifanyike kutunza kumbukumbu
hizo
(d).
Washiriki wazijadili njia mbadala za kutunza taarifa zinazohusiana na ukoo
|
Wawezeshaji na Washiriki wote
|
|
04.45-05.05
|
Kuwasilisha majadiliano katika Makundi |
Washiriki wote na Wawezeshaji
|
|
05.05-05.30
|
Majumuisho ya yote yaliyojitokeza katika Mada
|
Wawezeshaji
|
|
05:30 – 06:30
|
TAARIFA YA UTENDAJI WA KAUKI
1. Mipango na Shughuli zilizokusudiwa kufanywa na
KAUKI 2012/2013;
2. Taarifa ya Utendaji kwa Ujumla;
3. Taarifa ya Mahesabu na Fedha; na Mafanikio na
Matatizo ya KAUKI
4. Matarajio ya KAUKI 2013/2014
|
Makamu
Katibu Mkuu
Mhasibu
|
|
06.30 – 07.00
|
TAARIFA YA SHUGHULI ZA
MAENDELEO KATIKA KANDA
1. Uhamasishaji
2. Mwitikio wa Jamii
inayounda Ukoo
3. Ushirikiano miongoni mwa wanajamii
4. Mafanikio na Matatizo
|
Viongozi wa Kanda zote
|
|
07.00-08.00
|
CHAKULA
CHA MCHANA
|
Washiriki
wote
|
|
8:00 – 8:45
|
KUSOMA RIPOTI YA MKUTANO MKUU WA SABA WA KAUKI
Kujadili Mapungufu, Kutoa Ushauri, Nyongeza
Kupitisha Ripoti
|
Katibu Msaidizi
Washiriki wote
|
|
08:45 – 09:15
|
Salaam
mbalimbali kutoka kwa Washiriki wa Mkutano Mkuu (Wastani watu 6 na dakika @
5)
|
Washiriki
wa Mkutano
|
|
09:15– 09:45
|
Pumziko la Chai/Kahawa/Maji |
Washiriki
wote
|
|
09.45 -11:00
|
Mada III: UZOEFU WA
WANAUKOO KATIKA SHUGHULI ZA MAENDELEO
1.Kidamali/Magubike: Kilimo cha Nyanya /Tumbaku na shughuli
nyingine za kiuchumi dakika 25
2. Irole/Nduli/Itagutwa/Mgongo:
Uzoefu wa Shughuli za Kiuchumi dakika 25
3. Dar/ Morogoro/ Kilombero / Moshi dakika
15
4. Kalenga, Ifunda, Ilala Simba, Wasa, Idodi na
Nyamihuu
|
Washiriki wote; viongozi wa Kanda au wajumbe
watakaochaguliwa kutoa uzoefu wa shughuli hizo za kiuchumi
|
|
11.00
|
KUAHIRISHA MKUTANO
|
Mwenyekiti wa KAUKI
|
|
2:30 – 6:30 Usiku
|
Burudani
(Muziki wa Kisasa na Ngoma za Asili), vinywaji, kufahamiana zaidi na
kubadilisha mawazo
|
Wanaukoo
wote
|
Siku ya Pili ya Mkutano Mkuu – Kidamali, Iringa: Tarehe 30 Juni 2013 |
||
|
Muda
|
Shughuli/Jukumu
|
Wahusika
|
|
12.00
– 12.45
|
Wageni
Wote Kuamka na Kufanya Maandalizi ya Kuingia kwenye Mkutano
|
Wote |
|
12.45
– 01.15
|
Kupata
Kifungua Kinywa
|
Washiriki
wote
|
|
01:15
– 02:00
|
Kuwasili
Mkutanoni na Kujisajili
|
Washiriki
wote
|
|
02.00-02.45
|
MADA
IV: CHANGAMOTO ZINAZOIKABILI KAUKI KUJILETEA MAENDELEO
1.
Nini kifanyike kwa wana-KAUKI kujiletea Maendeleo?
2.
Mnadhani ni vitu gani vipewe Kipaumbele kwa wanaukoo kunufaika na KAUKI!
3.
Baadhi ya Malengo ya KAUKI ambayo mnayafahamu mnadhani yatasaidia kuleta
mabadiliko? Na ni kwa namna gani? Jadili
4.
KAUKI ni sehemu tu ya vikundi vingi vinavyofanya jitihada za kujiinua
kiuchumi na kimaendeleo, mnadhani ni changamoto gani tunaipata ukilinganisha
na mafanikio au matatizo ambayo yamevipata vikundi vingine? Yajadili na
kuyatoa mapendekezo hayo
|
Wawezeshaji
na washiriki wote
Mwenyekiti
wa KAUKI
|
|
02.45-03.15
|
Majadiliano katika Makundi : Kila mshiriki ajidiliane na wana kundi kikamilifu na kutoa hoja za msingi za kujenga. Kila hoja ya msingi iwasilishwe ila kila mwanaukoo asikie. |
Washiriki wote wagawanyike katika makundi |
|
03.15-03.45
|
Makundi kuwasilisha hoja
kutoka katika makundi
|
Washiriki wote |
|
03.45-04.30
|
Majumuisho ya yote yaliyojitekeza katika Mada |
Wawezeshaji |
|
04:30
– 05:00
|
Pumziko la Chai / Kahawa/Maji |
Washiriki Wote |
|
05.00-06.00
|
1. Kuibuka kwa tawala mbalimbali ndani ya Uhehe
(Wanitole, Wahabeshi, Wangazija)
2.
Chimbuko la Koo mbalimbali mkoani Iringa
3.
Mahusiano yaliyopo baina ya koo zilizoibuka wakati
wa vita za kikabila na wageni
4.
Mgawanyiko wa Koo katika Mkoa wa Iringa
|
Washiriki
wote na Viongozi wa KAUKI
|
|
06.00-07.00
|
MAHITAJI YA KAUKI NA JINSI YA KUFANIKISHA
KUPATIKANA KWA MAHITAJI HAYO: Huu ni mjadala wa jumla na kila mjumbe wa mkutano anashiriki moja kwa
moja kutoa mawazo yake. Katibu na watendaji wengine wa KAUKI wana jukumu ya
kuyanakili maswali na majibu yote kwa ajili ya kufanyiwa kazi
|
Washiriki na Viongozi wa KAUKI
|
|
07.00-08.00
|
CHAKULA
CHA MCHANA
|
Washiriki
wote
|
|
08:00–08.20
|
MAJADILIANO YA HOJA MBALIMBALI AMBAZO
ZIMEWASIISHWA NA WASHIRIKI WA MKUTANONI
|
1.
Ndg. Adam Kivenule
|
|
08:20
- 8:40
|
1.
MAJUMUISHO NA TATHMINI YA
MKUTANO
2. MIPANGO NA MIKAKATI YA MBELENI
3. KUTANGAZWA KWA TAREHE YA MKUTANO MKUU WA TISA
|
VIONGOZI
WA KAUKI
|
|
8:40 -
9:00
|
UCHAGUZI WA VIONGOZI
WA KAUKI
|
Washiriki Wote
|
|
09.00-09:15
|
SHUKRANI NA KUFUNGA MKUTANO
|
UONGOZI MPYA WA KAUKI NA MGENI RASMI
|
|
09:15–09:30
|
Pumziko la Chai/Kahawa/Maji |
Washiriki
wote
|
|
09:30
|
ZIARA
YA KUTEMBELEA MAENEO MBALIMBALI KWA WAGENI WOTE. Maeneo ambayo yatatembelwa ni pamoja na:
Mlafu, nk
|
Washiriki
Wote
|
Subscribe to:
Posts (Atom)









