Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Friday 15 February 2013

GHARAMA YA DHULUMA NI HOFU



Spika yapaswa utende haki kwa kuzingatia sheria na kanuni za Bunge

Katika hali ya kuwa na hofu kutokana na yaliyojitokeza katika Bunge la hivi karibuni, Spika wa Bunge, Anne Makinda ameongezewa ulinzi pamoja na kubadilishiwa namba za gari analotumia kutokana na vitisho anavyovipata kutoka kwa wananchi ambao wamekuwa wakimtumia ujumbe wa simu.


 


Ni vyema ndugu Makinda akajiuliza hii hofu ya kuongezewa ulinzi inatokana nini, kwa sababu hali haikuwa hivi siku za nyuma. Kuna msemo wa kidini ambao unasema kuwa, "Gharama ya Dhambi ni Mauti". Lazima ndugu Makinda atambue kuwa anachowafanyia Wabunge wa upinzani Bungeni, pia anawafanyia wananchi waliowatuma wabunge hao. 

 


Kwa hiyo, kama wawakilishi wa wananchi hawa maskini wanakwazwa na mtu mmoja au wawili kuwasilishwa kilio cha wananchi walio wengi kwa sababu zisizo za msingi, na atambue kuwa anatenda dhambi ya dhuluma. Na mara nyingi dhuluma ya wengi ni msiba na pia ni hatari sana.


 


Kitendo cha Wabunge wa Upinzani kuamua kutoa namba za simu za Spika na Naibu wake kwa wananchi, ilikuwa ni kuwashtaki na wategemee kupokea simu au ujumbe ambao hautakuwa na lugha njema kwao kwa sababu wamedhulumiwa sehemu ya haki zao.


 


Tatizo la elimu na maji si geni kwa Watanzania walio wengi maskini. Maji yamekuwa yakitoka sehemu ambako wakubwa na watu wenye hadhi na uwezo wanakoishi. Sehemu ambazo wanaishi walalahoi ambao Mhe. Mnyika alikuwa anawasemea, hamna maboma na pengine hayapo kabisa. Kwa kifupi, matatizo ya elimu na maji yanawagusa moja kwa moja wananchi wa kawaida.


 


Kuendelea kuporoka kwa kiwango cha elimu ni kikwazo kikubwa kwa watanzania walio wengi kwa sababu kunawanyima fursa watoto wao kuendelea mbele kielimu na kuishia mitaani na kuharibikiwa. Endapo mfumo wa elimu ungekuwa ni mzuri, wananchi walio wengi maisha yao yangekuwa yameboreka kwa sababu kuongezeka kwa fursa kwa watoto waliosomo.


 


Watoto wa hao viongozi ambao wanapinga hoja za msingi za matatizo yanayowakabili wananchi, wanasomo nje ya nchi au kwenye shule zenye hadhi ya juu hapa Tanzania. Wao wana uwezo wa kulipa mamilioni ya pesa ili watoto wao wafanikiwe kielimu. Lakini kwa mtoto wa Maskini hali ni tofauti kwa sababu yeye anaendelea kusota kwenye shule za Kayumba ambazo hazina walimu, vifaa wala tija kwa maisha ya sasa ya kidijitali.


 


Kwa hiyo, ulinzi wa Spika upo kwa wananchi wenyewe na siyo polisi. Ni vyema Mhe. Makinda akaondoa tofauti na upendeleo ambao amekuwa akiuelekeza kwa upande wa serikali na kurudi kwa wananchi. Natumaini mahusiano mazuri baina ya makundi haya mawili yatarudi na kuwa kama zamani. Kumbuka siku zote kuwa, "Mshahara wa Dhambi ni Mauti".

No comments:

Post a Comment