Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Wednesday 13 February 2013

GHARAMA YA DHULUMA YA HAKI YA WANANCHI



Katika Bunge lililoisha hivi karibuni, Wabunge wa Upinzani kwa pamoja waliungana kuupinga mpango wa Spika na Naibu wake wa kuendelea kuzizima hoja zao na pia kuongoza Kiti bila kufuata Kanuni kama wao Wabunge wanavyohimizwa kufanya hivyo.

Hii ilitokea kutokana na Hoja Binafsi ya Mhe. James Mbatia Kuzimwa. Hoja hiyo ya Mhe. Mbatia ilihusu suala la Mitaala, ikiiomba serikali kuiwasilisha Bunge ili iwe kujadiliwa kutokana na kuendelea kuporomoka kwa elimu hapa nchini.

Hoja Binafsi ya Pili kuzimwa ilikuwa ni Mbunge wa CHADEMA wa Jimbo la Ubungo, Mhe. John Mnyika, ambayo ilihusu hali ya huduma ya maji katika Jiji la Dar es Salaam, hasa akingalia wastani mdogo wa watu wanaopata maji safi na Salama. Hoja yake hiyo ilibainisha baadhi ya mapungufu ni kutotekelezwa kwa ahadi ya maji kama zilizovyoainishwa kwenye Ilala ya Uchaguzi ya CCM mwaka 2005 na mwaka 2005. Hali ya tatizo la maji linaonesha kuwa katika wastani wa watu 2 mtu mmoja hapati maji safi na salama.

Pamoja na Spika huyo kushindwa kutoa majibu ya rufani mbalimbali zilizoelekezwa kwake mwaka 2011 - 2012, ili kubaini kama anaongoza Bunge kwa mujibu wa sheria au anaongozwa kwa matakwa yake.

Katika Mkutano wa Wabunge wa CHADEMA waliokuwa Bunge uliofanyika Temeke mwisho Jijini Dar es Salaam, Wabunge hao waliamua kutoa namba ya simu ili itumike kumwambia Spika na Naibu Wake Wajiuzulu kwa kushindwa kuwajibika kikamilifu katika kulisimamia Bunge. 

Wananchi wameitikia wito huo na sasa na licha ya baadhi ya watu kuanza kuwatetea kutokana na kuwa na maslahi binafsi juu ya maamuzi ya viongozi hao. 

Hapa chini ni utetezi wao.


Wanachama wa CCM Mkoa wa Iringa, wamelaani vikali kitendo cha baadhi ya wafuasi wa Chadema kutuma ujumbe mfupi wa simu za mkononi kumkashifu Makinda huku baadhi yao wakipendekeza chama hicho kifutwe kwa kukosa ustaarabu.

Katibu wa Baraza la Wazee wa CCM Wilaya ya Iringa, Said Mdota alisema kitendo alichofanyiwa Spika Makinda si cha kiungwana na hakikubaliki na wapenda amani wote. Mdota alipendekeza wahusika wote wasakwe na wachukuliwe hatua kali za kisheria.

Naye Mwenyekiti wa Jumuiya wa Wanawake Mkoa wa Iringa, UWT, Zainab Mwamwindi alisema jumuiya hiyo inatarajia kukutana kesho pamoja na agenda nyingine itajadili suala hilo na kulitolea tamko.

 “Sisi kama wanawake na Spika ni mwanamke, suala hili limetudhalilisha sana na katika hili tunalikemea kwa nguvu zote na Februari 14, tunatarajia kufanya kikao cha Kamati ya Utendaji tutalijadili na kulitolea tamko,” alisema.

No comments:

Post a Comment