Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Tuesday 18 September 2012

Maoni ya Wananchi

Maoni ya Wananchi
 
Nchimbi angekatwa shingo!!!
Kama mtanzania niliyeumizwa na mauaji ya makusudi aliyofanyiwa Mwangosi na Jeshi la Polisi, nimesikitishwa sana na uamuzi wa Nchimbi kwenda kuingilia kati Maandamano halali ya wanahabari pale Jangwani yaliolenga kuonyesha hisia zao na kulaani. Nchimbi hakualikwa kuwepo mahala hapo kwa wakati huo, baada ya kumuomba aondoke, nilimsikia kwa kauli yake anasema wao (kama Serikali) wanachochukia sana ni Mtu kufanya maandamano bila kibali, je yeye alipata wapi kibali cha kuingilia kati maandamano ya waandishi wa habari?
Waziri wa Mambo ya Ndani Emmanuel Nchimbi akisindikizwa na Polisi kutoka eneo la Viwanja vya Jangwani
Jeshi la Polisi lililo chini ya mamlaka ya Nchimbi limekuwa likijichukulia sheria mkononi ikiwemo kuhukumu vifo kama lilivyofanya kwa Mwangosi kwa watu wa aina ya Nchimbi ambao kwa maelezo yao linadai wanakuwa wanasabibisha fujo, je hizi sheria za kudhibiti fujo hazi-apply kwa Nchimbi? Kwa polisi walio makini nilitegemea Nchimbi angekamatwa mara moja na kuhojiwa kwa kosa la kuingilia maandamano halali ya waandishi wa habari na hivyo kuhatarisha amani.
Nijuavyo mimi kwa maandamano ya majonzi kama yale yakifanywa na watu wasio wastahimilivu iwapo atatokea mtu asiyealikwa na kuyaingilia kati anaweza akauawa, hiki ndicho kilichonilazimu niandike thread hii kuwapongeza wanahabari kwa kuwa na mioyo ya ustahimirivu.
Ninawapongeza sana Waandishi wa habari kwa kumuonyesha Nchimbi kwamba wao ni wakomavu kuliko yeye kwasababu waandishi wa habari wameingiliwa katika maandamano yao lakini hawakuchukua sheria mkononi kama wanavyofanya Polisi mbali na ukweli kwamba waandishi wa habari hawajapata mafunzo maalumu kama Jeshi la Polisi jinsi ya kumshughulikia mharifu.
Nawapongeza sana waandishi wa habari msingekuwa wakomavu na wastahimirivu jana Nchimbi angekatwa Shingo.
Ushauri wangu kwa Waandishi wa Habari. Nawaombeni mumsamehe bure Nchimbi huenda hajui alifanyalo.
Ushauri wangu kwa Polisi. Nawaombeni mumkamate Nchimbi na kumhoji ili muweze kujua alikuwa amekusudia nini kwenda mahala ambapo hajaalikwa? je alitaka waandishi wa habari wamfanyie fujo ili wapigwe risasi na baadhi ya Polisi wasiojua kazi yao hasa ni nini? ikiwezekana mumshitaki Nchimbi kwa kuingilia kati maandamano yasiyo muhusu ili iwe onyo kwa wananchi wengine wasio staarabika kwani kitendo alichofanya jana Nchimbi kikiendelea kuchukuliwa kama ni cha kawaida ipo siku amani yaweza kuvunjika. kwa mfano Waislam waweza kuwa na maandamano yao akatokea Mchungaji mbele yao kwa nia ya kuwapokea, hopefully wasipokuwa wastahimilivu amani yaweza kutoweka.
Ushauri wangu kwa Nchimbi. Nakuomba uwatake radhi waandishi wa habari kwa fujo ulizozifanya jana, pia uwatake radhi wananchi maana wengi wetu hatukutegemea kama ipo siku kiongozi kama wewe unaweza kukosa busara kiasi hicho kwa kwenda mahala bila mualiko kwasababu uzijuazo wewe mwenyewe.

No comments:

Post a Comment