Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Tuesday 18 September 2012

WAZIRI NCHIMBI HAKUVAMIA KWA BAHATI MBAYA MAANDAMANO YA WAANDISHI


WAZIRI NCHIMBI HAKUVAMIA KWA BAHATI MBAYA MAANDAMANO YA WAANDISHI WA HABARI LEO JANGWANI

Mwandishi wa Kujitegemea
 
Nawapongeza sana waandishi wa habari kwa kumtimua waziri wa mambo ya ndani Emmanuel Nchimbi nawapongeza sana kwa kuonyesha hisia zenu kwa kitendo kiovu kabisa ambacho kila mpenda demokrasia na haki katika ulimwengu huu ambacho amefanyiwa mbali ya kuwa mwandishi wa habari ni Mtanzania mwenzetu huyu marehemu Daudi Mwangosi.

Haina ubishi polisi ndio wameua kinachopiganiwa hapa wahusika wote ambao wako nyuma ya mauji haya washughulikiwe zaidi wale ambao wanatoa amri dhalimu kwa polisi,lakini nataka niwaambie waandishi wa habari Emanuel Nchimbi waziri wa mambo ya ndani, kuvamia maandamano yenu ya wanahabari na kutaka kuhutubia bila kualikwa sio bahati mbaya anajua mtaandika zaidi kuhusu yeye kutimuliwa kwake kwenye maandamano na kuacha kuandika maaovu na ujumbe mliokusudia kuupeleka kwa serikali na polisi wao,haingii akilini kwa mtu mwenye ngazi ya waziri kuvamia kwa mfano sherehe ambayo hana kadi ya mwaliko?

Kwa hiyo rai yangu kwa wanahabari ni kuandika kile ambacho mlikusudia kukiwakilisha leo kwa watanzania na dunia nzima !!Hawa ndio mawaziri wa tanzania huwezi kujua wakati gani yuko serious!!

Je mnakumbuka mjadala wa dowans ulivyopamba moto wakatuletea kikombe cha babu loliondo?? Na viongozi wote waserikali wakawa wa kwanza kupata kikombe na kusifia kikombe?? Kwa hiyo nchimbi asiwatoe kwenye lengo lenu. Kama hamfahamu vizuri Nchimbi ni zao la wanamtandao waliomweka Kikwete madarakani na ndio mwenyekiti aliyevuruga uvccm, na kama mnataka ukweli zaidi nendeni mkamhoji Sumaye Fredrick waziri mkuu mstaafu alikua anamaanisha nini alivyosema "anayefagia njia ya kwenda ikulu kwa karatasi basi akifika huko atatumia risasi ili aweze kutawala"mwaka 2005 kwenye kinyang'anyilo cha urais alipokuwa amechafuliwa sana na wanamtandao kwenye kampeni za kuwania urais kwa tiketi ya CCM.
kwa hiyo waandishi mshikamane mno kipindi hiki kwani serikali inajaribu kutumia kila aina ya hila kuwagawa na kuwatoa kwenye mjadala wa msingi kuwa waliomuua Daudi Mwangosi wachukuliwe hatua na wengine wawajibishwe kutokana na nyadhfa zao.

No comments:

Post a Comment