Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Friday 21 September 2012

M4C JIMBO LA UBUNGO


CHADEMA YAZINDUA MISINGI KATA YA MAKUBURI KAMA SEHEMU YAKE YA OPERESHENI YA M4C

Na mwandishi wetu,

Mheshimiwa John Mnyika, Jumamosi ya tarehe 15 mwezi Septemba 2012, alikuwa na kazi nzito ya kufungua misingi katika Jimbo la Ubungo, hususani katika kata ya Makuburi. Akihitimisha ziara yake ya ufunguzi wa misingi, pamoja na kuhutubia mikutano mbalimbali ya hadhara, huku akijibu hoja mbalimbali zilizowasilishwa na wananchi. 

Mheshimiwa Mnyika aliwaeleza wakazi wa Jimbo la Ubungo kuhusiana na shughuli ambazo wamezifanya toka walipochaguliwa. Akiongozana na Madiwani wa Kata ya Ubungo na Kata ya Makuburi, alitoa fursa kwa wananchi kuuliza maswali mbalimbali ambayo baadaye aliyajibu kikamilifu.  

Mojawapo ya maswali yaliyoulizwa ni pamoja na tatizo la matapeli ambao wapo eneo la daraja la Ubungo, kwenye mitambo ya TANESCO, na jinsi polisi wa wa kituo cha Kata cha Ubungo RiverSide wanavyofumbia macho uhalifu huo na kuwakumbatia wahalifu, na namna watu wanavyotapeliwa na mateli hao.  

Akijibu hoji hiyo, Mhe. Mnyika aliwapa jukumu Madawani kulifuatilia kwa karibu suala hilo na kisha kumfahamisha hatua ambazo zimekwisha chukulia. Akiongezea, alisema, yeye kama Mbunge, anapambana na mtu kama Mkuu wa Jeshi la Polisi, Polisi wa Operesheni Mbalimbali na si polisi wa kituo cha polisi cha Kata.  

Kuhusu ujenzi wa daraja na barabara ya Mabibo External na Ubungo Maziwa, alisema, tayari mipango yote kuhusiana na kuanza ujenzi huo imekwisha kamilika. Kinachosubiliwa ni kuona kama kutakuwa na fungu la kuwalipa fidia watu waliofuatwa na barabara.  

Mwishoni mwa mkutano huo uliofanyika eneo la Riverside kwenye Kijiwe cha Taksi, Mhe. Mbunge alihitimisha ziara yake kwa kufungua msingi na kupandisha Bendera Mbili.

 

 

 

 

No comments:

Post a Comment