Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Friday 21 September 2012

WIKI YA NENDA KWA USALAMA HAINA TIJA


WIKI YA NENDA KWA USALAMA HAINA TIJA KATIKA KUPUNGUZA AJALI NA KUONGEZA WELEDI NA UMAHIRI KATIKA KUTUMIA NA KUHUDUMIA WATUMIAJI WA VYOMBO VYA USAFIRI 

Imekuwa ni kasumba kwa Jeshi la Polisi hususani kitengo cha Usalama Barabarani kuonekana wakiwa barabarani wakiwadhibiti madereva kuhusu zoezi la ukaguzi wa magari na leseni za udereva. Na kwa bahati mbaya ukaguzi wa magari umekuwa ukiegemea zaidi kwenye magari ya abiria na kuacha magari mengine watu binafsi yakiendelea kutembea mitaani.  
Kamanda mkuu kikosi cha usalama barabarani Mohamedi Mpinga akionyesha (waandishi wa habari hawapo pichani) jinsi ya kufungua na kubandika stika maaalum kwaajili ya kampeni ya kudhibiti Usalama barabarani mara baada ya kukabidhiwa stika hizo na wadhamini wao kampuni ya simu za mkononi Airtel na Puma, wanashudia pichani toka kulia ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa airtel Bi Beatrice Singano na Mkurugenzi wa kampuni ya Mafuta Puma bw, Maregesi Manyama, na kushoto ni Naibu waziri wa Mambo ya Ndani Mh, Pereira Ame Silima, wiki ya Nenda kwa usalama mwaka huu kitaifa itafanyika mkoani iringa ikiwa imebeba ujumbe usemao “ Pambana na ajiali za barabarani kwa vitendo, zingatia sheria
Ukaguzi wa vyombo vya usafiri kama magari ni muhimu kwa sababu kuna wamiliki wengine hujisahau na hivyo kushindwa kuchukua hatua za makusudi kuangalia na kuhudumia magari yao. Lakini pia katika ajali za barabarani magari yote huusika, yawe na binafsi au ya usafiri na kwa maana hiyo, sheria lazima izingatiwe sawe kwa vyombo vyote vya usafiri. 

Lakini kwa nini serikali haiweki nguvu yake katika kushughulikia kwa mapana yake Wiki ya Nenda kwa Usalama Tanzania? Ni dhahiri, viongozi hawana mwito au nia ya dhati katika kuhakikisha kuwa roho za watanzania zinalindwa kutokana na wimbi kubwa la ajali za barabarani. Mara nyingi najiuliza ni kwa nini hakuna bajeti maalum kwa ajili ya kutoa elimu kwa watumiaji wote wa barabara na waendesha vyombo vya usafiri na watumiaji wake. Sijawahi kusikia kutengwa kwa bajeti au fungu fulani kwa ajili ya kutoa elimu ya msingi/mahususi kwa watumiaji wa magari, abiria na pia watumia barabara zetu. 

Makampuni baki kwa maslahi yao, ndiyo yameonekana kujitokeza kutoa fedha kiasi na nguo au baadhi ya vifaa kiduchu ambavyo vinatumika wakati wa wiki hiyo moja tu ya nenda kwa usalama. Hii ni kijeli na dharau kwa Watanzania ambao wengi wao wanaendelea kuumia kutokana na lindi kubwa la ajili za barabarani zinazoendelea kutokea kila siku. 

Binafsi naamini kabisa, kama serikali kupitia jeshi la polisi, kitengo cha usalama barabarani wangeelekeza nguvu zake katika kutoa elimu badala ya kujipanga barabarani kula rushwa, ajili nyingi zinazoendelea kutokea, zingekoma kabisa. Madereva na watumia barabara wangepata umahiri katika bahari hii ya usalama barabarani. Elimu pekee ndiyo njia mahsusi ya kujikwamua na taifa hili na vifo na majanga ya ajali. 

Pia, kuendelea kushamiri kwa matatu katika barabara zote za Tanzania ni chanzo kikuu cha ajali. Na hii ni ishara ya kushindwa kwa jeshi la polisi na mamlaka nyingine husika katika kusimamia matumizi bora ya barabara na watumiaji wake. Matuta barabarani yanaendelea kudidimiza uchumi wa Tanzania kutokana na wananchi kulipa fedha nyingi za kigeni kuagiza spea/vipuri vya magari yao. Mtikisiko mkubwa ambao unalipata gari dogo, gari kubwa la mizigo na basi la abiria katika umbali wa kilometa 1000, ni ishara kwamba, katika kipindi cha mwaka mmoja, gari litakuwa limepunguza zaidi ya miaka miwili ya muda wake wa kufanya kazi kwa ufanisi.  

Matuta barabarani si suluhi ya matatizo ya ajali yanayoendelea kutokea katika nchi ya Tanzania. Serikali, polisi na mamlaka nyingine husika, zimeshindwa kabisa kutafuta suluhi ya kuboresha usalama barabara na kuishia kuweka matuta. Hapa ndipo akili za wadau wa usafiri zilipoishia. Hii ni aibu kwa taifa hili, hususani kwa wageni mbalimbali wanaondelea kumiminika Tanzania.

Ukitembelea nchi za wenzetu kuna mambo mengi ya kujifunza, mfano alama za barabarani huweka kwa kutumia mabanga makubwa ambayo hayahitaji mtu kuvaa miyani kuyaona. Na pia huwekwa kila baada ya umbali wa kilometa 1 au 2 huku humu katikati kukiwa na punguza la umbali wa mita mia 200 hadi mia 300 kabla ya tukio halisi ambalo lilikuwa limelengwa. Mfano kupinda kushoto kwenda mji mwingine, ambapo aina ya barabara na idadi ya barabara huashiriwa katika mapango hayo elekezi ya usalafiri.

Tofauti na hapa kwetu, kibao cha kuonesha kuwa unapaswa kutembelea kilometa 50 kwa saa huonekana ghafla tena kwa maandishi madogo sana. Na pengine, unamkuta askari wa tochi amekaa hapo hapo na kusema, umeovaspidi. Hii ni fedheha na ni aibu kwa taifa letu.

Naamini viongozi na watendaji mbalimbali ambao ni wadau wa usafiri na usalama barabarani wanatembea mara kwa mara katika nchi za wenzetu kwa nini hawaji na somo jipya.

Kauli mbinu na fulani hazina tija kwa taifa letu katika tasnia ya usalama barabarani kama kutakuwa hakuna sera na msingi mahsusi katika utoaji elimu na pia kuwaelimisha watumiaji wa barabara, vyombo vya usafiri na vyombo vyenyewe.

No comments:

Post a Comment