Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Wednesday 21 August 2013

RIPOTI YA MKUTANO MKUU WA TATU WA UKOO WA KIVENULE-KAUKI, 2007...

 

 

 

 

RIPOTI

YA

MKUTANO MKUU WA TATU WA

 KAUKI

(2007)

 

 

 

 

 

 

 

 

DIBAJI

M

kutano Mkuu wa Tatu wa UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI), ni mwendelezo wa mikutano, ambayo imekuwa ikifanyika Kijijini, Kidamali, toka mwaka Desemba 17-18, 2005, huku ikiwajumuisha wanajamii wanaunda ukoo Kivenule na pia jamii nyingine zilizo karibu na jamii hii. Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI, nao ulikuwa na majukumu yake muhimu na hususani utekelezaji wa mipango mbalimbali iliyopangwa kufanyika toka upolifanyika Mkutano Mkuu wa Pili wa KAUKI. Hadi wakati huo mkutano mkuu wa tatu wa KAUKI unapofanyika, tayari taswira na mwelekeo wa umoja huu ulikuwa umeshajidhihirisha wazi, hivyo kilichosubiriwa ni kuendelea kuhamasisha jamii hii kuyafanikisha yale ambayo yamekusudiwa kufikiwa kwenye dira yake.

 

Tayari Katiba ya KAUKI imeshasambazwa kwa wadau wake na kuendelea kutumika. Kila shughuli inayofanyika baada ya Mkutano Mkuu wa Pili wa KAUKI ni rasmi kwa sababu inafanyika chini ya usimamizi na msingi wa Katiba Mama ya KAUKI. Malengo makuu ya KAUKI yamebaki pale pale, ikiwa ni kujaribu kwa kila hali kwa kutumia ujuzi na maarifa, kuinua uwezo wa kielimu, kiuchumi, kijamii na kimaisha, kwa wanajamii wanaunda umoja huo, kwa kutumia rasimali mbalimbali zinazopatika katika nchi ya Tanzania na hususani katika maeneo wanayoishi; ikiwa ni pamoja kuihamasisha jamii hii kufanya kazi kwa juhudi na maarifa ili kupunguza umaskini unaowakabili.

 

KAUKI ipo ili kujitahidi kukidhi shida na mahitaji ya jamii iliyounda umoja huu na hususani katika maeneo lengwa ya elimu, afya, uchumi na jamii, kwa kushirikisha mawazo, fikra, ujuzi na maarifa ya kila mwanaukoo, katika mikutano mikuu na mikutano midogo midogo, ambayo inaandaliwa na wanaukoo wenyewe. Kwa kukutana pamoja, fikra za kujenga, ujuzi, uzoefu, kujengewa uwezo na maarifa, huunganishwa pamoja na kisha kupanga mikakati mbadala ya kuweza kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika maisha.

 

Ripoti ya Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI, inatathmini yale yote ambayo tayari yamekwisha fanyika toka mwaka 2005, pale mkutano mkuu wa kwanza ulipofanyika. Kwa mapana yake ripoti hii inajaribu kuyafafanua na kuyatolea maelezo yale yote yaliyojitokeza katika mkutano mkuu wa tatu, na hususani, suala la mwelekeo wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule baada ya kuwa na Katiba yake. Ripoti hii, inabainisha uwazi na uangavu uliopo katika Katiba ya KAUKI. Kipaumbele kilichopo hapa ni namna gani jamii hii inapaswa kushirikishwa katika shughuli mbalimbali za maendeleo na pia zile ambazo zitaujenga umoja huu na pia suala nzima la uchangiaji wa michango ambayo ni sehemu ya ajenda muhimu katika kila mkutano mkuu unapofanyika.

 

Ripoti hii ya KAUKI inabeba ujumbe mahususi kwa wasomaji wote hususani wanaukoo. Ni wa wajibu wa KAUKI kuhakikisha kuwa Ripoti hii inasambazwa na kuwafikia walengwa. Bila kuwafikia walenge basi ujumbe uliomo ndani utashindwa kuwafikia walengwa na hivyo faida ya kuandaliwa kwa taarifa hizi haitaonekana/dhihirika. Pia KAUKI inafurahi zaidi pale jamii nyingine zinapopata nakala hii kwa sababu inapata fursa ya kukosolewa pale iliposhindwa kufanya vizuri ni vile vile inasaidia kusambaza taarifa za aina hii kwa watu wengine ili nao wapata hamasa na ari ya kuunda umoja kama huu. Ndiyo maana tunasisitiza kuwa ripoti hizi ni vyema zikayajumuisha matukio yote muhimu yanayojitokeza katika siku mbili za mikutano hii. Mkutano Mkuu wa tatu wa KAUKI ulihudhuriwa na washiriki wapatao 108. Watu wazima wakiwa 88 na watoto 20. Kwa tathmini ya haraka, haya siyo mahudhurio mazuri sana ukilinganisha na idadi kubwa katika mikutano miwili iliyotangulia. Sababu za kupungua kwa mahudhurio zinaeleweka na ndiyo maana tumesisitiza kuwepo na mikakati mbadala kwa mikutano ijayo hususani ule ambao utafanyika eneo la Ilole ili idadi ya washiriki iweze kuongezeka.

 

Mwisho ya yote, shukrani ziwaendee ndugu wote waliojitoa kwa hali na mali hadi kufanikisha kuandaa Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI pamoja na jitihada dhahiri zilizotumika kuiandaa na kuikamilisha ripoti ya Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI.

 

 

 

 

Faustino Kivenule                                                                   Adam A. Kivenule

Mwenyekiti                                                                         Katibu Mkuu                      

 

 

 

 

 

UTANGULIZI

Mkutano Mkuu wa Tatu wa Ukoo wa Kivenule ni mojawapo ya Harakati za Maendeleo zinazofanywa na Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) katika kujikwamua na kuondokana na matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii hii. Mkutano huu ni sehemu wa mwendelezo wa Mikutano ya namna hii ambayo imekuwa ikifanywa mara moja kila mwaka. Kwa mara kwanza katika historia, Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule, ulifanyika, tarehe 17 – 18 Desemba 2005, katika Ukumbi wa Sanga, Kijijini Kidamali, mkoani Iringa.

 

Katika Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI), jumla ya ndugu/wanaukoo wapatao 129 toka sehemu mbalimbali mkoani Iringa na kwingineko hapa Tanzania waliohudhuria. Mkutano Mkuu wa Pili wa KAUKI ulihudhuriwa na jumla ya ndugu/wanaukoo wapatao 140. Baadhi ya ndugu/wanaukoo waliohudhuria mikutano hiyo walitoka sehemu za Kidamali, Nyamihuu, Ilala-Simba, Nyamahana, Magubike, Kipera, Nduli, Iringa Mjini, Morogoro, Mikumi, Dar es Salaam, Mufindi, Mbeya, Kilimanjaro, Tosamaganga, Mseke, Mwanga, Kalenga, Idodi, Mgongo, Ilole, Itagutwa, Kipera, Idete na Nzihi.

 

Umoja wa Ukoo wa Kivenule ulizinduliwa rasmi mwaka 2006, katika Mkutano Mkuu wa Pili wa Ukoo wa Kivenule uliofanyika tarehe 24 – 25 Juni 2006 katika Ukumbi wa Sanga Kijijini Kidamali, Iringa. Kuzinduliwa kwa Umoja wa Ukoo wa Kivenule, kulienda sambamba na uzinduzi wa Mfuko wa Ukoo pamoja na Kuipitisha Rasimu ya Katiba ya Umoja wa Ukoo wa Kivenule na hivyo kuwa Katiba Rasmi. Kuwepo kwa Katiba ya KAUKI kulitoa fursa ya kuanza kwa utekelezaji wa shughuli na mipango mbalimbali ya maendeleo. Pia, pamoja na mambo mengine, katika Mkutano Mkuu wa Pili wa Ukoo, kulifanya uchaguzi wa Viongozi wa Kanda, uchaguzi wa Walezi wa Ukoo na hivyo utendaji rasmi wa KAUKI kuruhusiwa kuanza.

 

Mkutano mkuu wa tatu wa KAUKI umezidi kupanua wigo, maono na mipango inayohusiana na maendeleo ya umoja huu. Mahudhurio ya washiriki katika mkutano pia nayo yamepanuka kutokana na kupata washiriki wapya wengi zaidi kutoka maeneo ya Ilole, Nduli, Mgongo na Mufindi.

Japo safari hii, mahudhurio ya wanaukoo nje ya mkoa wa Iringa hayakuwa ya kuridhisha katika ilivyofanyika katika MKutano Mkuu wa Pili wa KAUKI – 2006. Kwa mfano hapakuwepo na mwakilishi yeyote toka katika mkoa wa Kilimanjaro kama ilivyokuwa mwaka 2006. Mahudhurio toka mkoa wa Dar es Salaam yalikuwa nia madogo sana ilinganishwa na mwaka 2006.

 

Kwa wastani uwakilishi wa ndugu/wanaukoo waliohudhuria Mkutano Mkuu wa Tatu wa Ukoo wa Kivenule haukuwa wa mtawanyiko zaidi katika ilivyojidhihirisha katika mkutano mkuu wa pili wa KAUKI. Hii kwa Umoja wa Ukoo wa Kivenule ni changamoto kubwa ambayo inabidi ifanyiwe kazi.

 

Japo baadhi ya malengo ya umoja huu yalianza kujidhirisha katika mkutano mkuu wa pili wa KAUKI, hali ni tofauti kabisa katika mkutano mkuu wa tatu. Tofauti baina ya ndugu/wanaukoo zimeendelea kujidhihirisha. Hii imechangia pia mahudhurio kuwa duni hususani kwa wanaukoo toka eneo la Kidamali. Suala jingine ambalo limechangia mahudhurio duni ni uchangaji wa michango ya kufanikisha Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI. Kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Tatu toka Kidamali ilipitisha uamuzi wa kutowaalika ndugu/wanaukoo ambao hawakuonyesha nia ya kuchangia au kuchangia kabisa.

 

Kwa KAUKI haya siyo malengo yake, lakini kuna wakati inabidi kukubaliana na hali halisi ili kuweza kukamilisha baadhi ya shughuli ambazo zinakuwa zimepangwa kufanyika. Baada ya kufanya tathmini, uongozi wa KAUKI ulikubaliana na uamuzi wa Kamati ya Maandalizi ya Kidamali ya kuwazuia kuhudhuria mkutano mkuu wa tatu wa KAUKI wale ndugu/wanaukoo ambao hawakuchangia chochote ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

 

Kutokana na ufinyu wa bajeti na pia kukosa vyanzo vingine vya mapato, inabidi taratibu nyingine ambazo ni kinyume cha malengo ya KAUKI kuruhusiwa kutumika ili kunusuru baadhi ya shughuli zinazokusudiwa kufanyika. Japo KAUKI haikuridhishwa na uamuzi wa kuwazuia baadhi ya ndugu/wanaukoo ambao hawakuchanga michango kwa ajili ya maandalizi ya mkutano, haikuwa na namna nyingine ya kuweza kusaidia tatizo hilo kutokana na kukosa fedha toka katika mfuko wake.

 

Jambo la kufurahisha zaidi ni kupanuka kwa wigo wa mahudhurio na mwitikio katika mikutano hii; na pia kuanza kutolewa kwa fursa ya kufanya mikutano ya namna hii sehemu nyingine mfano Mkutano Mkuu wa Nne wa KAUKI utafanyika Ilole. KAUKI inaamini hii fursa nzuri ya jamii husika kutoka katika maeneo ambako mkutano unafanyika kuhamasishana wenyewe kwa wenyewe na hivyo kuongeza ari na moyo wa ushirikiano.

 

Viongozi wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule bado wanaamini kuwa hawajatimiza lengo lao la kuandaa mikutano ya namna hii kwa kiwango cha juu; kwani wanaamini kuwa bado kuna idadi kubwa ya ndugu/wanaukoo ambao bado hawajapata fursa ya kuhudhuria mikutano hii. Ndiyo maana, Umoja wa Ukoo wa Kivenule bado unahamasisha ndugu/wanaukoo wahamasishane kuhudhuria mikutano hii.

 

Vijiji ambavyo vimeonyesha mwelekeo mzuri na ambapo kwa Viongozi wa Ukoo ni mafanikio makubwa ni pamoja na Kidamali, Nyamihuu, Ilala-Simba, Nyamahana, Magubike, Idete na Nzihi. Pia, maeneo ya Nduli, Ilole na Mgongo, zimeonyesha mwelekeo mzuri na ndiyo maana Mkutano Mkuu wa Nne wa KAUKI unafanyika Ilole ikiwa ni mzunguko uliopangwa kuanza kutekelezwa baada ya mikutano mitatu (3) ya KAUKI kufanyika Kidamali. Umoja wa Ukoo wa Kivenule unadhani kuwa hii changamoto tosha kwa viongozi pamoja na ndugu/wanaukoo toka sehemu husika kudhihirisha ari yao na jinsi wanavyohamasika kuutumia umoja huu wa KAUKI kuunganisha ukoo na nguvu zao.

 

Kuendelea kufanyika kwa mikutano ya KAUKI ni sehemu ya mapambano na pia harakati endelevu za kukabiliana na mabadiliko ya kisera, kisiasa, kiuchumi, kijamii, kiutamaduni, kisayansi na teknolojia, na hususani utandawazi na soko huria ambayo yanapelekea jamii kubwa ya Watanzania kuwa tegemezi. Kwa kutambulia hilo, KAUKI inajaribu kutafuta mbadala/mwafaka wa changamoto hizi kwa kuunganisha nguvu ya wanajamii wanaounda KAUKI kushiriki kikamilifu katika masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo hasa suala la kupata elimu, kuwa na hali nzuri kiuchumi na kimaisha na kuyakubali mabadiliko ya dunia na hivyo kuchukua hatua mahsusi kuweza kukabiliana nayo.

 

UKIMWI, ufisadi, njaa, umaskini uliopindukia ni sehemu ya matatizo na changamoto kubwa zinayoikabili KAUKI. Mabadiliko ya hali ya hewa, uharibifu wa mazingira ni changamoto ambayo Ukoo wa Kivenule unawajibu wa kukabiliana nayo. Athari na

madhara ya majanga hatarishi tayari yanaonekana katika jamii zetu na katika maisha yetu ya kila siku. Mfano ongezeko la watoto yatima, watoto wa mitaani wasio na walezi, kuongezeka kwa utegemezi kutokana na wajane kutokuwa na msaada baada ya kupoteza/kufiwa na ndugu/wanaume zao kutokana na maradhi ya UKIMWI bado ni tatizo kubwa.

 

Jamii hii tegemezi tunayoijenga na ambayo tunaishuhudia ikikua pole pole siku hadi siku, inatutegemea sisi ndugu/wanaukoo wa kila kitu. Kwa mfano jamii yetu ina wajibu wa kuhudumiwa chakula, malazi, mavazi, madawa, nyumba nzuri za kuishi na elimu. Je, jamii hii itaweza kukabiliana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia kama sisi kama wanajamii husika tutashindwa kukubali kuwajibika kwa kuwapa elimu na huduma zingine za msingi? Hii ni changamoto kubwa ambayo hatuna budi kuifanyia kazi, na kila ndugu/mwanaukoo kukubali kila jukumu ambalo atakuwa amepewa na jamii inayomzunguka.

 

Nasi kama jamii inayounda Ukoo wa Kivenule tuna wajibu wa kushirikiana na asasi za kijamii na kiserikali katika kuleta maendeleo. Wimbi la umaskini uliokithiri, janga la UKIMWI, ujinga na rushwa vimekuwa ni vikwazo vikubwa vya maendeleo na ambavyo vinazidi kudidimiza harakati mbalimbali za kuweza kujiinua na kujikwamua katika hali hiyo. Harakati hizi za kutafuta maendeleo zimegawanyika katika makundi mbalimbali ya kijamii hususani makundi ya wasomi, wakulima, wafugaji, wafanyabiashara, wanawake na wananchi wa kawaida.

 

Pia haja ya kufahamiana baina ya wanajamii na ndugu wanaounda ukoo, pamoja na kuujua Ukoo kwa ujumla ni sehemu ndogo tu ya changamoto japo ina madhara makubwa zaidi kama wanaukoo hawafahamu. Kuwa wengi ni sehemu ya raslimali. Kama tunahitaji maendeleo, tunahitaji watu, uongozi bora na siasa safi. Japo suala la fedha ni muhimu, lakini kama huna mipango thabiti, fedha inaweza isiwe muhimu kwani itapotea bure bila kufanya jambo la msingi.

 

Kuna baadhi ya majukumu muhimu bado hayajafanyiwa kazi. Mfano sensa haijafanyika ili kuweza kujua idadi ya ndugu/wanaukoo wanaounda KAUKI. Bila kujitambua sisi wenyewe hatuwezi kutekeleza mipango yetu kama wana-KAUKI. Sensa ni muhimu sana kwa kuandaa mipango yetu na pia kujiwekea malengo yetu kama wana-KAUKI.

Changamoto zitakazopatikana baada ya kuyagusia mambo haya ya msingi katika mikutano hii inayofanyika, pia inawapa fursa washiriki wa mikutano hiyo kujenga ajenda mpya za mikutano ijayo.

 

Mkutano mkuu wa kwanza wa KAUKI uliyaangalia kwa kina mahusiano duni baina ya wana ndugu, kukosekana kwa ushirikiano katika mambo mbalimbali ya kimaendeleo, hali duni ya kiuchumi na kijamii, matatizo ya kifamilia na kiukoo.

 

Mwelekeo na nafasi ya ukoo wa Kivenule katika suala nzima la Elimu hasa katika dunia hii ya Utandawazi (Globalization). Maendeleo ya sayansi na teknolojia ambapo yameifanya dunia kuwa kama kijiji kisicho na mipaka na kila mtu anaruhusiwa kuingia na kutoka; kuongezeka kwa viwanda vinavyotumia teknolojia ya hali ya juu; kuongezeka kwa teknolojia ya habari na mawasiliano (Internet); kupanuka na kujengeka kwa miji, pamoja na soko huria. Mambo yote haya ndiyo yanayoweza kuonyesha mustakabali na nafasi ya ukoo wa Kivenule kwa maisha ya baadaye. Bado inajidhihirisha kuwa ukoo wetu upo nyuma sana katika suala nzima la elimu, hii linajidhihirisha kutokana na kuwa na ndugu wachache sana ambao wameweza kupata elimu kwa kiwango kinachostahili. KAUKI inakabiliwa na changamoto za mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia yanayojitokeza kila kukicha na yanayoibadili dunia na hivyo kutulazimisha nasi katika ukoo wa Kivenule kubadilika. Matumizi ya teknolojia ya habari na mawasiliano katika simu za mikononi, Internet, kompyuta, redio na satelaiti ni changamoto kubwa katika Ukoo wa Kivenule.

 

Ajenda kuu katika Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI zilikuwa ni pamoja na:

§         Kuwasilishwa kwa mada: “CHIMBUKO NA HISTORIA YA UKOO”. Wawezeshaji wa mada hii walikuwa ni Ndugu William S. Kivenule toka Kidamali, Ndugu Augustino Kivenule toka Mgongo na Benard Kivenule toka Ilole;

§         Kusomwa kwa Ripoti ya Mkutano Mkuu wa Pili wa KAUKI – Katibu Msaidizi wa KAUKI;

§         Kusomwa kwa Taarifa ya Mipango na Maendeleo ya KAUKI – Katibu Mkuu wa KAUKI;

§         Kuwasilishwa kwa Taarifa za Mipango na Maendeleo kutoka katika Kanda – Viongozi wa Kanda;

§         Kuwasilishwa kwa mada: “CHANGAMOTO ZINAZOIKABILI KAUKI KATIKA KUJILETEA MAENDELEO”. Mwezeshaji alikuwa ni Mheshimiwa Diwani – Stephan Mhapa;

§         Kupeana uzoefu wa shughuli mbalimbali za Kiuchumi na Maendeleo kutoka katika maeneo mbalimbali wanakoishi ndugu/wanaukoo. Uzoefu mkubwa ulikuwa ni Kilimo cha Nyanya Magubike; na

§         Uchaguzi wa Viongozi wa Kamati Ndogo na Kamati ya Utendaji.

 

Kwa ujumla shughuli zote zilizopangwa kufanyika siku hiyo zilifanyika vizuri na hakukuwa na tatizo lolote. Msisitizo ulitolewa kwa masuala ambayo yalihitaji uangalizi wa karibu. Japo kuna baadhi ya majukumu ambayo bado hayajafanyika, hii imebaki kuwa ni changamoto kwa KAUKI. Kutofanyika kwa sensa bado hili ni tatizo na inabidi liendelea kushughulikiwa kwa umakini. Ukusanyaji wa taarifa za ukoo unaendelea kufanyika japo si kwa kiwango cha kuridhisha. Uangalizi wa mali unafanyika kikamilifu kama ilivyokwisha kukubaliwa katika mikutano iliyokwisha fanyika.   Viongozi wapo na wanaendelea na shughuli zao japo si kwa kiwango cha kuridhisha. Msukumo wa hali ya juu unahitajika sana kutoka kwa viongozi wa KAUKI na pia wana-KAUKI wenyewe.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

MAANDALIZI YA MKUTANO MKUU WA TATU WA KAUKI

Jukumu la kuandaa Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI ilizihusisha Kamati za Maandalizi kutoka Kidamali, Dar es Salaam, Magubike, Ilole na Nduli. Jukumu kubwa lilikuwa ni ukusanyaji wa michango ya kuweza kufanikisha kufanyika kwa mkutano huo. Michango ilitengwa kwa viwango tofauti kama ilivyokubalika wakati wa mkutano mkuu wa pili wa KAUKI.

 

Kwa upande Dar es Salaam, maandalizi hayakuwa mazuri sana kwa sababu hakuna sura mpya zilizojitokeza kusaidia kufanikisha Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI. Tatizo hili pia lilijitokeza katika eneo la Kidamali ambapo ilifikia hatua ya kuchukua uamuzi wa kutowaruhusu kuhudhuria mkutano wale wote ambao hawakutoa michango. Kweli hii ni hali ya kukatisha tamaa kwani haya siyo malengo ya KAUKI. Tatizo la Dar es Salaam ni sugu na tayari limekuwa likiripotiwa katika Mikutano Mikuu ya KAUKI.

 

Ni wajumbe wachache tu ndio ambao wamekuwa wakijitoa mara kwa mara katika kuhakikisha kuwa mikutano ya namna hii inafanikiwa. Ni vikao vichache tu ndivyo vilivyofanyika huku mahudhurio yake yakiwa ni madogo na siyo ya kuridhisha. Wapo ambao waliahidi kutoa michango ya kufanikisha kufanyika kwa mkutano mkuu lakini hadi mwisho hawakufanya hivyo.

 

Kwa upande wa Nduli, Mgongo na Ilole nao walishiriki kikamilifu katika kuhakikisha kuwa Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI unafanyika. Hata mahudhurio yao yalikuwa ni makubwa ulikilinganisha na umbali wa safari yao.

 

Uchangishaji wa michango ulifanyika kwa mfumo wa kadi. Kazi za kuombea michango ziliandaliwa na kusambazwa kwa kila mwanaukoo/ndugu. Huu ni utaratibu ambao KAUKI imekuwa ikiutumia katika kukusanya michango ya kufanikisha kufanyika kwa mikutano hiyo. Kutokana na makusanyo kuwa finyu yaliathiri atoaji wa huduma siku ya mkutano. Japo hapakuwa na tatizo lolote katika huduma ya chakula lakini kuna baadhi ya mambo ya msingi hayakufanyika kutokana na hilo.

 

Changomoto zinatufundisha kuwa wakati wa kuandaa mikutano hii ni vyema tukaweka muda mrefu wa maandilizi ili kuweza kukabiliana na matatizo ya hapa na pale; na pia kupata mbadala pindi tatizo linapokosa sululu. Tatizo kama la Kidamali la watu kutohudhuria mkutano kutokana na kushindwa kuchangia ni vyema likawa ni funzo kwa wengine. Hatutegemei hali kama hiyo kuendelea kutokea kwa sababu inachangia mgawanyiko katika KAUKI.

 

Siku ya tareh 29 Juni 2007, viongozi wa KAUKI walikutana pamoja Kijijini Kidamali ili kuweza kutathmini maendeleo ya maandalizi ya Mkutano Mkuu ambao ilibidi ufanyike siku ya 30 Juni na 01 Julai 2007. Kwa ujumla makusanya hayakuwa ya kuridhisha. Hii haikuzuia utaratibu mwingine kuendelea. Mfano uandaaji wa ratiba ulifanyika sambamba na kufanya marekebisho madogo madogo pale ilipobidi.

Lengo la kutathmini hatua za maandalizi ni kubaini matatizo yanayoikabili KAUKI katika kuandaa mikutano yake. Jumla ya kiasi cha shilingi 300,000/- kilikusanywa kwa ajili ya kufanikisha kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI.

 

Kamati ya Dar es Salaam ilijitahidi kufanya maandalizi ya moja kwa moja kwa kuandaa Ripoti ya Mkutano Mkuu wa Pili wa KAUKI na mabango. Maandalizi mengine yalihusisha vitambulisho kwa ajili ya washiriki wa Mkutano Mkuu wa Tatu wa Ukoo wa Kivenule. Lengo ilikuwa ni kuhakikisha kuwa kila mshiriki anakuwa na kitambulisho wakati Mkutano ukiendelea.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

MIALIKO KWA WANAUKOO PAMOJA NA WASHIRIKI WENGINE

Mialiko ya wanandugu pamoja na wanaukoo kwa ujumla, kuhudhuria MKutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI ilifanyika wazi kwa kila mtu bila upendeleo, kila mwanaukoo alipewa taarifa za kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Ukoo na kuombwa kuhudhuria. Aidha kamati zote za maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule, zilikubaliana kwamba, kila mwanandugu au mwanaukoo anapaswa kuhudhuria mkutano huo bila kukosa katika maeneo yote. Japo kwa maeneo ya Kidamali na Magubike, uongozi wa maeneo hayo ulikubalina kutowaalika wale wote ambao hawakuonesha nia ya kutoa au kutoa kabisa michango. Hivyo kuponi au kadi za mwaliko ziandaliwa na kugawiwa kwa waliochangia tu.

 

Mialiko ilifanyika kwa namna mbalimbali ikiwemo ile ya mdomo. Yaani kumwalika mwanaukoo au ndugu moja kwa moja kwa kumpa maelekezo kuhusiana na mahali unapofanyika mkutano mkuu, tarehe pamoja na muda. Familia yote, yaani baba, mama na watoto, wote walipaswa kuhudhuria mkutano mkuu huo.

 

Pia mialiko ilifanyika kwa kubandika matangazo ya kuutangaza Mkutano Mkuu wa Tatu wa Ukoo wa Kivenule sehemu mbalimbali Kijijini Kidamali pamoja na maeneo mengine ambako Kamati ziliamini ndugu na wanaukoo wanaishi kule.

 

Kila ndugu aliyefika na kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Tatu wa Ukoo wa Kivenule, alipewa kitambulisho cha kuweza kumtambulisha kwa ndugu wengine. Kitambulisho hicho kilionyesha namba ya kitambulisho, jina la ndugu, mahali anapoishi na simu au sanduku la posta. Kamati ziliepuka ile hali ya kuulizana maswali ya kuwa wewe unaitwa nani, unaishi wapi na simu yako iko wapi? Hii ilikuwa ni sababu ya msingi ya kutoa kitambulisho kwa kila mwanaukoo au ndugu.

 

 

UBANDIKAJI WA MATANGAZO

Kama ilivyo ada, shughuli ya uandaji na ubandikaji wa matangazo kwa ajili ya mkutano mkuu hufanywa na kamati za maandalizi kutoka katika eneo kunakofanyika mkutano huo. Japo viongozi wa kamati za maandalizi kutoka maeneo mengine nao huwajibika kuutangaza mkutano kwa namna ambayo wao wanaona inafaa. Kuutangaza mkutano ni jambo la muhimu sana kwani linawasaidia walengwa wa mkutano huo kujitokeza kwa wingi siku ya mkutano wenyewe.

 

Mkutano hutangazwa kwa namna mbalimbali zikiwemo zile za kubandika mabango ya matangazo yaliyochapishwa au kupigwa durufu; kutumia barua na kadi za mwaliko pamoja na mawasiliano ya simu na ana kwa ana. Mara nyingi mabango ya matangazo yamekuwa yakibandikwa katika eneo ambako mkutano unafanyika pamoja na maeneo mbalimbali ambayo  yanalizunguka eneo ambako mkutano mkuu unafanyika.

 

Katika maandalizi ya mkutano mkuu wa tatu wa KAUKI, ubandikaji wa matangazo ya kuutangaza mkutano huo yalifanyika sehemu mbalimbali Kijijini Kidamali pamoja na maeneo mengine ambako Kamati ziliamini ndugu na wanaukoo wanaishi kule mfano Magubike, Nzihi, Kinyamlewa, Idete na Nyamahana.

 

Sehemu nyingine kulikobandikwa matangazo ni pamoja na Ipogolo na maeneo mbalimbali ya mjini. Ubandikaji wa matangazo ya Mkutano Mkuu wa Ukoo, uliibua hisia za ushawishi na hivyo wanajamii wanaoshi maeneo husika kushawishika kuhudhuria Mkutano huo. Wapo majirani, marafiki na watu wasio wanaukoo waliokuwa na shauku kubwa ya kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Tatu wa Ukoo wa Kivenule kama ilivyojitokeza katika mikutano iliyopita yaani mkutano mkuu wa kwanza na pili wa umoja wa ukoo wa Kivenule.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

HOTUBA YA UFUNGUZI

Mkutano Mkuu wa Tatu wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) ni sehemu ya harakati za maendeleo zilizoanza toka mwezi Februari 05, 2005 zikiwa na jukumu la kuinua hali za maisha za wanaukoo wanaoishi katika maeneo mbalimbali hapa Tanzania. Harakati hizo ndizo zilizopelekea kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Kwanza, wa Pili na wa Tatu; Desemba 17 – 18, 2005; Juni 24 na 25, 2006 na Juni 30 na Julai 01, 2007.

 

Mkutano Mkuu wa Tatu wa Ukoo wa Kivenule ulifunguliwa na Mwenyekiti wa KAUKI Ndugu Faustino Kivenule. Awali ya yote, Mwenyekiti wa KAUKI ambaye pia alikuwa ni msimamizi wa Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Pili wa Ukoo, Ndugu Faustino Kivenule, aliwakaribisha ndugu, jamaa, mgeni rasmi, wageni waalikwa na wanaukoo kwa ujumla kwenye mkutano huo. Aliwashukuru kwa kuitikia wito na kufika Kijijini Kidamali kuhudhuria mkutano.

 

Kabla ya kusoma hotuba ya Ufunguzi wa Mkutano mkuu huo, Mwenyekiti wa Ukoo alimkaribisha Ndugu George Kivenule, kuuombea mkutano kwa sala. Baada ya Sala ya kuuombea mkutano, Mwenyekiti wa Ukoo, alitumia fursa hiyo kuisoma Hotuba ya Ufunguzi.

 

Alianza kwa kuwajulisha ndugu, wageni waalikuwa na wanaukoo kuwa, lengo la Mkutano Mkuu wa Tatu wa Ukoo wa Kivenule ni kuwaunganisha wanaukoo wote, wanaoishi sehemu mbalimbali hapa Tanzania, ili wafahamiane, waelimishane na kupeana ujuzi katika nyanja mbalimbali za maendeleo na pia kupeana uzoefu.

 

Pia, lengo jingine la Mkutano Mkuu wa Pili wa Ukoo wa Kivenule ilikuwa ni kutolewa na kufundishwa kwa Mada ya HISTORIA NA CHIMBUKO LA UKOO WA KIVENULE na CHANGAMOTO YA KAUKI KATIKA KUJILETEA MAENDELEO; ambayo kwa siku hiyo mada hizo ziliwasilishwa na Ndugu William (Kadungu) Sigatambule Kivenule kutoka upande wa maeneo ya Kidamali; Ndugu Augustino Kivenule wa Nduli na Benard Kivenule toka Ilole kwa Mada ya Kwanza; na mada ya pili iliwasilishwa na Mheshimiwa Stephan Mhapa, Diwani wa Kata ya Nzihi.

 

Mwenyekiti aliwaeleza washiriki wa mkutano kuwa Harakati hizi kwa mara ya kwanza zilifanyika Kijijini Kidamali kwa upande mmoja na kwa upande mwingine jijini Dar es Salaam mwaka 2005. Kamati za maandalizi ziliundwa toka pande zote na kujipa majukumu mbalimbali, likiwemo lile la kuwaalika na kuwashirikisha ndugu na wanaukoo katika suala zima la maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Ukoo katika vikao, na pia utoaji wa michango.

 

Katika harakati za maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Tatu wa Ukoo wa Kivenule, kamati zote zilizipata vikwazo mbalimbali likiwemo tatizo la mwitikio duni katika kulipokea wazo hili. Kwa ujumla, katika kuliuza suala/wazo hili la kuandaa na kuwa na Mkutano Mkuu wa Tatu wa Ukoo wa Kivenule, kamati ilibidi zitumiea nguvu na mbinu za ziada ili kuweza kufanikiwa.

 

Mahudhurio duni yanatoa changamoto kwa Kamati za Maandalizi ya Mkutano Mkuu, kuongeza juhudi/jitihada na kutafuta njia mbadala za kufikia lengo. Kwa upande wa Kijijini Kidamali, ushawishi unazaa matunda, kwa sababu ongezeko la wanaukoo na ndugu kuliunga mkono wazo la kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Tatu wa Ukoo linavuna washiriki wengi.

 

Kwa upande wa Dar es Salaam, suala la mahudhurio duni, liliendelea kuwa ni kikwazo kwa kipindi chote cha maandilizi ya Mkutano Mkuu wa Tatu wa Ukoo wa Kivenule. Kwa upande wa Nduli, Mgongo na Ilole, hali ni shwari kutokana kuonesha nia kuwa pamoja katika kuijenga KAUKI. Katika suala la utoaji wa michango, watu wamekuwa na ari na mwitikio wa hali ya juu hapa Kijijini Kidamali, na kwa kiwango kikubwa ndio waliosaidia kufanikisha kufanyika kwa Mikutano Mkuu ya Umoja wa Ukoo wa Kivenule.

 

Licha ya wanaukoo waishio Dar es Salaam kuchangia, lakini mchango wao umesaidia kidogo sana, kwa sababu kiwango kikubwa cha fedha pamoja na mahitaji mengine, yamepatikana Kijijini Kidamali.

 

Sehemu nyingine, nje ya Kidamali, utoaji wa michango hapo mwanzo ulikuwa wa wastani, lakini kadiri siku zilivyokuwa zinakaribia, ari na kasi mpya ilijitokeza na kuwa kubwa hasa toka sehemu za Magubike, Nyamihuu, Ilole, Mgongo na Nduli.

 

Majirani na watu wengine wasio wanaukoo wamejitolea kutoa michango katika kuusaidia Ukoo wa Kivenule, kufanikisha kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Tatu wa Ukoo wa Kivenule. Majirani na marafiki wanajitokeza kwa hali na mali katika kutoa fedha, vyombo na vifaa mbalimbali.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

VII. UTAMBULISHO

Kwa mujibu wa Ratiba ya Mkutano Mkuu wa Tatu wa Ukoo, Mwenyekiti wa Ukoo Ndugu Faustino Sigatambule Kivenule alitumia fursa hii kuwaalika ndugu/wanaukoo kujitambulisha. Utambulisho ulifanyika kwa kila ndugu/mwanaukoo kujitambulisha mwenyewe Jina lake na pia kutaja majina matatu au zaidi ya hapo akimjumuisha Baba, Mama, Bibi na Babu zake.

 

Utambulisho ulifanyika kwa rika zote, toka mtoto mdogo hadi mtu mzima wa makamo. Lengo la kujitambulisha ni kuwawezesha ndugu wengine walioshiriki mkutano mkuu kuwatambua na kuwafahamu ndugu zao wanaoishi maeneo mengine.

 

Pia utambulisho ulifanyika kwa kuandaliwa vitambulisho ambavyo kila mshiriki wa Mkutano Mkuu wa Tatu wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule, alipewa. Kitambulisho kiliandikwa jina la mshiriki wa mkutano kikitaja majina matatu yaani Jina Lake, jina la baba na jina la ukoo. Pia anuani nyingine nazo ziliandikwa kwenye kitambulisho ili kuwarahisishia ndugu wengine kuzitambua kirahisi anuani za ndugu zao wengine.

 

Sambamba na hilo pia uandikishaji (kujisajili) kwenye daftari kulifanyika ikiwa ni sehemu ya kutunza kumbukumbu za washiriki wa mkutano mkuu wa pili. Mahudhurio yote yameambatanishwa kwenye ripoti hii.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

TAARIFA YA UTENDAJI NA MAENDELEO YA KAUKI

KAUKI ni Umoja wa Ukoo wa Kivenule. Ni jina la Katiba ya Umoja huo, lililokubaliwa kutumika na wana-KAUKI katika Mkutano Mkuu wa Pili wa  Umoja wa Ukoo wa Kivenule, uliofanyika tarehe 24 na 25 Juni 2006, Kijijini Kidamali, Mkoani Iringa. Katiba ya KAUKI tayari ilishaanza kutumika mara tu baada ya Mkutano Mkuu wa Pili. Nakala kadhaa za KAUKI tayari zimesambazwa na zinaendelea kutumika. Katiba ya KAUKI ni mwongozo wa shughuli mbalimbali zinazofanyika ndani na ikibidi kama kuna umuhimu nje ya KAUKI ili kuuletea maendeleo umoja huu.

 

KAUKI ina viongozi wa ngazi mbalimbali waliochaguliwa katika Mkutano Mkuu wa Pili. Viongozi hao wanajulikana kama Viongozi wa Kanda. Kila Kanda ambayo ilikubalika kuwepo, wakati wa Mkutano Mkuu wa Pili wa KAUKI, ina viongozi siyo zaidi ya mmoja.

 

Viongozi hawa, wanawajibika kwa wanaukoo wanaotoka katika maeneo yale wanayoishi. Wajibu na majukumu ya viongozi wa KAUKI yamebainishwa katika Katiba. Wajibu wao ni kushirikiana miongoni mwao pamoja na Viongozi wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule katika kutekeleza masuala mbalimbali ya maendeleo yanayouhusu ukoo. Pia, ni wajibu wa viongozi hawa, kuwashauri Viongozi wa KAUKI katika masuala mbambali yanayoukabili ukoo wetu kwa mfano masuala ya ugonjwa, elimu, uchumi na maendeleo.

 

Viongozi wa Kanda wana nguvu ya Kikatiba katika kutimiza wajibu wao na pia wana wajibu wa kuhakikisha kuwa mipango mbalimbali inayopangwa kupitia Kamati Kuu au Mkutano Mkuu wa KAUKI inatekelezwa.

 

Viongozi wa ngazi nyingine za juu kama Katibu, Mwenyekiti, Makamu wa Katibu, Makamu wa Mwenyekiti, Mweka Hazina na Msaidizi wake, wana wajibu wa kuwahimiza viongozi wa Kanda, kushirikiana baina yao wenyewe na pia kushirikiana na viongozi wakuu kutekeleza wajibu na majukumu mbalimbali ambayo yanatukabili.

 

Kwa mujibu wa KAUKI, viongozi wa Kanda, wana wajibu kuhudhuria vikao mbalimbali kama inavyoainishwa kwenye Katiba ya KAUKI. Wajibu huo pia unawagusa viongozi wengine wa KAUKI na wanawajibika ipasavyo kutekeleza na kutimiza wajibu wao.

RIPOTI YA MKUTANO MKUU WA PILI WA KAUKI

Ripoti ya Mkutano Mkuu wa Pili ilishawasilishwa katika Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI. Ripoti hii iliyokuwa inaandaliwa na Katibu Mkuu wa KAUKI tayari ilikuwa imekwisha kamilika toka mwaka jana (2006); lakini kwa bahati mbaya na pia kwa sababu ya matatizo ya kiteknolojia, mashine (Kompyuta) iliyokuwa ikitumiwa kuandaa ripoti hiyo ya KAUKI ilipata hitilafu na hivyo taarifa zote zilizoandikwa kupotea. Hadi zinapotea taarifa hizo, ripoti ilikuwa na kurasa sabini na sita (76). Kwa hiyo, kazi ya kuandika ripoti hiyo ilibidi ianze kufanyika upya. Kwa bahati nzuri ripoti ilikamilika ndani ya muda uliopangwa na hivyo kuwasilishwa kwenye Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI.

 

MICHANGO YA MFUKO WA KAUKI

Kama inavyobainishwa katika Ibara ya 5.0 ya Katiba ya KAUKI na ilivyokubaliwa kwenye Mkutano Mkuu wa Pili wa KAUKI, kila mwanaukoo, anawajibika kulipa michango kama ilivyopangwa. Katiba ya KAUKI inafafanua kwa mapana kuhusiana na michango hiyo ya kila mwezi. Mojawapo ya matumizi ya michango hiyo ni kuwasaidia wanaukoo katika matatizo mbalimbali ya ugonjwa, masomo na pia kiuchumi pale utakapokuwa umejiimarisha. Pia michango hiyo inaweza kusaidia kugharamia gharama za kufanya mikutano ya KAUKI.

 

Viongozi wa Kanda, walipewa jukumu la kukusanya michango hiyo. Kwa mujibu wa makubaliano yaliyofikiwa katika Mkutano Mkuu wa Pili wa KAUKI, stakabadhi zikiwa na mhuri wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI), ilibidi zisambazwe kwa viongozi husika wa Kanda kwa ajili ya shughuli za ukusanyaji wa michango hiyo. ‘Taarifa kuhusiana na suala la michango, viongozi wa kadha watatoa taarifa zaidi’.

 

MAANDALIZI YA MKUTANO MKUU WA TATU WA KAUKI

Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI ilibidi yaanze mapema kabisa toka mwezi Januari mwaka 2007. Vikao mbalimbali ilibidi vifanyike ili kuweka mikakati mbalimbali ya kuweza kuiboresha Mikutano hiyo na hasa Mkutano Mkuu wa Tatu KAUKI utakaofanyika Juni mwaka huu 2007.

 

Katiba ya KAUKI, inaeleza wazi kuhusiana na wajibu wa kila mwanaukoo kuchangia maandalizi ya Mkutano Mkuu wa KAUKI (Ibara ya 5:3(ii). Viwango mbalimbali vilishawekwa na kuainishwa kwenye Katiba ya KAUKI na kila mwana ukoo alishepewa taarifa kuhusiana na viwango hivyo katika Mkutano Mkuu wa Pili wa KAUKI. Katika michango ya kuandaa Mkutano Mkuu, wana-KAUKI wanaweza kutoa fedha taslimu, mifungo au mazao kulingana na thamani ya pesa kwa kipindi kile.

 

Viwango vinavyopangwa kutolewa ili kufanikisha mkutano mkuu, havina mipaka. Mwanaukoo yupo huru kutoa zaidi. Mara nyingi katika utoaji wa michango kwa ajili ya maandalizi ya Mikutano Mikuu, kadi huandaliwa na kusambazwa kwa wana ndugu mbalimbali na pia kwa jamaa na marafiki zetu. Jambo hili ni nzuri kwa sababu linaonyesha heshima kwa yule unayemwomba atoe mchango wako. Kwa sababu hiyo, kadi maalum ziliandaliwa na kila mwana-ukoo ilibidi akabidhiwe kadi ya kuomba mchango.

 

Pia, viongozi wa KAUKI walipendekeza wanaukoo kuwa wabunifu katika kutoa michango yao, hii ni pamoja na kutoa bidhaa au mazao ambayo yatajulikana kama mchango. Kama ni nafaka au mifugo, inaweza kutumika kama chakula moja kwa moja au ikauzwa na zikapatikana fedha ambazo zitajumuishwa kwenye bajeti inayoandaliwa.

 

MICHANGO TOKA VYANZO VINGINE

Tumekuwa tukijitahidi kutafuta fedha toka vyanzo vingine ili kuweza kufanikisha Mikutano hii japo bado hatujapata mafanikio kwa kiasi kikubwa. Tuliweza kupata sehemu ya mchango toka Kiwanda cha Maji ya Kunywa ya Afrika kilichopo Kijijini Kidamali, katika Mkutano Mkuu wa Kwanza wa KAUKI. Jumla ya kiasi cha shilingi za Tanzania Laki Moja zilitolewa. Kwa hiyo, tunawahimiza wana KAUKI kubuni vyanzo vingine vya mapato kwa ajili ya michango ya kufanikisha mikutano hii.

Tunaweza kubuni miradi ya maandazi au chapati, au miradi yoyote ambayo mnadhani itatusadia kupata fedha kwa ajili ya kuweza kufanikisha Mkutano Mkuu huo.

 

TAREHE YA MKUTANO MKUU WA TATU WA KAUKI

Awali ya yote, Mkutano Mkuu wa Tatu ulipendekezwa ufanyika tarehe 23 na 24 Juni 2007, kijijini Kidamali, mkoani Iringa. Mkutano huo haukuweza kufanywa katika tarehe hizo kutokana na sababu zilizokuwa juu ya uwezo wetu. Kwa hiyo tarehe nyingine ya kufanyika kwa mkutano huo ilipangwa. Mkutano Mkuu wa KAUKI ulifanyika rasmi tarehe 30 Juni hadi 01 Julai, 2007, Kijijini Kidamali.

 

YALIYOJIRI KATIKA MKUTANO MKUU WA TATU WA KAUKI

Mambo yaliyojiri katika Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI ni pamoja na kuwasilishwa kwa Mada kama ‘Historia na Chimbuko la Ukoo wa Kivenule’, na ‘Changamoto za KAUKI katka Kujiletea Maendeleo’. Pia kulikuwa na taarifa mbalimbali kutoka kwa Viongozi wa Wakuu wa KAUKI na Viongozi wa Kanda. Kulikuwepo na muhimizo katika masuala ya elimu, maendeleo na ushirikiano wa dhati baina ya wanandugu.

 

Pamoja na masuala mengine, utambulisho baina ya wanaukoo yalifanyika kwa kina na kila ndugu/mwanaukoo alikuwa na kitambulisho ambacho alikivaa kifuani kwake. Kulikuwa na fursa mbalimbali kwa wanandugu kupeana uzoefu mbalimbali katika utafutaji wa maisha bora. Mbinu za kujiinua kimaisha zilifundishwa na wadau wenye uzoefu pamoja na aina mbalimbali za miradi ambayo ndugu wanaweza kufanya.

 

Kulikuwa na Mada Somo (Case Study) ambazo zilitumika kujifunzia mfano Kilimo cha Nyanya kinachofanywa na baadhi ya wanaukoo katika eneo la Magubike. Tunaamini kupata elimu ya kufanya shughuli za kujiletea maendeleo kama inavyofanywa na ndugu hao, itawasaidia wanandugu toka maeneo mengine kupata mwanga wa shughuli mbadala zitakazosaidia kupata kipato.

 

MIPANGO YA KAUKI

KAUKI inajikita kujiimarisha katika ngazi zote za kiutendaji, kiuendeshaji na kuleta mabadiliko ya kiuchumi, kielimu na kimaendeleo. Baadhi ya mikakati ambayo ni muhimu kuzingatiwa ni pamoja na:

1.        KAUKI kuwa na ofisi yake Kijijini Kidamali na pia sehemu nyingine za Kanda ambapo wanaukoo wanadhani kuna umuhimu kuwepo.

2.       Kushughulikia usajili wa KAUKI ili tupate fursa ya kufanya shughuli kubwa zaidi.

3.       KAUKI kuwa na sanduku lake la posta.

4.       Kufungua Akaunti katika Benki yeyote. Suala na akaunti limo ndani ya Katiba na kinachotakiwa ni utekelezaji tu.

5.       KAUKI kuwa na vitendea kazi mfano Kompyuta, Printa, Simu, Meza na Viti.

6.       KAUKI kuanza kutoa elimu mbalimbali kwa wadau wake.

7.       KAUKI kubuni na kutekeleza miradi mbalimbali ambayo itawasadia wanajamii.

8.       KAUKI kuwa na kitengo cha Utaalam wa Kitaaluma na Kiujuzi ambacho kitafanya shughuli za kuiletea fedha KAUKI, pamoja na miradi mbalimbali.

9.       KAUKI kujitangaza kwa asasi nyingine za ndani ya nchi na nje.

 

MAPUNGUFU YA KAUKI NA WATENDAJI WAKE

Uongozi wa KAUKI ulioapishwa rasmi wakati wa Mkutano Mkuu wa Pili, kuanza kutekeleza wajibu wake, umeonyesha mapungufu mengi, katika mfumo mzima wa utendaji kazi zake. Baadhi ya mapungufu hayo ni pamoja na kushindwa kubisa kutekeleza baadhi ya mikakati ambayo ilikuwa ni sehemu ya makubaliano na pia mipango ya mbeleni ya maendeleo ya KAUKI. Kwa mfano baadhi ya majukumu ambayo bado hayajatekelezwa ni pamoja na:-

1.        Kusambaza Ripoti ya Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule kwa Viongozi wa Kanda na pia kwa wanaukoo wa ujumla.

2.       Kushindwa kutolewa kwa nakala nyingi za Ripoti ya Mkutano Mkuu wa Kwanza;

3.       Kutokuwa na Kalenda ya Shughuli za Mwaka;

4.       Kushindwa kufanya uchaguzi wa Viongozi wa Kamati Ndogo.

5.       Kushindwa kufanya vikao vya Kamati Kuu;

6.       Kushindwa kutolewa na kusambazwa kwa Katiba ya KAUKI;

7.       Kushindwa kusambaza stakabadhi za malipo kwa viongozi wa kanda;

8.       Ushirikiano finyu baina ya viongozi wa ngazi mbalimbali wa KAUKI;

9.       Viongozi wengi wa KAUKI kushindwa kutekeleza wajibu wao;

 

MAPUNGUFU YALIYOFANYIWA KAZI

Kusambaza Ripoti ya Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule kwa Viongozi wa Kanda na pia kwa wanaukoo wa ujumla. Katika mkutano mkuu wa Tatu angala nakala kadhaa za ripoti hiyo zilidurufiwa (tolewa) na kugawiwa kwa viongozi mbalimbali wa kanda.

 

Uchaguzi wa Viongozi wa Kamati Ndogo. Uchaguzi wa Viongozi wa Kamati ulifanyika wakati wa Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI, na hivyo kuwapata viongozi wa Kamati Mbalimbali.

 

Kusambazwa kwa Katiba ya KAUKI: Katika Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI, nakala kadhaa za Katiba zilisambazwa kwa viongozi wa Kanda ili kuwapelekea wanaukoo wengine waweze kuzisoma na kuzielewa.

 

Kusambaza stakabadhi za malipo kwa viongozi wa kanda. Umuhimu wa kuzisambaza stakabadhi ulijidhihirisha katika Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI. Nakala za Stakabadhi zilinunuliwa, kugongwa mhuri wa KAUKI na kusambazwa kwa Viongozi wa Kanda.

 

Viongozi wakuu wa KAUKI

Wafuatao ni Viongozi wanaounda Uongozi wa KAUKI.

1.        Mwenyekiti                       Faustino          S.         Kivenule

2.       Makamu Mwenyekiti      Christian          J.          Kivenule

3.       Katibu Mkuu                    Adam              A.         Kivenule

4.       Katibu Msaidizi                 Donath            P.         Mhapa

5.       Mhasibu Mkuu                 Justin               D.         Kivenule

6.       Mhasibu Msaidizi              Carolina          S.         Kivenule

 

 

 

 

WALEZI

1.        Stephan                Mhapa

2.       John                       Kivenule

3.       Augustino             Kivenule

 

 

 

 

Imeandaliwa na:                                                   Imethibitishwa na:

 

…………………………………………….                                         …………………………………………………

ADAM A. KIVENULE                                                 DONATH P. MHAPA

KATIBU MKUU – KAUKI                                       KATIBU MSAIDIZI- KAUKI

 

TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI YA MFUKO WA KAUKI

Mnamo tarehe 25 Juni 2006, wakati wa Mkutano Mkuu wa Pili wa KAUKI, wanaukoo kwa pamoja walikubaliana na pendekezo kuanzishwa kwa mfuko wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule, ambalo pia limo ndani ya Katiba [Ibara ya 5, kifungu cha 5.1, Sehemu ya (ii)]. Kama inavyoelezwa katika Katiba ya KAUKI, lengo la mfuko huu ni kusaidia kuinua hali za maisha na kukabiliana na matatizo mbalimabli ya kiuchumi, kiafya na kimaendeleo (ugonjwa, elimu na kujijiinua kiuchumi) kwa wana-KAUKI pale utakapokuwa umeimarika.

 

Pendekezo la kuanzishwa kwa mfuko wa KAUKI lilipitishwa na kukubaliwa na washiriki wote wa Mkutano Mkuu wa Pili, wakati tukiijadili Katiba ya KAUKI. Mara baada ya kupitishwa, washiriki wa mkutano huo walianza utekelezaji papo kwa papo kwa kuanza kutoa michango ya kuanzia (kiingilio) ya shilingi elfu mbili (2,000/-) kwa kila mwana-KAUKI.

 

Katika zoezi hili, jumla ya shilingi 29,300/-zilipatikana. Kiasi hicho kilipatikana kutoka kwa baadhi ya washiriki wa mkutano ambao walikuwa tayari kulipa kiasi hicho kwa siku hiyo.  Baada ya kulipa kiasia cha shilingi 2,000/=, mwana-KAUKI ana wajibu wa kuendelea kulipa michango wa kila mwezi wa shilingi 500/= kama inavyobainishwa katika Katiba ya KAUKI [Ibara ya 5.0, Kifungu cha 5.2, Sehemu ya (ii)].

 

MAKUSANYO YA MICHANGO KUTOKA KANDA MBALIMBALI

Tarehe

Maelezo

Kiasi

30/06/2006

Makusanyo wakati wa Mkutano Mkuu wa KAUKI

29,300.00

25/05/2007

Mweka Hazina alikabidhiwa na Mwakilishi Kanda ya Kidamali

38,000.00

10/06/2007

Mweka Hazina alikabidhiwa na Mwakilishi Kanda ya Magubike

10,000.00

30/06/2007

Mweka Hazina alikabidhiwa na Mwakilishi Kanda ya Ilole

22,000.00

30/06/2007

Mweka Hazina alikabidhiwa na Mwakilishi Kanda ya Dar es Salaam

40,000.00

Jumla ya Mkusanyo

139,300.00

 

MATUMIZI

Mnao tarehe 26/07/2006, kiasi cha shilingi 20,000/= kilitolewa kwa Bwana Adam Alphonce Kivenule, ambaye ni Katibu Mkuu wa KAUKI kwa ajili ya shughuli ya uchapishaji wa Katiba ya Umoja wa Ukoo wa Kivenule.

 

Tarehe 10/07/2006 kiasi cha shilingi 2,000/= kilitumika kununua vitabu vya stakabadhi kwa ajili ya michango endelevu na kianzio ya KAUKI.

 

Kwa hiyo jumla ya matumizi ni shilingi 22,000/= tu. Salio baada ya matumizi ni shilingi 117,300/= fedha taslimu.

 

Taarifa hii iliandaliwa na Mhasiku Mkuu wa KAUKI, Ndugu Justin D. Kivenule

 

 

 

 

 

Imeandaliwa na:                                                   Imethibitishwa na:

 

 

…………………………………………….                                         …………………………………………………

JUSTIN D. KIVENULE                                                 FAUSTINO KIVENULE

MHASIBU MKUU – KAUKI                                   MWENYEKITI - KAUKI

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

CHIMBUKO NA HISTORIA YA UKOO

Wawezeshaji

1.      William               Kivenule

2.     Augustino          Kivenule

3.     Benard                Kivenule

 

TAARIFA YA UJUMLA YA CHIMBUKO NA HISTORIA YA UKOO

Mada hii Historia na Chimbuko la Ukoo wa Kivenule, iliwasilishwa na Ndugu William Sigatambule Kivenule kutoka Kidamali kwa kushirikiana na Ndugu Augustino Kivenule kutoka Nduli na Bwana Benard Kivenule wa Ilole. Wote kwa ujumla wao walijitahidi kueleza na kufafanua Kiini na Chimbuko la Ukoo huu. Kwa kuanza Mwezeshaji kutoka Kidamali Ndugu William, aliwaeleza washiriki wa mkutano huo kuwa Babu MTELINGOMA BALAMA ndiye aliyekuwa mwanzilishi halisia wa ukoo wa Kivenule. MTELINGOMA ndiye aliyemzaa Babu TAGUMTWA BALAMA (KIVENULE).

 

Babu TAGUMTWA BALAMA (KIVENULE) ndiye aliyewazaa Babu TAVIMYENDA KIVENULE na Babu KALASI KIVENULE. Ikumbukwe kuwa, jina halisi la ukoo wa Kivenule ni BALAMA. Kama ilivyokwisha julikana katika mada iliyowasilishwa katika Mkutano Mkuu wa Kwanza na wa Pili wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule, ambapo ilielezwa kuwa, neno KIVENULE linamaanisha sifa ya kuwa jasiri Vitani na hasa katika kutumia silaha za Mishale na Mikuki yaani kwa Lugha Asilia ya Kihehe “KUMIGOHA”.  Yaani kwa maana nyingine LIGALU yenye maana ya Kwihoma ImigohaKuhoma Watavangu au Kuvenula Avatawangu. LIGALU maana yake Vita. Kuhoma maana yake Kuchoma na Migoha maana yake Mikuki. Venula maana yake ua, fyeka maadui.

 

LIGALU ndiyo iliyochangia kuzaliwa kwa jina la Ukoo la KIVENULE. KIVENULE maana yake ni Ushujaa kutokana na Shabaha ya Mikuki.

 

KUVENULA likiwa na maana halisi ya kuwa na shabaha ya kuwaangamiza maadui kwa kutumia silaha ya Mishale na Mikuki. Babu zetu akina TAGUMTWA BALAMA walilidhihirisha hili katika Vita na Watavangu na hivyo kusababisha kuzawadiwa kwa jina la KIVENULE kama jina la sifa kutokana na ushujaa katika Vita.

 

Baada ya kuwazaa watoto hawa wawili yaani TAVIMYENDA na KALASI, walisafiri na kufika hadi sehemu ya KALENGA, wakiwa katika harakati za kutafuta maisha. Ndipo Babu TAVIMYENDA KIVENULE alipoombwa na Mzee MYINGA aende akamsaidie kumchungia mifugo yake eneo la MAGUBIKE na pia Babu KALASI KIVENULE naye kuamua kwenda eneo la ILOLE kutafuta maisha.

 

Akiwa eneo la MAGUBIKE, Babu Tavimyenda Kivenule akafanikiwa kupata watoto Saba (7), yaani BABU KAVILIMEMBE KIVENULE, BABU MGAYAFAIDA KIVENULE, BABU SIGATAMBULE KIVENULE, BIBI MGASI KIVENULE, BIBI MALIBORA KIVENULE, BIBI SIGINGULIMEMBE KIVENULE, BABU ABDALAH KIVENULE NA BIBI SIKIMBILAVI SEMABIKI.  Huyu Bibi Sikimbilavi Semabiki hakuwa mtoto wa Babu Tavimyenda ila alikuwa ni mtoto wa kufikia kwa  Bibi yetu.

Baadhi ya akina Babu walifanikiwa kuwa na wake zaidi ya mmoja na hawa walikuwa ni Babu SIGATAMBULE KIVENULE, ambaye mke wake wa kwanza alikuwa anaitwa SIWANGUMHAVI SINGAILE, mke wake wa pili alikuwa anaitwa  NYANYILIMALE SINGAILE na mke wa Tatu, PANGULIMALE SETWANGA. Mke wa pili na tatu wa Babu Sigatambule bado wapo hai.

 

Babu HUSEIN KIVENULE naye alikuwa na wake wawili ambao ni YIMILENGERESA SEMSISI na DALIKA SETALA. Taarifa za wake wa Babu wengine bado zinaendelea kufanyiwa utafiti. Babu MGAYAFAIDA KIVENULE yeye hakubahatika kuoa wala kuwa na mtoto. Alikuwa ni mlemavu na ndiyo maana ya jina lake MGAYAFAIDA.

 

Kwa upande wa ILOLE, Babu KALASI KIVENULE alibahatika kuwa na watoto watatu ambao ni Babu SALAMALENGA (KAHENGULA) KIVENULE, MGUBIKILA (NYAKUNGA) KIVENULE NA SEKINYAGA KIVENULE.

 

BABU SALAMALENGA KIVENULE alikuwa mwanaume peke yake na wawili waliobaki walikuwa ni wanawake. Babu Salamalenga Kivenule alioa wake watatu ambao ni Bibi NYANGALI, BIBI SEMFILINGE MHENGAATOSA NA BIBI SEMKONDA CHOGAVANU. Kupitia kwa wake zake watu, Babu Salamalenga ndiye aliyeeneza Ukoo wa Kivenule katika maeneo ya Nduli, Ilole, Mgongo na Kigonzile.

 

MABORESHO YA TAARIFA ZILIZOPO KUHUSU HISTORIA YA UKOO WA KIVENULE

Kwa mujibu wa taarifa za kihistoria kutoka eneo la ILOLE inaonesha kuwa, Babu Salamalenga alitokea Magubike na kuelekea eneo la Kaskazini. Baadaye kulitokea ugomvi baina ya makabila, na hivyo kusababisha vita. Salamalenga akapelekwa eneo la Pawaga Vitani, ambako alipigana mpaka vita ilipoisha. Baada ya kurudi toka Vitani, Babu Salamalenga alifanikiwa kupata wake watatu, yaani Bibi Nyangali, Bibi Semfilinge na Bibi Semkonda. Hawa wake zake wote wa watatu alifanikiwa kuzaa nao watoto.

 

Awali, Bibi Semkonda aliolewa na Mwamatagi na kuzaa mtoto analiyeitwa Sipanganakumutwa Sematagi. Semnyawanu wapo Kalenga na ni watoto wa Sipanganakumtwa.

 

Watoto wa kila mke wake wameooneshwa kama ifuatavyo:

1.      Bibi   Semkonda

  • Pangayena                 Kivenule
  • Jonas                            Kivenule
  • Samwel                       Kivenule
  • Balasamaneno           Kivenule
  • Daud (William)           Kivenule
  • Barton                         Kivenule

 

2.     Bibi Semfilinge

  • Chogavanu                 Kivenule
  • Munguatosa               Kivenule
  • Mwilimilisa (Gungamesa) mtoto wa Sekinyaga

 

3.     Bibi Nyangali

  • Tindasulanga              Kivenule
  • Sigondola                    Kivenule
  • Shaban                       Kivenule
  • Gungamesa                Kivenule

 

Mpaka, inaonyesha katika historia ya Ukoo wa Kivenule kuwa Babu Kalasi alimzaa Babu Salamalenga.

 

Katika Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI, wawezeshaji wa Mada ya Chimbuko na Historia ya Ukoo, bado hakujawa na taarifa rasmi zinazojitosheleza kuhusiana na mtiririko wa kizazi hiki cha Ukoo wa Kivenule. Katika mkutano wa Tatu wa KAUKI, wawezeshaji walibainisha kuwa, muundo wa Ukoo kwa upande wa Kidamali na Magubike upo kama ifuatavyo:

Babu Mtelingoma Balama alimzaa Babu Tagumtwa. Pia, Babu Tagumtwa alikuwa na wake wawili (2); yaani Bibi Sesambagi na mwingine ambaye jina lake halikuweza kuandikwa (patikana) ambaye alimzaa Babu Kalasi.

 

Babu Tavimyenda ambaye ni mtoto wa Babu Mtelingoma, alikuwa na wake watatu (3) ambapo mmoja wa wake zake alikuwa anaitwa Bibi Mkami Sekabogo. Bibi Mkami Sekabogo alikuwa na mtoto wake wa kwanza ambaye aliitwa Sikimbilavi Semabiki.  Mtoto huyu alimzaa kwa mme mwingine. Baadaye alipokuja kuolewa na Babu Tavimyenda, aliweza kuwazaa watoto wafuatao:

1.        Myumbila                         (Kavilimembe) Kivenule

2.       Mgaifaida             Kivenule

3.       Sigatambule         (Matesagasi) Kivenule

4.       Hussein                  Kivenule

 

Mke wa pili wa Babu Tavimyenda Kivenule aliwazaa watoto wafuatao:

Abdalah                      Kivenule

Sigungilimembe          Kivenule

Malibora                     Kivenule

 

Mke wa Tatu wa Babu Tavimyenda Kivenule alimzaa mtoto mmoja tu aliyejulikana kwa jina la Mgasiyumhavi Kivenule.

 

Nao watoto wa Babu Tavimyenda kwa Mke wake Bibi Mkami Sekabogo walijaliwa kuwa na familia zao isipokuwa kwa Babu Mgaifaida ambaye hakubahatika kupata familia. Babu Mgaifaida pia alikuwa mlemavu.

 

Babu Kavilimembe ambaye pia ni mtoto wa kwanza wa Babu Tavimyenda Kivenule, alijaliwa kuwa na wake wawili na kuzaa nao watoto. Mke wa kwanza wa Babu Kavilimembe alikuwa anaitwa Bibi Sekusiga ambaye alizaa watoto wafuatao:

1.        Elizabert               Kivenule

2.       Dalikimale            Kivenule

3.       Sandra                  Kivenule

4.       Pangalasi              Kivenule

 

Mke Mdogo wa Babu Kavilimembe Kivenule ambaye pia alijulikana kwa jina la Sekusiga Mdogo alizaa watoto wafuatao:

1.        Salikuvaganga     Kivenule; na

2.       Francis                   Kivenule

 

NAMNA YA KUHIFADHI KUMBUKUMBU ZA KAUKI

Mada ya Historia na Chimbuko la Ukoo, pia ilileta mjadala ni namna gani tutahifadhi kumbukumbu za ukoo; na pia njia mbadala za kutunza taarifa zinazohusiana na Ukoo. Wana-KAUKI kwa ujumla wao walikuja na hoja mbalimbali zikiwemo hizi zifuatazo:

Kuwepo na viongozi (uongozi) wenye jukumu la kufuatilia taarifa mbalimbali zinazohusiana na ukoo katika maeneo mbalimbali ambapo wanadhani zinaweza kupatikana. Pia pawepo na mfumo unaoeleweka wa kuhifadhi kumbukumbu aidha katika maandishi au namna nyingine yeyote. Pia ilipendekezwa pawepo na taarifa za mara kwa mara katika maandishi ambazo zitakuwa zinawasilishwa wakati wa mikutano mikuu ya KAUKI.

Wajumbe wa mkutano walipendekeza umuhimu wa kumtumia Babu Hussein ambaye bado yupo hai kwa sababu ana taarifa nyingi zinazohu ukoo wa Kivenule. Pia ilikubaliwa na wana-KAUKI kuwa licha ya kuwepo kwa majina ya kisasa na ya Ubatizo ambayo walipewa hawa Babu na Bibi zetu; ni vyema pia majina yote yakajumuishwa kwenye makaburi yao ikiwa ni sehemu mojawapo ya kutunza kumbukumbu. Majina mapya siyo maarufu (au hayafahamiki sana); kwa hiyo ni vyema bado tukaendelea kutumia majina yote ili tusipoteze kumbukumbu.

 

Wana-KAUKI pia walipendekeza yachongwe mawe yenye majina ya marehemu ambapo tutayaweka katika makaburi kwa sababu siyo rahisi kufutika na kupotea. Taarifa za historia ya ukoo ni muhimu ziwekwe kwenye maandishi hususani vijitabu vidogo vidogo ambavyo vitasambwa kwa wanaukoo mbalimbali na kuweza kujisomea.

 

Mada hii ya Chimbuko na Historia ya Ukoo wa Kivenule, ni mwendelezo wa taarifa mbalimbali ambazo tumekuwa tukizitafuta na kuziwasilisha katika Mikutano kama hii. Katika Mkutano Mkuu wa Kwanza, wa Pili na pia huu wa tatu Mada ya Chimbuko na Historia ya Ukoo iliwasilishwa. Kinachofanyika kwa hivi sasa ni kuzidi kuiboresha na kuziongeza taarifa kwenye taarifa za awali ambazo tayari tulikwisha zipata.  

 

Tafsiri za Majina Mbalimbali yaliyopo katika Ukoo wa Kivenule

Kidagamhindi             Heka heka za kukimbia kodi wakati wa mkoloni

Tunyahindi                  Kupigwa pigwa na wakoloni

Mwanitu                     Alizaliwa kweusi (kwa kutumia lung’ali). Kuwasha moto ili kupata mwanga kwa kutumia kuni au aina fulani ya nyasi. Mara nyingi ving’ali vinakuwa vinazimika.

Kadungu                     Kuwa na Dungu kubwa (kuwa na kitovu kikubwa)

Kibumo                       Mvefi (Mtu anayelialia)

Mlagile                        Alizaliwa wakati Bibi yake hayupo. Wakati anaonyeshwa Bibi yake akisema Mlagile  akaitwa Mlagile.

Fatamali                     Alifuata mali

Yamkopita                 Bibi alipomzaa mtoto wa kwanza na kisha kufariki, akapata jina la ya Mkopite

Luhanage                   Wakati Bibi anazaa watoto wanakufa, alipomzaa mtoto na akaugua sana basi akaitwa Luhanage. Luhanage maana yake ni kuugua sana.

Mgendwa                   Alizaliwa kwa taabu. Alizaliwa kwa waganga wa kienyeji kwa tabu wakiwa safarini

Msinziwa                    

Kanolo                         Wakati ameugua, anapiga ramli huki akitembea kwa waganga.

Yimilengeresa              Mzee Babu Husein alichukuliwa kwenye Vita ya Pili ya Dunia. Wahindi walikufa sana na Waingereza wakashinda Vita.

Misamiti ya Lugha ya Kihehe

Mhisive                        Binamu

Nyavana                    Degedege

Ligalu                          Vita

Watavangu                Wakubwa (Wakuu wa Nchi) kabla ya Ukoloni

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


MUUNDO UKIONESHA CHIMBUKO LA UKOO WA KIVENULE (MWIBALAMA)

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 



TAARIFA YA UTENDAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO ZA KAUKI KATIKA KANDA

Katika ratiba ya Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI, kulikuwa na kipengele ambacho kilihusu utoaji na upokeaji wa taarifa mbalimbali za utendaji wa shughuli za maendeleo katika kanda. Viongozi wa kanda husika walitakiwa kuwasilisha taarifa rasmi kwa wajumbe wa mkutano mkuu, kuhusu shughuli mbalimbali za maendeleo katika maeneo yao. Jumla ya kanda tano ziliweza kuwasilisha taarifa zao za utendaji kwenye hadhara ya mkutano huo. Kanda hizo ni pamoja na Kidamali, Magubike, Nduli ambayo ilijichanga na Mgongo na Itagutwa, Ilole na Dar es Salaam. Lifuatalo hapa chini jedwali linaloonyesha muainisho wa shughuli mbalimbali zilizofanyika katika kipindi cha mwaka 2006 hadi 2007.

 

Kanda

Uhamasishaji

Mwitikio

Ushirikiano

mafanikio

Matatizo

Dar es Salaam

Duni/finyu

Hakuna maendeleo

Watu wavivu kufika katika vikao

Duni: Visingizio vingi mfano kukosa muda (busy); kukosa fedha

Ni mdogo hususani kuona wagonjwa; na pia wakati wa matatizo, watu hawajitoi kwa hiari

Hakuna

Mwitikio duni ni tatizo sugu.

Visingizio/Sababu haviishi

Ilole

Hawatoi fedha bila stakabadhi

Hawajaelewa dhana zima ya Umoja wa Ukoo wa Kivenule

Duni: Hawaitikii kwenye mikutano au vikao

Duni

Wanashiriki kikamilifu

Tatizo la kushiriki kwa ni kutoa fedha kidogo sana mfano shilingi mia moja (100/=)au mia mbili (200/=)

Mgongo/ Nduli na Itagutwa

Viongozi wanahamasisha;

Ndugu hawaelewi;

Wanaomba viongozi wa KAUKI watembelee kusaidia kuhamasisha

Upo wa wasiwasi

Hawatekelezi

Kidogo mzuri.

Misiba wanaukoo wanashiriki kikamilifu

Ushiriki katika matatizo upo

Stakabadhi zinahitajika

Mwitikio hauridhishi.

Imani kwa viongozi wao bado ni mdogo. Wanahitaji stakabadhi ili kutoa michango na malipo mbalimbali.

Magubike

Mzuri isipokuwa Ibogo

Mzuri

Upo katika matatizo na raha. Lakini bado kuna tatizo katika kuona wagonjwa

Yapo

Kidogo

Kidamali

Mzuri. Wanashiriki kikamilifu na vizuri

Duni hususani katika michango; na pia mwitikio katika vikao sio mzuri

Ushirikiano katika matatizo mfano misiba, ugonjwa ni mzuri,

Yapo kwa kiasi kikubwa

Kiasi Fulani bado kuna upinzani katika kutoa michango ya mwezi na pia ya Mikutano Mikuu

Nyamahana

 

 

 

 

 

Igangimale

 

 

 

 

 

 

Taarifa ya utendaji wa kanda mbalimbali zilizowasilishwa na viongozi wa kanda husika zilikuwa ni fupi kutokana na kutopewa taarifa mapema kuhusu kuwasilisha. Tunatarajia kupokea taarifa rasmi zinazojitosheleza katika Mkutano Mkuu wa Nne wa KAUKI, utakaofanyika Ilole, tarehe 28-29 Juni 2008.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

UONGOZI WA KAUKI

Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) ina viongozi ambao jukumu lake ni kuhakikisha kuwa gurudumu la maendeleo ya wana-KAUKI linasonga mbele. Viongozi hawa walichaguliwa katika Mkutano Mkuu wa Pili wa KAUKI uliofanyika tarehe 24 na 25 Juni 2006. Kwa mujibu wa Katiba ya KAUKI, viongozi wataitumikia KAUKI kwa muda wa miaka mitatu. Hii ikimanisha kuwa muda wa kuitumikia KAUKI utakoma ifikapo mwaka Juni 2006. Yafuatayo ni majina ya viongozi na vyeo vyao:

1.        Ndugu      Faustino          Sigatambule   Kivenule          Mwenyekiti    

2.       Ndugu      Christian          John                 Kivenule          Makamu Mwenyekiti

3.       Ndugu      Adam              Alphonce         Kivenule          Katibu Mkuu

4.       Ndugu      Donath            Peter               Mhapa            Katibu Msaidizi

5.       Ndugu      Justin               Daniel              Kivenule          Mweka Hazina

6.       Ndugu      Carolina          Sigatambule   Kivenule          Mweka Hazina Msaidizi

 

Picha za Viongozi Wakuu wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI)

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

VIONGOZI WA KANDA WA KAUKI

Uchaguzi wa Viongozi wa Kanda ulifanyika sambamba na uchaguzi wa Walezi wa KAUKI. Kuna baadhi ya kanda zinaendelea kuwa na viongozi wake wa zamani. Kanda chache bado hazijapata viongozi wake, lakini tunategemea kufanya utaratibu wa kuweza kufanikisha upatikana wa viongozi hao.

 

Wafuatao hapa chini ni viongozi wapya wa Kanda wa KAUKI.

A. Ilole

  1. Pius                 Kivenule
  2. Bernadi           Kivenule
  3. Titus                Kivenule

 

B. Nduli

  1. Anna               Kivenule
  2. Augustino       Kivenule

 

C. Itagutwa

  1. Anyesi             Kivenule
  2. Gipson             Kitu

 

D. Dar es Salaam

  • Ilole
  1. Ignas                Kivenule
  2. Innocent          Kivenule
  3. Delphinus        Kivenule

 

  • Kidamali
  1. Athuman        Mtono
  2. Sijali                 Kivenule

 

E. Nyamihuu

  1. Benjamin         Kivenule

 

F. Nyamahana

  1. Otavina          Kivenule

 

G. Ilala Simba

 

H. Kidamali

  1. George            Kivenule
  2. Jovin                Kivenule
  3. Jermana          Kivenule
  4. Pyela               Kivenule

MUUNDO WA KANDA

Kanda ya Magubike

  1. Magubike
  2. Ilala Simba
  3. Ibogo

 

Kanda ya Kidamali

  1. Kidamali
  2. Nzihi
  3. Nyamihuu
  4. Nyamahana
  5. Kalenga

 

Kanda ya Nduli

  1. Nduli
  2. Mgongo
  3. Itagutwa

 

 

Kanda ya Ilole

  1. Ilole

 

Kanda ya Dar es Salaam

  1. Dar es Salaam
  2. Morogoro

 

Kanda ya Mufingi

  1. Igowole
  2. Mafinga

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

UCHAGUZI WA VIONGOZI WA KAMATI MBALIMBALI NA KAMATI YA UTENDAJI

KANDA YA MAGUBIKE

Mipango na Maendeleo

Mwenyekiti:                Severin            Nyangalima

Katibu:                        Edimery          Nzala

 

Mahesabu na Fedha

Mwenyekiti:                Vitus                Nzala

Katibu:                        Conjeta           Kivenule

 

Maafa na Matatizo

Mwenyekiti:                Josephat          Lupola

Katibu:                        Romanus         Kivenule         

 

Nidhamu na Maadili

Mwenyekiti:                Anyesi                         Kivenule

Katibu:                        Kastilia            Nzala

 

KANDA YA KIDAMALI

Mipango na Maendeleo

Mwenyekiti:                Atanas                        Mbunda

Katibu:                        Jovin                Kivenule

 

Mahesabu na Fedha

Mwenyekiti:                George            Kivenule

Katibu:                        Janeth             Kivenule                     

 

Maafa na Matatizo

Mwenyekiti:                Sebastian        Nzala

Katibu:                        John                 Mgumba        

 

Nidhamu na Maadili

Mwenyekiti:                Jermana          Mhapa

Katibu:                        Innocent          Malambo

 

KANDA YA NDULI

Mipango na Maendeleo

Mwenyekiti:                Msafiri             Kivenule

Katibu:                        Winfrida          Kivenule

 

Mahesabu na Fedha

Mwenyekiti:                Anna               Kivenule

Katibu:                        Gipson             Kiito

 

Maafa na Matatizo

Mwenyekiti:                Alois                 Kivenule

Katibu:                        Aneth              Kivenule         

 

Nidhamu na Maadili

Mwenyekiti:                Augustino       Kivenule

Katibu:                        Machelina       Kivenule

 

KANDA YA ILOLE

Mipango na Maendeleo

Mwenyekiti:                Benard            Kivenule

Katibu:                        Atanas                        Kivenule

 

Mahesabu na Fedha

Mwenyekiti:                Pius                 Kivenule

Katibu:                        Anamalia        Kivenule

 

Maafa na Matatizo

Mwenyekiti:                Thadei             Nyakunga

Katibu:                        Anita               Kivenule         

 

Nidhamu na Maadili

Mwenyekiti:                Faustina          Kivenule

Katibu:                        Farida             Kivenule

 

KANDA YA DAR ES SALAAM

Mipango na Maendeleo

Mwenyekiti:                Innocent          Kivenule

Katibu:                        Fredy              Mapembe

 

Mahesabu na Fedha

Mwenyekiti:                Ignas                Kivenule

Katibu:                        Mwanne          Mtono

 

Maafa na Matatizo

Mwenyekiti:                Evaristo           Kivenule

Katibu:                        Evaristo           Mapembe      

 

Nidhamu na Maadili

Mwenyekiti:                John                 Kivenule

Katibu:                        Mzee               Mapembe

 

KANDA YA MUFINDI

Mipango na Maendeleo

Mwenyekiti:                Zavery             Kivenule

Katibu:                        Bakhita           Kivenule

 

Mahesabu na Fedha

Mwenyekiti:                Gloria              Kivenule

Katibu:                        Florian             Kivenule

 

 

Maafa na Matatizo

Mwenyekiti:                Ailin                 Kivenule

Katibu:                        Victoria            Kivenule         

 

Nidhamu na Maadili

Mwenyekiti:                Rustica                        Kilimwiko

Katibu:                        Anamery         Kidenya

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

WALEZI WA KAUKI

Mkutano Mkuu wa Pili wa KAUKI uliitumia fursa hiyo kufanya uchaguzi wa viongozi wa ngazi mbalimbali zikiwemo zile za walezi wa umoja huo. Lengo la kuwa na walezi ni kuusaidia uongozi unaounda timu ya uendeshaji wa KAUKI kwa kutoa ushauri pale panapoonekana panapwaya au kuyumba ili lengo na makusudio ya KAUKI yaweza kufikia lengo.

Walezi waliochaguliwa jukumu lao jingine ni kuhamasisha jamii inayounda umoja huo kuujua na pia kutoa ushirikiano baina ya wanandugu katika mambo mbalimbali yanayofanyika kwa manufaa ya KAUKI.

Waliochaguliwa kuwa walezi wa KAUKI ni pamoja na:

1.        Ignas          Kivenule          Dar es Salaam

2.       Augustino Kivenule          Ilole

3.       Stephan    Mhapa                        Kidamali

4.       John           Kivenule          Kilombero

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

MIPANGO NA MIKAKATI YA KAUKI KWA MWAKA 2006/7 – 2007/2008

Uongozi wa KAUKI ulioapishwa rasmi wakati wa Mkutano Mkuu wa Pili wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule, kuanza kutekeleza wajibu na majukumu mbalimbali yaliyopangwa kutekelezwa katika mwaka 2006/2007, ulipanga kutekeleza yafuatayo:-

1.        Kusambaza Ripoti ya Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule kwa Viongozi wa Kanda na pia kwa wanaukoo wa ujumla;

2.       Kutoa nakala nyingi za Ripoti ya Mkutano Mkuu wa Kwanza;

3.       Kuandaa Kalenda ya Shughuli za Mwaka 2006/2007;

4.       Kufanya uchaguzi wa Viongozi wa Kamati Ndogo;

5.       Kufanya vikao vya Kamati Kuu;

6.       Kutolewa nakala nyingi za Katiba ya KAUKI na kusambazwa;

7.       Kusambaza stakabadhi za malipo kwa viongozi wa kanda;

8.       Kuonyesha ushirikiano baina ya viongozi wa ngazi mbalimbali wa KAUKI;

9.       Viongozi wa KAUKI kutekeleza wajibu wao;

10.   KAUKI kuwa na sanduku lake la posta;

11.      KAUKI kufungua Akaunti kwa ajili michango mbalimbali ambayo inachangwa na wanachama wake.

 

Katika malengo ya mwaka 2006/2007 KAUKI imejitahidi kutekeleza majukumu yake kadri ya muda na hali ya fedha ilivyoruhusu. Usambazaji wa ripoti umefanyika kwa kiwango cha juu katika Mkutano wa Pili na Tatu; Uchaguzi wa Viongozi wa Kamati Ndogo na Kamati ya Utendaji ulifanyika wakati wa Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI. Uchaguzi wa Viongozi ulishafanyika kwa ngazi mbalimbali na Usambazaji wa Stakabadhi za Malipo tayari umefanyika katika Kanda husika.

 

MIPANGO YA KAUKI 2007/2008

KAUKI inajikita kujiimarisha katika ngazi zote za kiutendaji, kiuendeshaji na kuleta mabadiliko ya kiuchumi, kielimu na kimaendeleo. Baadhi ya mikakati ambayo ni muhimu kuzingatiwa ni pamoja na:

1.        KAUKI kuwa na ofisi yake Kijijini Kidamali na pia sehemu nyingine za Kanda ambapo wanaukoo wanadhani kuna umuhimu kuwepo.

2.       Kushughulikia usajili wa KAUKI ili tupate fursa ya kufanya shughuli kubwa zaidi.

3.       KAUKI kuwa na sanduku lake la posta.

4.       Kufungua Akaunti katika Benki yeyote. Suala na akaunti limo ndani ya Katiba na kinachotakiwa ni utekelezaji tu.

5.       KAUKI kuwa na vitendea kazi mfano Kompyuta, Printa, Simu, Meza na Viti.

6.       KAUKI kuanza kutoa elimu mbalimbali kwa wadau wake.

7.       KAUKI kubuni na kutekeleza miradi mbalimbali ambayo itawasadia wanajamii.

8.       KAUKI kuwa na kitengo cha Utaalam wa Kitaaluma na Kiujuzi ambacho kitafanya shughuli za kuiletea fedha KAUKI, pamoja na miradi mbalimbali.

9.       KAUKI kujitangaza kwa asasi nyingine za ndani ya nchi na nje.

 

 

 

 

 

MAJUMUISHO YA MKUTANO MKUU WA TATU WA KAUKI

Katika mkutano mkuu wa tatu wa KAUKI, shughuli mbalimbali zilitarajiwa kufanyika kwa mujibu wa ratiba na pia kuna majukumu ambayo yalionekana ni muhimu na ni vyema yakawasilishwa kwa wajumbe waliohudhuria mkutano huo, pia yalifanyika. Lengo la kufanya majumuisho hayo ni kumwezesha msomaji wa ripoti hii kuelewa kwa kina kile kilichofanyika kwa siku mbili za mkutano mkuu. Ripoti hizi mara nyingi huwa ni kubwa na lengo la kuwa na kipengele cha majumuisho pia ni kumsaidia msomaji ambaye atahitaji kuisoma ripoti yote, kupata angalau dondoo ya kile kilifanyika katika mkutano huo.

 

Katika Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI, Mada ya Chimbuko na Historia la Ukoo ilikuwa ya kwanza kuwasilishwa kwa mujibu wa ratiba. Wawezeshaji wa mada walikuwa ni Ndugu William Sigatambule KIvenule, Ndugu Augustino Kivenule na Ndugu Benard Kivenule. Hii haikuwa mara ya kwanza kwa mada hii ya Chimbuko na Historia ya Ukoo wa kuwasilishwa katika mikutano mikuu kama huu. Kumekuwepo na mada hii katika mikutano mikuu mengine iliyokwisha fanyika. Katika Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI, lengo la kuwasilisha mada hii ilikuwa ni kuzidi kuijadili kimapana zaidi na pia kupata taarifa mbalimbali ambazo zimekuwa zikikusanywa katika kipindi cha mwaka mmoja tangu ulifanyika Mkutano Mkuu wa Pili wa KAUKI, June 24 na 25, 2006. Baada ya kuwasilishwa na kujadiliwa kwa mada hii, wajumbe waliohudhuria mkutano huu walipendekeza hatua za makusudi zifanyike za kutunza kumbukumbu za Historia ya Ukoo; na hususani kuwa na chombo cha kutunza kumbukumbu za ukoo.

 

Hatua ya awali tayari inaendelea kufanyika kadri muda unavyozidi kwenda kwani kila mwaka baada ya kufanyika mkutano mkuu, ripoti yenye taarifa za matukio mbalimbali inaandaliwa na kutunzwa katika makaratasi na Sidi (Compact Disk [CD]). Hii ni hatua nzuri kwa kuanza, na tumekuwa tukihifadhi taarifa mbalimbali zinazowasilishwa katika mkutano mkuu. Hii ni pamoja na michoro na majedwali, orodha ya majina ya wanaukoo na pia majina mbalimbali ambayo yalikuwa yakitumika na pia bado yanaendelea kutumika na ndugu zetu.

 

Baadhi ya majina ya wazee wetu ambayo tayari tumeanza kuyaenzi ni pamoja na “Tagumtwa”; “Tavimyenda”; “Sigatambule”; “Mtelingoma”; “Kalasi” na majina mengine mengi ambayo kwa siku ya leo hatujayataja. Ni vyema majina hayo ya asili pia yakaandikwa kwenye makabuli na kwenye mabano yataandikwa majina ya ubatizo. Wazo la kuchonga mawe toka Chuo cha Sukari cha Taifa kama lilivyopendekezwa itabidi litafanyiwe kazi.

 

Kama ilivyokubaliwa awali kuwa kuna umuhimu wa kuchapisha vitabu vya “Historia ya Ukoo” vitakavyouzwa na kuongeza kipata katika mfuko wa Ukoo. Suala la kuandaa vitabu halitakuwa gumu sana kwa sababu tayari tumekuwa tukizindaa ripoti za mikutano mikuu kila mwaka. Kwa msaada wa teknolojia ya habari na mawasiliano sasa angalau wigo wa usomaji wa taarifa mbalimbali za Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) unaendelea kupanuka. Kwa wale ambao watashindwa kupata nakala za ripoti za mikutano mikuu iliyopita pamoja na taarifa mbalimbali sasa pia wanaweza kupata taarifa hizo kupitia www.tagumtwafoundation.wetpaint.com

UZOEFU WA WANA UKOO KATIKA SHUGHULI ZA MAENDELEO

Uzoefu wa takwimu zinaonyesha kuwa wana-KAUKI walio wengi ni wakulima kwa asilimia 85% na 5% ni wafanyakazi, 5% ni wafanyabiashara na 5% wako katika sekta isiyo rasmi (ajira binafsi). Hivyo basi kwa kutambua hilo, KAUKI imetumia fursa ya mkutano huu kubadilisha uzoefu kwa kuangalia maeneo ya kuwekeza katika kilimo mfano: Wilaya ya Kilombero mkoa wa Morogoro, wanaukoo wameshauriwa kwenda kuwezekeza katika kilimo hasa maeneo ya Mbingu, Mgeta, Chita na Mlimba. Kwa mfano baadhi ya mazao yayostawi zaidi ni Miti, Mbunga, Ndizi na Mahindi.

 

Eneo la Itatugwa, imebainika kuwa kuna maeneo mazuri ya kilimo; hivyo jamii inayounda KAUKI imeshauriwa na kukaribishwa kwenda kuwekeza katika kilimo cha Tumbaku, Alizeti, Maharage, Mahindi na Kunde.

 

Katika eneo la Ilole, imebainishwa kuwa kuna ardhi nzuri na yenye rutuba, hivyo fursa ya kuwekeza imejionesha dhahiri na hivyo wana-KAUKI kushauriwa kwenda huko na kujishughulisha na shughuli za kiuchumi.

 

Uzoefu katika jiji na Dar es Salaam unaonyesha kuwa kuna shughuli nyingi za kiuchumi, kijamii na kimaendeleo na hivyo ndugu wameshauriwa kuwa kabla ya kuamua kwenda huko, kwanza wajiulize wanataka kufanya shughuli gani. Wana-KAUKI walishauriwa kutopenda kukimbilia mijini hususani Dar es Salaam kwani kuna hatari ya kujenga jamii omba omba kama ilivyo kwa akina Matonya. Ni jambo la busara zaidi kama tutafikiria kubuni miradi ya maendeleo katika maeneo tuliyoyataja na kuepukana na maeneo ya mijini.

 

CHANGAMOTO ZA KAUKI KATIKA KUJILETEA MAENDELEO

Elimu:Umuhimu wa Elimu katika dunia ya leo umejitokeza sana kila mahali ambapo tunajaribu kupakimbilia. Vijana wetu ni vyema wakazitia umuhimu wa elimu na si vinginevyo ili wasiishie kuwa wakulima wadogo wasio na tija na pia wafanyakazi wa majumbani. Shule nyingi zinafunguliwa katika maeneo yetu ya vijijini yaani shule za Kata (Community Schools). Basi ni vyema tukatumia fursa hii kuwasomesha watoto kwani hata ada yake ni ndogo (20,000/-).

 

Kilimo: Kwa kuzingia mabadiliko ya hali ya hewa na teknolojia ya kisayansi hatuna budi kubadili mfumo wa kilimo tulionao hivi sasa. Kilimo cha tija ni vizuri kikatiliwa mkazo. Kilimo cha kisasa ndicho kilimo kitakachomkomboa mwana-KAUKI. Ni vyema tukawatumia wataalam mbalimbali wa kilimo wanaopatikana katika maeneo yetu ili kuongeza mapato. Elimu na kilimo cha kisasa havikwepani bado matumizi ya elimu katika kuinua kilimo ni vitu visivyoepukika. Mageuzi ya kilimo yanategemea kuwepo kwa utalaamu ulioshenezwa na elimu ihusiyo kilimo.

 

Umoja: Dhana ya umoja ni pana na kuna misemo mingi isemayo ‘Umoja ni Nguvu na Utengano ni Udhaifu’. Dhana ya umoja inatumika na inaendelea kutumika maeneo mbalimbali hapa dunia. KAUKI ni mfano mdogo tu wa vikundi mbalimbali vya kijamii ambavyo vimeungana. Kuungana kwa wanaukoo wa Kivenule kupitia KAUKI ni sehemu ndogo ya jitihada ambazo kama wanajamii tumeifikia. Safari bado ni ndefu kwa sababu kwa kuungana kwetu lazima tuonyeshe mafanikio Fulani. Kuungana bila malengo ni kazi bure. Ndiyo maana pamoja na kuungana pia tumeweka taratibu kupitia Katiba ambayo ni msingi wa taratibu za kutuongoza kufikia kule ambako tunakukusudia. Kila mwana-KAUKI ana wajibu wa kuisoma na kuilewa Katiba ya KAUKI.

 

Ushirikiano: Huu ni mmojawapo wa msingi wa umoja ambayo kama wana-KAUKI tayari tunao. Ushirikiano unapatikana katika nyanja mbalimbali mfano elimu, afya, furaha, kilimo na shida (matatizo). Mojawapo ya malengo ya kuanzishwa kwa KAUKI ni kudumisha ushirikiano na umoja miongoni mwa wanandugu. Ushirikiano unaanzia ngazi ya chini kabisa mtu mmoja mmoja, familia hadi jamii nzima. Msingi wa Katiba ya KAUKI ni usawa. Hakuna aliye bora zaidi ya mwenzake. Ndani ya KAUKI kila mmoja ana fursa sawa na mwingine; ana sauti sawa na mwingine; anastahili heshima kadri anavyostahili. Ndani ya Usawa kuna Utu. Hivyo, KAUKI nayo inahamasisha kuwepo na kulindwa kwa Haki za Binadamu. Mahitaji muhimu ya binadamu yamezingatiwa katika KAUKI na hivyo kuleta usawa.

 

Uongozi unabaki kuwa ni wajibu kwa kila mwana-KAUKI. Hivyo ni busara kwa kila kiuongozi kuongoza kwa msingi wa Katiba.

 

Mojawapo ya jitihadi za kuimarisha ushirikiano baina ya viongozi ni kufanya ziara mbalimbali katika maeneo ambayo viongozi na wana-KAUKI wanaishi kule. Katika kutekeleza maazimio hayo ziara zifuatazo zilipendekezwa kufanyika:

1.        Septemba 2007               - ILOLE

2.       Octoba 2007                    - NDULI

3.       Desemba 2007                 - MAGUBIKE

 

Hivyo tarehe rasmi za ziara katika maeneo husika ni vizuri zikapangwa na kujulikana ili kupunguza usumbufu usio wa lazima.

 

Kwa ujumla, mkutano mkuu wa tatu wa KAUKI umeonyesha mafanikio makubwa na tunatarajia mipango yote ya maendeleo tunayojiwekea kupitia mkutano huu itakuwa na mafanikio. Tunamtakia kila la kheri mwana KAUKI katika kipindi chote hiki mpaka hapo tutakapofanya mkutano mkuu mwingine wa nne, Kijijini Ilole.  

 

 

 

 

 

 

 

 

TATHMINI YA MKUTANO MKUU

Mahudhurio: Safari hii, ndugu/wanaukoo waonaishi sehemu za mbali mfano Dar es Salaam, Kilimanjaro, Mbeya, Morogoro na Ilole, waliohudhuria kwa wingi. Kwa mfano, kwa upande wa Dar es Salaam pekee, jumla na ndugu/wanaukoo 11 walihudhuria Mkutano Mkuu.

 

Upande mwingine ambao nao pia ulikuwa na uwakilishi mkubwa ulikuwa ni Ilole, Nduli, Kigonzile na Mgongo, ambapo kwa ujumla, ndugu/wanaukoo wapatao 12 walihudhuria mkutano huo, tofauti na uwakilishi wa mwaka jana, ambapo ndugu mmoja (1) alihudhuria Mkutano Mkuu.

 

Kwa upande wa ndugu/wanaukoo waliohudhuria Mkutano Mkuu toka mbali, ndugu/wanaukoo toka Mwanga mkoani Kilimanjaro, walikuwa ni baadhi ya ndugu waliosafiri safari ndefu kuja kwenye Mkutano Mkuu wa Pili wa Kivenule. Safari hii jumla ya ndugu/wanaukoo wapatao wawili (2) walihudhuria Mkutano Mkuu wa Pili wa Ukoo wa Kivenule tofauti na mwaka jana ambapo tulikuwa hatuna uwakilishi wa aina yoyote.

 

Kwa wastani uwakilishi wa ndugu/wanaukoo waliohudhuria Mkutano Mkuu wa Pili wa Ukoo wa Kivenule ulikuwa ni wa mtawanyiko zaidi. Hii kwa Umoja wa Ukoo wa Kivenule ni jambo la kufurahisha na kujivunia kwani baadhi ya malengo ya umoja huu ni kuwakusanya ndugu toka sehemu mbalimbali hapa Tanzania. Viongozi wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule bado wanaamini kuwa hawatimiza lengo lake la kuandaa mikutano ya namna hii kwani wanaamini kuwa bado kuna idadi kubwa ya ndugu ambao bado hawajapata fursa ya kuhudhuria mikutano hii. Ndiyo maana, Umoja wa Ukoo wa Kivenule bado unahamasisha ndugu wahamasishane kuhudhuria mkutano huu.

 

Vijiji ambavyo vimeonyesha mwelekeo mzuri na ambapo kwa Viongozi wa Ukoo ni mafanikio makubwa ni pamoja na Kidamali, Nyamihuu, Ilala-Simba, Nyamahana, Magubike, Idete na Nzihi. Umoja wa Ukoo wa Kivenule unadhani kuwa hii changamoto tosha kwa viongozi pamoja na ndugu/wanaukoo toka sehemu mbalimbali hapa Tanzania.

 

Chakula na vinywaji: Katika hali ya kawaida, Kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Pili wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule, chini ya uongozi wa ukoo, ilikusudia kuwapa huduma ya chakula na vinywaji ndugu/wanaukoo pamoja na wageni waalikwa wote waliohudhuria mkutano huo. Kwa ujumla, huduma hizo zimetolewa kwa kadri bajeti ilivyoruhusu. Huduma ya chakula na chai ilitolewa kwa kila mshiriki na viongozi walihakikisha kuwa kila mshiriki anapata huduma zote. Licha ya ufinyu wa bajeti uliojitokeza, huduma bora ya chakula ndiyo ilikuwa kauli mbiu yetu.

 

Bajeti: Mkutano Mkuu wa Pili wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule, umekuwa na tatizo la ufinyu wa bajeti yake. Tumeshindwa kutoa huduma zaidi mfano maji na soda wakati wote wa mkutano na badala yake, huduma hiyo imetolewa wakati wa chakula tu. Vinywaji kama soda vimeweza kutolewa mara tu tofauti na mipango na matarijio ya uongozi wa KAUKI.  Kwa ujumla Kamati ya Maandalizi chini ya Uongozi wa KAUKI, walijitahidi sana kuweka kipaumbele kwenye huduma za msingi.

 

Kwa mfano, baadhi ya huduma hazikutolewa kutokana na ufinyu wa bajeti. Ripoti ya Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule, haikuweza kudurufiwa (kutolewa nakala nyingi); kuwaleta waandishi wa habari wa magazeti, redio na televisheni; uchukuaji wa picha za video na picha za mnato.

 

Mojawapo ya malengo ya kufanya mikutano hii ni kutunza kumbukumbu hizo kwa njia mbalimbali mfano mikanda ya video, vitabu, magazeti pamoja na kuandika ripoti kama hii iliyosomwa katika Mkutano Mkuu wa Pili wa KAUKI.

 

Ufinyu wa bajeti umetufanya tuwe na aina moja tu ya utunzaji wa kumbukumbu za matukio mkutanoni. Wanaukoo ndio wachangiaji wakubwa wa bajeti zinazoaandaa mikutano hii. Kutokana na hali duni ya miahsa, tunashindwa kufikia malengo. Kwa mfano, kuna uhaba wa vitendea kazi kama kompyuta, printa, photokopi, projekta na televisheni kwa ajili ya kufundishia. Tunafikiria zaidi, kuwa na miradi ya kujijengea uwezo ambayo itasaidia uongozi wa KAUKI, kumudu baadhi ya gharama.

 

Ushiriki katika Mkutano: Kwa ujumla, ndugu/wanaukoo walishiriki kikamilifu wakati wote katika siku mbili za Mkutano Mkuu wa Pili wa KAUKI. Kamati ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Pili wa KAUKI iliteua Kamati Ndogo Ndogo zilizosaidia kuratibu shughuli zote za mkutano. Mfano, Kamati ya Mapokezi ilifanya kazi yake ipasavyo pamoja na Kamati nyingine kama Kamati ya Ulinzi na Usalama na Kamati ya Chakula. Kamati zote hizi, zilishirikiana vyema na wawezeshaji wa Mkutano Mkuu wa Pili wa KAUKI, kuhakikisha kuwa ratibu inafuatwa ipasavyo.

 

Mikutano Mikuu ya KAUKI, huendeshwa kwa kumshirikisha kila mshiriki ili kuweza kuibua hisia na mawazo toka miongoni mwa washiriki. Mikutano hii, huwa katika mfumo wa darasa, ambapo, huwepo na mchanganyiko wa matukio mfano warsha, ambapo mada mbalimbali huwasilishwa na kufundishwa, majadiliano katika vikundi hufanyika na pia mrejesho toka katika makundi huwasilishwa mbele ya washiriki.

 

Makundi huundwa kutumia njia mbalimbali ikiwemo ile ya kuhesabu namba 1 hadi 4 na kasha kugawanyika kutokana na namba walizozihesabu. Baada ya kila kundi kuwasilishwa, makundi mengine huuliza maswali au kutoa hoja au nyongeza kutokana na hisia au mawazo mbalimbali yaliyoibuliwa miongoni mwa wanakikundi. Jinsi huzingatiwa kwa kila jambo linalofanyika katika vikundi na mkutano mzima kwa ujumla.

 

Baada kila kikundi kuwasilisha, hoja zilizoibuliwa hujumuishwa na mwezeshaji na pia baadaye kuandikwa kwenye ripoti kwa ajili ya kumbukumbu na utekeleza hapo baadaye.

 

Tathmini ya Jumla: Inagusa zaidi kuzingatiwa kwa muda na ratiba katika kipindi chote cha mkutano. Kamati ya kuratibu mkutano huchangamka zaidi na kwenda sambamba na ratiba. Kwa mfano chakula na chai huandaliwa na kutolewa kwa wakati kama ratiba inavyoonyeshwa. Japo kuna matatizo ambayo hujitokeza wakati wa kuanza kwa mkutano ambapo wanaukoo/washiriki huchelewa kufika kutokana na umbali.

 

Licha ya kasoro na uhaba wa vitendea kazi, shughuli zilizopangwa kutekelezwa kwa mujibu wa ratiba, hufanyika kama ilivyopangwa. Wawezeshaji hujitahidi kufikisha ujumbe kwa hadhira (washiriki wa mkutano) kama ilivyokusudiwa kwa kutumia mbinu mbadala mfano vipaza sauti, mbao wa karatasi (flip charts), stendi ya ubao wa karatasi (flip chart stand) na kalamu za kuandikia (mark pens). Ukosefu wa kifaa cha kufundishia kwa uangavu zaidi yaani projekta huwa ni changamoto kwetu kubuni njia bora zaidi.

 

Mafanikio yanajitokeza kwa ujumla na kwa mtu mmoja mmoja kupitia mazungumzo au mahojiano. Uongozi wa Umoja wa Ukoo baada ya kuanza shughuli zake rasmi unategema kuboresha mambo mbalimbali mfano huduma za chakula na vinywaji, kupata vitenda kazi kama Kompyuta, Printa, Photokopi na Projekta. Kuboresha ofisi iliyopo kwa huduma za mawasiliano za Intaneti na pia kutafuta wafadhili wa kutusaidia kutujengea uwezo na kutupatia vifaa vya kufanyia kazi.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

SHUKRANI

Kama ilivyo desturi mwisho wa mikutano mikuu iliyokwisha tangulia, wana-KAUKI hupata fursa ya kuzungumza machache (shukrani) kuhusiana na yote yaliyofanyika na kujitokeza katika mkutano. Shukrani huwa katika mitindo mbalimbali; mfano changamoto, motisha, fundisho na elimu. Uongozi wa KAUKI huzitumia shukrani hizo kurekebisha au kuboresha baadhi ya mambo ambayo yalionesha udhaifu na pia kuimarisha yale ambayo yalionesha mafanikio.

 

Katika mkutano mkuu wa tatu wa KAUKI, jumla ya wajumbe wanne walitoa salaam zao za shukrani. Wajumbe hao ni Bwana Atanas Mbunza, Gipson Kitu, Mama Neema (Anyesi Kivenule) na Jermana Mhapa.

 

Bwana Anatas Mbunza (Kidamali): Mikutano ya KAUKI imepata nguvu kutokana na uelewa miongoni mwa wana-KAUKI kuongezeka. Wigo wa kutambuana umepanuka. Kwenda kuufanyia Mkutano Mkuu wa Nne wa KAUKI Ilole ni hatua ya maendeleo. Watu wengi hawapajui Ilole. Pia mikutano hii imekuwa ni fursa ya kujifunza mfano KAUKI kuwa na mtandao [http://www.tagumtwafoundation.wetpaint.com] na pia wana-KAUKI wenyewe kujua maana ya mtandao (website) ni maendeleo. Kuna umuhimu wa kuisajili KAUKI kutokana na faida mbalimbali zilizokwisha bainishwa na viongozi.

 

Gipson Kitu (Nduli): Yeye ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuhudhuria mikutano ya namna hii (Mikutano Mikuu ya KAUKI). Huu ulikuwa ni Mkutano Mkuu wa Tatu wa KAUKI. Anawashukuru viongozi wa KAUKI kwa kazi nzuri na ngumu ya kuitumikia KAUKI. Anatambua ugumu wa kazi hii ya kiutendaji na mazingira halisi ya kiutendaji. Alimshukuru pia mwezeshaji (Stephan Mhapa) aliyewasilisha mada ya: CHANGAMOTO ZA KAUKI KUJILETEA MAENDELEO. Pia alitumia fursa hiyo kuwashukuru wanaukoo (wana-KAUKI) kwa ujumla jinsi wanalivyofanikisha kufanyika kwa mkutano huo.

 

Bwana Gipson alitoa changamoto na kusisitiza kuwa tuyategemee mabaya. Akinukuu katika vitabu vya Ala, alisema; hata ukiwa muumini mzuri, utegemea shetani siku moja atakujaribu. Jambo la msingi kuwa imara. Anaamini hatutaweza kuyumbishwa kamwe na watu baki, alimalizia.

 

Mama Neema (Anyesi Kivenule-Magubike): alifurahishwa sana na jinsi mkutano ulivyoendeshwa na pia watu wanavyojitoa, na mambo yote yanayotokea na kutendeka katika mikutano hii. Anasikitika kwa kuwa umri wake ni mkubwa. Angetamani arudi udogoni (awe mtoto); angefanya mambo makubwa hata ikibidi kufika Ulaya (yaani amechelewa) kwa sababu enzi zake mambo haya hayakufanyika. Anawasikitia wale walioshindwa kuhudhuria bila sababu za msingi. Wamekula harasa katika nyanja zote yaani elimu iliyopatikana katika shughuli za kiuchumi, kimaendeleo na kibiashara ni kubwa na kweli inafunza.

 

Mapato tunayoyakusanya ni finyu mno, angetamani katika Mkutano Mkuu wa Nne wa KAUKI, mapato yaboreke. Tuonyeshe mabadiliko katika makusanyo yetu. Kiwango cha makusanyo kiboreke. Angetamani kuzirudisha gharama zote za mkutano, lakini kwa sababu hali yake kiuchumi ni duni hatoweza. Yeye binafsi anajiona ananza maisha mapya katika hali yoyote ile ambayo itaboresha mfuko wa KAUKI. Angefurahi sana kama mambo yangeenda vizuri na hivyo kutoa fursa nyingine za kusaidiwa. Msisitizo wake ni katika kuboresha elimu, alimaliza.

 

Jermana Mhapa (Kidamali): Amekuwa ni chachu ya mafanikio ya Mikutano ya KAUKI. Kama Mwenyekiti wa Kamati ya Chakula, anasema “anashukuru kwa sababu hamna hata mshiriki mmoja ambaye hakupata chakula”. Alitumia fursa hiyo kuwashukuru viongozi wa KAUKI kwa kuweka taarifa mbalimbali hususani za kauki katika mtandao wa Intaneti. Aliwashuruku washiriki toka Dar es Salaam kwa kufanikisha kuweka taarifa ya Mkutano wa 2005 na 2006 katika mtandao (website). Shukrani pia ziwaendea wale wote walioshughulika pamoja naye katika kamati ya chakula kwa sababu walijitoa sana kuhakikisha maandalizi na utoaji wa huduma hiyo unaenda vizuri.

 

Mwishowe alitoa ombi kwa wanaukoo wote waliohudhuria mkutano huo; alisema kila mtu ana wazo japokuwa ametokea sehemu tofauti na pale ulipofanyika mkutano (Kidamali). Si vyema mtu akajiona ni mgeni katika eneo hili la Kidamali. Maadamu sisi sote ni ndugu, hapa ni nyumbani pa kila mtu. Kufanikiwa kwa mikutano hii kunategemea jitihada za kila mmoja wetu. Ni vyema siku nyingine, mahali potote, shughuli za maandalizi ya utoaji wa huduma yoyote katika mikutano liwe ni jukumu la kila mshiriki wa mkutano, kwa manufaa na mafanikio ya mikutano hii, alimaliza.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

VIAMBATANISHO

MAHUDHURIO KWENYE MKUTANO MKUU WA TATU WA UKOO WA KIVENULE

JINA KAMILI

MAHALI UNAPOISHI

ANUANI/SIMU

1.        IGNUS P. KIVENULE

DAR ES SALAAM

P.O. BOX 70112, DAR ES SALAAM

0787260971,0712949977

2.       IRENE KIVENULE

MUFINDI

0755703430

3.       VICKY I. KIVENULE

DAR ES SALAAM

0786282521

4.       FRIDA KIVENULE

MGONGO

P.O. BOX 1777, MGONGO

5.       AUGUSTINO KIVENULE

MGONGO

P.O. BOX 1777, MGONGO

6.       KASTILIA NZALA

MAGUBIKE

P.O. BOX 108, MAGUBIKE

7.       DALIA MGAYA

MAGUBIKE

P.O. BOX 108, MAGUBIKE

8.       EDIMELI NZALA

MAGUBIKE

P.O. BOX 108, MAGUBIKE

9.       AMALIA KIVENULE

ILOLE

P.O. BOX 250, ILOLE

10.   FRANK KIVENULE

DAR ES SALAAM

0754749889

11.      GEORGE KIVENULE

KIDAMALI

0787826614

12.    TEUDUS KIVENULE

MAGUBIKE

P.O. BOX 1243, MAGUBIKE

13.    BONIFAS NZALA

MAGUBIKE

P.O. BOX 1243, MAGUBIKE

14.    ANNA KIVENULE

NDULI

P.O. BOX 289, KIDAMALI

15.    JOVIN KIVENULE

KIDAMALI

0786085874

16.    GREISON KILASI

MAGUBIKE

0786356869

17.     ELIAS MDONGWE

KIDAMALI

P.O. BOX 772, KIDAMALI

18.     DANIEL KIVENULE

KIDAMALI

KIDAMALI

19.    VITUS NZALA

MAGUBIKE

P.O. BOX 108, MAGUBIKE

20.  ARUNA NGENG’ENA

MAGUBIKE

P.O. BOX 1243, MAGUBIKE

21.    HUZUNI KIVENULE

NDULI

P.O. BOX 289, NDULI

22.   ANETA KIVENULE

NDULI

P.O. BOX 289, NDULI

23.   EDWIN NZALA

MAGUBIKE

P.O. BOX 1243, MAGUBIKE

24.   ESTELINA P. KIVENULE

ILOLE

P.O. BOX 250, ILOLE

25.   BENARD KIVENULE

ILOLE

P.O. BOX 250, ILOLE

26.   DAVID F. KIVENULE

MAGUBIKE

0787824099

27.   CHELINA NYAKUNGA

ILOLE

P.O. BOX 289, NDULI

28.   PIUS KIVENULE

ILOLE

0786524578

29.   JOHN KIVENULE

KILOMBERO

0784332354

30.  ADAM KIVENULE

DAR ES SALAAAM

0713270364/0784270364

31.    FAUSTINO KIVENULE

KIDAMALI

0787626185

32.   WILLIAM KIVENULE

KIDAMALI

S.L.P. 193, KIDAMALI

33.   JESCA KIVENULE

MAGUBIKE

S.L.P. 108, MAGUBIKE

34.   LUSI KIVENULE

MAGUBIKE

S.L.P. 108, MAGUBIKE

35.   AGATA KIVENULE

MAGUBIKE

S.L.P. 108, MAGUBIKE

36.   KRISTIAN KIVENULE

MOROGORO

0784380195/0714146382

37.   JANETH KIVENULE

KIDAMALI

S.L.P. 145, KIDAMALI

38.   KALOLINA KIVENULE

KIDAMALI

0787344925

39.   MALIA NGUVILA

KIDAMALI

0787826614

40.  MELINA MBWILO

KIDAMALI

0786213760

41.    CATHELINI NGAHETWA

KIDAMALI

0787626185

42.   HURUMA CHUNGULA

KIDAMALI

0787843563

43.   JELITA MUVELA

KIDAMALI

S.L.P. 742, KIDAMALI

44.   FAUSTINA MSIGALA

KIDAMALI

S.L.P. 742, KIDAMALI

45.   KONJETA KIVENULE

MAGUBIKE

S.L.P. 108, MAGUBIKE

46.   ATANAS MBUNZA

KIDAMALI

0784451891

47.   INNOCENT MALAMBO

KIDAMALI

0784472643

48.   SEVELINI NYANGALIMA

MAGUBIKE

0787104990

49.   JERUMANA MHAPA

KIDAMALI

0784470734

50.  PONSIANO KIVENULE

KIDAMALI

S.L.P. 108, MAGUBIKE

51.    DAVIDIKA NZALA

MAGUBIKE

S.L.P. 108, MAGUBIKE

52.   YUSTINA NZALA

MAGUBIKE

S.L.P. 108, MAGUBIKE

53.   RUKIA NZALA

MAGUBIKE

S.L.P. 108, MAGUBIKE

54.   MADESTA KIVENULE

MAGUBIKE

S.L.P. 108, MAGUBIKE

55.   NESIA KIVENULE

MABUGIKE

S.L.P. 108, MAGUBIKE

56.   ANJETINA KIVENULE

MAGUBIKE

S.L.P. 108, MAGUBIKE

57.   EMMANUEL L. KIVENULE

MAGUBIKE

S.L.P. 108, MAGUBIKE

58.   DOMINICUS KIVENULE

MAGUBIKE

S.L.P. 108, MAGUBIKE

59.   JOHN MGOMBA

KIDAMALI

S.L.P. 108, KIDAMALI

60.  JOHN MKWAMBE

KIDAMALI

0787008035

61.    ANYESI KIVENULE

MAGUBIKE

MAGUBIKE

62.   ANAMARIA KIDENYA

IGOWOLE

S.L.P. 28, IGOWOLE

63.   ANJELIKA MADUGA

KIDAMALI

S.L.P. 108, KIDAMALI

64.   MUSA KIVENULE

NDULI

S.L.P. 129, NDULI

65.   DAUDI NYAKUNGA

KIDAMALI

S.L.P. 108, MAGUBIKE

66.   STANI SINGAILE

KIDAMALI

0784536692

67.   JUSTIN KIVENULE

KIDAMALI

KIDAMALI, IRINGA

68.   LUJINA KIVENULE

NYAMAHANA

NYAMAHANA, IRINGA

69.   HAMISI MAPEMBE

KIDAMALI

S.L.P. 193, KIDAMALI

70.  GIBSON KITU

ILOLE

0762005699

71.     FREI NYWALE

KIDAMALI

S.L.P. 742, KIDAMALI

72.   TANFOD FUNGO

KIDAMALI

S.L.P. 193, KIDAMALI

73.   AMANI MBUNZA

KIDAMALI

S.L.P. 193, KIDAMALI

74.   DOLISI KIVENULE

KIDAMALI

KIDAMALI, IRINGA

75.   GWELINO SINGAILE

IRINGA-MJINI

0755772594

76.   GRACE KIVENULE

KALENGA

S.L.P. 225, KALENGA

77.    REHANI KIVENULE

MAGUBIKE

S.L.P. 108, MAGUBIKE

78.    SHABAN SASA

KIDAMALI

KIDAMALI, IRINGA

79.   AGNESI KIVENULE

KIDAMALI

KIDAMALI, IRINGA

80.  MARINO KIVENULE

KIDAMALI

S.L.P. 109, KIDAMALI

81.     RICHINI KIVENULE

KIDAMALI

KIDAMALI, IRINGA

82.   ZUWENA KIVENULE

KIDAMALI

KIDAMALI, IRINGA

83.   MALTINA KALINGA

KIDAMALI

KIDAMALI, IRINGA

84.   MARIA MBUNZA

KIDAMALI

0784451891

85.   BEATRICE NYAMWANGI

KIDAMALI

KIDAMALI

86.   JOSEPHAT LUPOLA

MAGUBIKE

S.L.P. 642, MAGUBIKE

87.    JUSTIN D. KIVENULE

KIDAMALI

0787843561

88.    MFALINGUNDI NGENG’ENA

MAGUBIKE

P.O. BOX 108, MAGUBIKE

WATOTO

89.   KRELIA KIVENULE

 

 

90.  AGAPE KIVENULE

 

 

91.    AIVON KIVENULE

 

 

92.   BAKHITA KIVENULE

 

 

93.   SILENI KIVENULE

 

 

94.   GELASIA KIVENULE

 

 

95.   TASMILI KIVENULE

 

 

96.   KEVIN KIVENULE

 

 

97.   FESTO KIVENULE

 

 

98.   GLOLIA KIVENULE

 

 

99.   FARIDA SASA

 

 

100.          HUSSEIN SASA

 

 

101. SALUM SASA

 

 

102.           MWANAIDI SASA

 

 

103.           TAITANA NZALA

 

 

104.           JELIDA NZALA

 

 

105.           MACHELINA NZALA

 

 

106.           BENADETA KIVENULE

 

 

107.            FARIDA MAKSI

 

 

108.            EDWIN MHAPA

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

RATIBA YA MKUTANO MKUU WA TATU WA UMOJA WA UKOO WA KIVENULE

RATIBA YA MKUTANO MKUU WA TATU WA KAUKI

SIKU YA KWANZA

30 Juni 2007

Muda

Shughuli/Jukumu

Wahusika

12.00 – 12.45

Wageni Wote Kuamka na Kufanya Maandalizi ya Kuingia kwenye Mkutano

Wote

12.45 – 01.15

Kupata Kifungua Kinywa

Washiriki wote

01:15 – 02:00

Kuwasili Mkutanoni na Kujisajili na kupata vitambulisho

Washiriki wote

02.00 – 02.20

Kusoma Hotuba ya Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Pili wa Ukoo wa

Mwenyekiti wa KAUKI

02.20-02.45

Ufunguzi Rasmi wa Mkutano na Mgeni Rasmi

Mgeni Rasmi

02.45-03.15

Utambulisho baina wa Ndugu na Wageni Waalikuwa

Wote

03.15 – 04:00

Mada: CHIMBUKO NA HISTORIA YA UKOO

(a). Washiriki wasambaziwe nakala ya muundo wa Ukoo na kasha kuujadili na kutoa mawazo yao

1.                    Mwakilishi - Kidamali

2.                 Mwakilishi toka Ilole

3.                 Washiriki wote

04:00 – 04:30

Pumziko la Chai / Kahawa/Maji

Washiriki Wote

04.30-04.45

Mada Inaendelea.

(b). Washiriki waijadili mada na kutoa mapendekezo

(c). Washiriki waijadili mada na kupendekeza nini kifanyike kutunza kumbukumbu hizo

(d). Washiriki wazijadili njia mbadala za kutunza taarifa zinazohusiana na ukoo

Wawezeshaji na Washiriki wote

04.45-05.05

Kuwasilisha majadiliano katika Makundi

Washiriki wote na Wawezeshaji

05.05-05.30

Majumuisho ya yote yaliyojitokeza katika Mada

Wawezeshaji

05:30 – 06:30

TAARIFA YA UTENDAJI WA KAUKI:

1. Mipango na Shughuli zilizokusudiwa kufanywa na KAUKI 2006/2007;

2. Taarifa ya Utendaji kwa Ujumla;

3. Taarifa ya Mahesabu na Fedha; na

4.                   Mafanikio na Matatizo ya KAUKI

4. Matarajio ya KAUKI 2007/2008

Katibu Mkuu

Makamu wa Katibu

Mhasibu

06.30 – 07.00

TAARIFA YA SHUGHULI ZA MAENDELEO KATIKA KANDA

1. Uhamasishaji

2. Mwitikio wa Jamii inayounda Ukoo

3. Ushirikiano miongoni mwa wanajamii

4. Mafanikio na Matatizo

Viongozi wa Kanda zote

07.00-08.00

CHAKULA CHA MCHANA

Washiriki wote

8:00 – 8:45

KUSOMA RIPOTI YA MKUTANO MKUU WA PILI WA KAUKI

Kujadili Mapungufu, Kutoa Ushauri, Nyongeza

Kupitisha Ripoti

1.                    Katibu Mkuu

2.                   Katibu Msaidizi

3.                   Washiriki wote

08:45 – 09:15

Salaam mbalimbali kutoka kwa Washiriki wa Mkutano Mkuu (Wastani watu 6 na dakika @ 5)

Washiriki wa Mkutano

09:15– 09:45

Pumziko la Chai/Kahawa/Maji

Washiriki wote

09.45 -11:00

Uzoefu wa wanaukoo katika shughuli za maendeleo

1.Kidamali/Magubike: Kilimo cha Nyanya /Tumbaku na shughuli nyingine za kiuchumi dakika 25

2. Ilole/Nduli/Kigonzile/Mgongo: Uzoefu wa Shughuli za Kiuchumi dakika 25

3. Dar/ Morogoro/ Kilombero / Moshi dakika 15

4. Maeneo Mengine

Washiriki wote; viongozi wa Kanda au wajumbe watakaochaguliwa kutoa uzoefu wa shughuli hizo za kiuchumi

11.00

KUAHIRISHA MKUTANO

Mwenyekiti wa KAUKI

2:30 – 6:30 Usiku

Burudani (Muziki wa Kisasa na Ngoma za Asili), vinywaji, kufahamiana zaidi na kubadilisha mawazo

Wanaukoo wote


 

SIKU YA PILI

01 Julai 2007

Muda

Shughuli/Jukumu

Wahusika

12.00 – 12.45

Wageni Wote Kuamka na Kufanya Maandalizi ya Kuingia kwenye Mkutano

Wote

12.45 – 01.15

Kupata Kifungua Kinywa

Washiriki wote

01:15 – 02:00

Kuwasili Mkutanoni na Kujisajili

Washiriki wote

02.00-02.45

MADA: CHANGAMOTO ZA KAUKI KUJILETEA MAENDELEO

1.Nini kifanyike wana KAUKI kujiletea Maendeleo?

2. Mnadhani ni vitu gani vipewe Kipaumbele kwa wanaukoo kunufaika na KAUKI!

3. Baadhi ya Malengo ya KAUKI ambayo mnayafahamu mnadhani yatasaidia kuleta mabadiliko? Na ni kwa namna gani? Jadili

4. KAUKI ni sehemu tu ya vikundi vingi vinavyofanya jitihada za kujiinua kiuchumi na kimaendeleo, mnadhani ni changamoto gani tunaipata ukilinganisha na mafanikio au matatizo ambayo yamevipata vikundi vingine? Yajadili na kuyatoa mapendekezo hayo

Wawezeshaji na washiriki wote

02.45-03.15

Majadiliano katika Makundi

Washiriki wote wagawanyike katika makundi

03.15-03.45

Makundi kuwasilisha hoja kutoka katika makundi yao

 

Washiriki wote

03.45-04.30

Majumuisho ya yote yaliyojitekeza katika Mada

Wawezeshaji

04:30 – 05:00

Pumziko la Chai / Kahawa/Maji

Washiriki Wote

05.00-06.00

MAJADILIANO YA HOJA MBALIMBALI AMBAZO ZIMEWASIISHWA NA WASHIRIKI WA MKUTANONI

1.

2.

3.

4.

5.

6.

7.

Washiriki wote na Viongozi wa KAUKI

06.00-07.00

MAHITAJI YA KAUKI NA JINSI YA KUFANIKISHA KUPATIKANA KWA MAHITAJI HAYO

1.

2.

3.

4.

5.

6.

7.

8.

Washiriki na Viongozi wa KAUKI

 

07.00-08.00

CHAKULA CHA MCHANA

Washiriki wote

08:00–09.00

UCHAGUZI WA VIONGOZI WA KAMATI NDOGO NDOGO PAMOJA NA VIONGOZI WA KANDA

1. Kamati ya Mipango na Maendeleo

-Mwenyekiti:

-Katibu

2. Kamati ya Mahesabu na Fedha

-Mwenyekiti:

-Katibu

4.       Kamati ya Nidhamu na Maadili

-Mwenyekiti:

-Katibu

4. Kamati ya Maafa na Matatizo

-Mwenyekiti:

-Katibu

Viongozi wa Kanda

1.                                2.

3.                                4.

 

Washiriki wote na Viongozi

 

09:00–09:30

Pumziko la Chai/Kahawa/Maji

Washiriki wote

09.30-11:00

MAJUMUISHO NA TATHMINI YA MKUTANO

MIPANGO NA MIKAKATI YA MBELENI

KUTANGAZWA KWA TAREHE YA MKUTANO MKUU WA NNE

SHUKRANI

KUFUNGA MKUTANO

VIONGOZI WA KAUKI NA Washiriki wa Mkutano Mkuu

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Mawasiliano na Kanda za Ukoo wa Kivenule

Magubike

1.        Vitus Nzala

2.       Severine Nyangalima

0787 104990

 

Nduli

1.        Augustino Kivenule

2.       Gibsoni Kitu

0762 005699

 

Ilole

1.        Pius Kievnule

0786 524571

 

Kidamali

1.        George Kivenule

0787 826614

 

Mufindi

1.        Irene Kivenule

2.       Gloria Kivenule

0786 282553

 

 

 

No comments:

Post a Comment