Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Wednesday 9 January 2013

SAFARI YA MWISHO YA FLOMINA KIVENULE

MAZISHI YA MAREH FLOMINA KIVENULE

 enzi ya uhai wakeHuko nyumbani kwa marehemu, Ibada fupi ya kumwombea ilifanyika, pamoja na kutoa heshima za mwisho kwa ndugu, jamaa na marafiki waliojumuika nyumbani hapo. 

Hatimaye, mwili wa Marehemu Flomina Kivenule ulisafirisha siku ya Jumamosi ya tarehe 29 Desemba 2012 kwenda Kijijini kwa Mumewe Mbuta huko Igula Mkoani Iringa. Awali kabla ya mwili huo kusafirishwa, kulikuwa na mipango ya ama kumzika Ilula au hapa Jijini Dar es Salaam.

Mume wa Marehemu aliiomba familia ya upande wa marehemu kumruhusu kwenda kumzika mpendwa wake huko kwao Kijijini Igula. Ombi la Mume wa marehemu lilikubaliwa na hivyo safari kuelekea Iringa kuanza mnamo wa saa moja kasoro jioni.

Huko Iringa, mwili wa marehemu uliwasili majira ya saa moja asubuhi ambapo ndugu mbalimbali wa marehemu kutoka Ilula, Magubike na Kidamali walipata fursa ya kushirikiana na ndugu wengine waliotoka Dar es Salaam katika kumsindikiza Flomina Kivenule katika safari yake ya milele.

Mwenyezi Mungu ailaze Roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi, Amina.

Imeandaliwa na:


Adam Kivenule

Katibu - KAUKI


PICHA ZA KUMBUKUMBU ZA MAREHEMU FLOMINA KIVENULE

Hizi ni baadhi ya kumbukumbu za Mareh Flomina Kivenule katika uhai wake. Matukio mengine ya picha yataletwa.



Marehemu Flomina Kulia ambaye ni shangazi yake na Lemija Mkini Kushoto wakati wa vikao vya harusi vya ndugu Adam Alphonce Sigatambule Kivenule, Chonya Inn, Ubungo Riverside Jijini Dar es Salaam


Marehemu Flomina Kulia ambaye ni shangazi yake na Lemija Mkini Kushoto wakati wa vikao vya harusi vya ndugu Adam Alphonce Sigatambule Kivenule, Chonya Inn, Ubungo Riverside Jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment