Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla

Mchakato wa Kuandaa Kitabu cha Chimbuko, Muundo na Historia ya Ukoo wa Kivenule na Uhehe kwa Ujumla
Karibu uone yale ambayo KAUKI inafanya

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014

Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI, 2014
Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule (2005 - 2009)

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI

Mkutano Mkuu wa10 wa KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Thursday 24 January 2013

TAARIFA KWA UMMA WA WANA-KAUKI NA JAMII KWA UJUMLA


Umoja wa Ukoo wa Kivenule-KAUKI
TAARIFA KWA UMMA WA WANA-KAUKI NA JAMII KWA UJUMLA

Katibu Mkuu wa KAUKI
Uongozi wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) kwa heshima na taadhima unautambua na pia kuwapongeza wote waliojitoa kwa hali na mali katika kipindi cha miaka 8 tangu mikutano hii ilipoanza kufanyika mwaka 2005.

Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 9 wa KAUKI, unaenda sambamba na kuangalia mafanikio na changamoto mbalimbali ambazo KAUKI inaendelea kukumbana nazo. Lakini katika maisha yeyote ya binadamu, mafanikio na changamoto huenda pamoja.

Mafanikio makubwa ambayo KAUKI imeyapata kwa kipindi cha miaka 8 ni pamoja na:

  1. Kuwaunganisha Wanaukoo kutoka maeneo ya Kidamali, Nduli, Magubike, Igominyi, Nduli, Ilalasimba, Kalenga, Mufindi, Irore, Nyamahana, Mgongo, Nyamihuu, Idodi, Idete, Mufindi, Iringa Mjini, Itagutwa, Mtera, Morogoro, Kilombero, Dar es Salaam na Dodoma. Watu wengi wameweza kufahamiana tofauti na mwanzo.
  2. Kufahamiana baina yetu pia kumetufanya tujitambue na pia kuona athari ya kuingiliana majina kutokana na uwingi wetu. Ushirikiano umeanza kuonekana katika matukio mbalimbali ya Kijamii. Blogu yetu ya http://www.tagumtwa.blogoak.com imekuwa ni kiunganishi kikubwa kwa sababu taarifa mbalimbali zimeanza kusambazwa.
  3. Ushirikiano na upendo wa dhati baina yetu sasa umeanza kuonekana, na tunashirikiana katika shida na raha.
  4. Wachache wetu wamekuwa mstari wa mbele katika kuchangia Mfuko wa KAUKI na Mikutano Mikuu. Ombi letu ni kuwahamasisha wengine nao wachangie Mfuko wa KAUKI na hususani Mkutano Mkuu wa Tisa wa KAUKI, ambapo kwa mwaka huu utafanya uchaguzi wa viongozi na pia kuzindua ofisi yake Kidamali kama mipango ya ujenzi itaenda vizuri kama ilivyokubalika katika Mkutano Mkuu wa 8 wa KAUKI uliofanyika Jijini  Dar es Salaam, mwezi Juni 2012.
  5. Fanikio jingine muhimu ni kufanikiwa kutengeneza Muundo wa Ukoo (Clan Structure) yenye kurasa karibu ya 80. Kila mwana KAUKI atapata nakala yake Wakati wa Mkutano Mkuu wa 9 wa KAUKI itakayofanyika Kijijini Kidamali. Inaonesha toka kizazi hiki kilipoanza hadi sasa…, pamoja na taarifa mbalimbali kuhusiana na Kabila la Wahehe zitatolewa.

Hima tunawaomba ndugu, jamaa na marafiki wenye moyo wa kweli wa kuisaidia jamii inayotahidi kujisaidia kutuunga mkono katika mchakato huu. Mfuko wa KAUKI una malengo mengi, ripoti zilizomo kwenye blogu zinaeleza vizuri. Lakini pia unaweza kuwasiliana na viongozi wa KAUKI kupitia anuani yao: tagumtwa-kauki@gmail.com  au tagumtwa@gmail.com na simu 0713 270364

Kwa taarifa mbalimbali unaweza kuzipata kupitia blogu http://www.tagumtwa.blogoak.com

 
Imeandaliwa na kutolewa kwa niaba ya uongozi na:

 

Adam Alphonce Sigatambule Tavimyenda Tagumtwa Kivenule

KATIBU KAUKI


 

 

 

 

No comments:

Post a Comment